< 1 Samuel 30 >

1 Le troisième jour, David et ses hommes arrivèrent à Tsiklag. Les Amalécites avaient fait une incursion dans le Sud et à Tsiklag, ils avaient frappé Tsiklag et l'avaient incendiée,
Daudi na watu wake wakafika Siklagi siku ya tatu. Basi Waamaleki walikuwa wamevamia Negebu na Siklagi. Wakawa wameshambulia mji wa Siklagi na kuuteketeza kwa moto,
2 et ils avaient fait prisonniers les femmes et tous ceux qui s'y trouvaient, petits et grands. Ils n'en tuèrent aucun, mais les emportèrent et s'en allèrent.
nao wakawa wamewachukua mateka wanawake pamoja na wote waliokuwamo humo, vijana na wazee. Hawakuua yeyote, bali waliwachukua wakaenda zao.
3 Lorsque David et ses hommes arrivèrent à la ville, voici qu'elle était brûlée par le feu; leurs femmes, leurs fils et leurs filles avaient été emmenés captifs.
Daudi na watu wake walipofika Siklagi, wakakuta mji umeangamizwa kwa moto na wake zao pamoja na wana wao na binti zao wamechukuliwa mateka.
4 Alors David et le peuple qui était avec lui élevèrent la voix et pleurèrent jusqu'à ce qu'ils n'aient plus la force de pleurer.
Hivyo Daudi na watu wake wakapiga yowe mpaka wakaishiwa na nguvu za kulia.
5 Les deux femmes de David furent emmenées en captivité: Ahinoam, la Jizreelite, et Abigaïl, la femme de Nabal, le Carmélite.
Wake wawili wa Daudi walikuwa wametekwa: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli.
6 David était dans une grande angoisse, car le peuple parlait de le lapider, car l'âme de tout le peuple était affligée, chacun pour ses fils et pour ses filles; mais David se fortifiait en Yahvé, son Dieu.
Daudi alihuzunika sana kwa sababu watu walikuwa wakisemezana juu ya kumpiga kwa mawe. Kila mmoja alikuwa na uchungu rohoni kwa sababu ya wanawe na binti zake. Lakini Daudi akajitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.
7 David dit au prêtre Abiathar, fils d'Ahimélec: « Apporte-moi l'éphod, je te prie. » Abiathar apporta l'éphod à David.
Kisha Daudi akamwambia kuhani Abiathari mwana wa Ahimeleki, “Niletee kisibau.” Abiathari akamletea,
8 David consulta Yahvé en disant: « Si je poursuis cette troupe, l'atteindrai-je? » Il lui répondit: « Poursuis, car tu les rattraperas sûrement, et tu les récupéreras tous sans faute. »
naye Daudi akamuuliza Bwana, “Je, nifuatie kundi hili la wavamizi? Je, nitawapata?” Bwana akajibu, “Wafuatie. Hakika utawapata na utafanikiwa kuwaokoa.”
9 Et David partit, lui et les six cents hommes qui étaient avec lui, et il arriva au torrent de Besor, où étaient restés ceux qui étaient restés en arrière.
Daudi pamoja na watu wake 600 wakafika kwenye Bonde la Besori, mahali ambapo wengine waliachwa nyuma,
10 David poursuivit sa route avec quatre cents hommes, car deux cents hommes restèrent en arrière, qui étaient si faibles qu'ils ne purent franchir le torrent de Besor.
kwa kuwa watu 200 walikuwa wamechoka sana kuweza kuvuka hilo bonde. Lakini Daudi pamoja na watu 400 wakaendelea kufuatia.
11 Ils trouvèrent un Égyptien dans les champs, l'amenèrent à David, lui donnèrent du pain, et il mangea, et lui donnèrent de l'eau à boire.
Wakamkuta Mmisri katika shamba fulani, nao wakamleta kwa Daudi. Wakampa huyo Mmisri maji ya kunywa na chakula;
12 Ils lui donnèrent un morceau d'un gâteau de figues et deux grappes de raisins secs. Quand il eut mangé, son esprit revint à lui, car il n'avait pas mangé de pain ni bu d'eau depuis trois jours et trois nuits.
kipande cha andazi la tini na andazi la zabibu zilizokaushwa. Akala naye akapata nguvu, kwa kuwa hakuwa amekula chakula chochote wala kunywa maji kwa siku tatu usiku na mchana.
13 David lui demanda: « A qui appartiens-tu? D'où viens-tu? » Il dit: « Je suis un jeune homme d'Égypte, serviteur d'un Amalécite; mon maître m'a abandonné, car il y a trois jours, je suis tombé malade.
Daudi akamuuliza, “Wewe ni wa nani, na umetoka wapi?” Akajibu, “Mimi ni Mmisri, mtumwa wa Mwamaleki. Bwana wangu alinitelekeza nilipougua siku tatu zilizopita.
14 Nous avons fait une incursion dans le sud des Kéréthiens, dans ce qui appartient à Juda et dans le sud de Caleb, et nous avons brûlé Ziklag par le feu. »
Tulivamia Negebu ya Wakerethi, na nchi ya Yuda, na Negebu ya Kalebu. Nasi tulichoma moto Siklagi.”
15 David lui dit: « Veux-tu me faire descendre dans cette troupe? » Il lui dit: « Jure-moi par Dieu que tu ne me tueras pas et que tu ne me livreras pas aux mains de mon maître, et je te ferai descendre dans cette troupe. »
Daudi akamuuliza, “Je, unaweza kuniongoza kufikia kundi hili la uvamizi?” Akajibu, “Niapie mbele ya Mungu kwamba hutaniua wala kunikabidhi mikononi mwa bwana wangu, nami nitakupeleka hadi waliko.”
16 Quand il l'eut fait descendre, voici qu'ils se répandirent sur toute la surface du sol, mangeant, buvant et dansant, à cause de tout le grand butin qu'ils avaient enlevé du pays des Philistins et du pays de Juda.
Akamwongoza Daudi mpaka mahali walipokuwa, nao walikuwa wametawanyika eneo lote, wakila, wakinywa na wakifanya karamu kwa sababu ya nyara nyingi walizochukua kutoka nchi ya Wafilisti na kutoka Yuda.
17 David les frappa depuis le crépuscule jusqu'au soir du jour suivant. Pas un seul d'entre eux n'en sortit, à l'exception de quatre cents jeunes gens qui montèrent sur des chameaux et s'enfuirent.
Daudi akapigana nao kuanzia machweo ya jua hadi kesho yake jioni, na hakuna yeyote miongoni mwao aliyetoroka, isipokuwa vijana wanaume 400 waliopanda ngamia na kutoroka.
18 David récupéra tout ce que les Amalécites avaient pris, et il sauva ses deux femmes.
Daudi akarudisha kila kitu Waamaleki walikuwa wamechukua, pamoja na wake zake wawili.
19 Il ne leur manquait rien, ni petit ni grand, ni fils ni filles, ni butin, ni rien de ce qu'ils avaient pris. David les ramena tous.
Hakuna chochote kilichopotea: kijana au mzee, mvulana au msichana, nyara au kitu kingine chochote walichokuwa wamechukua. Daudi akarudisha kila kitu.
20 David prit tous les troupeaux de bœufs et de vaches, qu'ils conduisirent devant les autres bêtes, et il dit: « Voici le butin de David. »
Akachukua makundi yote ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, nao watu wake wakawaswaga wanyama hao mbele ya wanyama wengine wa kufugwa, wakisema, “Hizi ni nyara za Daudi.”
21 David arriva auprès des deux cents hommes qui étaient si faibles qu'ils ne pouvaient pas suivre David, qu'ils avaient aussi fait séjourner au torrent de Besor; et ils sortirent à la rencontre de David et du peuple qui était avec lui. Lorsque David s'approcha du peuple, il le salua.
Kisha Daudi akafika kwa wale watu 200 waliokuwa wamechoka sana kumfuata na ambao waliachwa nyuma kwenye Bonde la Besori. Wakatoka kwenda kumlaki Daudi na wale watu aliokuwa nao. Daudi na watu wake walipowakaribia, akawasalimu.
22 Alors tous les méchants et les vauriens de ceux qui étaient allés avec David prirent la parole et dirent: « Parce qu'ils n'ont pas marché avec nous, nous ne leur donnerons rien du butin que nous avons récupéré, si ce n'est à chacun sa femme et ses enfants, afin qu'il les conduise et s'en aille. »
Lakini watu wote waovu na wakorofi miongoni mwa wafuasi wa Daudi wakasema, “Kwa sababu hawakwenda pamoja nasi, hatutagawana nao nyara tulizorudisha. Lakini, kila mtu aweza kuchukua mkewe na watoto wake na kuondoka.”
23 David dit alors: « N'agissez pas ainsi, mes frères, avec ce que l'Éternel nous a donné, qui nous a préservés et qui a livré entre nos mains la troupe qui était venue contre nous.
Daudi akajibu, “La hasha, ndugu zangu, kamwe hamwezi kufanya hivyo kwa kile ambacho Bwana ametupatia. Yeye ametulinda na kuweka mikononi mwetu majeshi yale yaliyokuja kupigana dhidi yetu.
24 Qui vous écoutera dans cette affaire? Car, de même que sa part est celle de celui qui descend au combat, de même sa part sera celle de celui qui reste avec les bagages. Ils auront la même part. »
Ni nani atasikiliza yale mnayosema? Fungu la mtu aliyekaa na vyombo litakuwa sawa na la yule aliyekwenda vitani. Wote watashiriki sawa.”
25 Il en fut ainsi à partir de ce jour, et il en fit une loi et une ordonnance pour Israël jusqu'à ce jour.
Daudi akafanya hili liwe amri na agizo kwa Israeli kutoka siku ile hata leo.
26 Lorsque David arriva à Ziklag, il envoya une partie du butin aux anciens de Juda, même à ses amis, en disant: « Voici un présent pour vous, tiré du butin des ennemis de l'Éternel. »
Daudi alipofika Siklagi, akatuma baadhi ya nyara kwa wazee wa Yuda, waliokuwa rafiki zake, akasema, “Tazama, hapa kuna zawadi kwa ajili yenu kutoka nyara za adui za Bwana.”
27 Il l'envoya à ceux qui étaient à Béthel, à ceux qui étaient à Ramoth du Sud, à ceux qui étaient à Jattir,
Akazituma kwa wale waliokuwa Betheli, Ramoth-Negebu na Yatiri;
28 à ceux qui étaient à Arœr, à ceux qui étaient à Siphmoth, à ceux qui étaient à Eshtemoa,
kwa wale walioko Aroeri, Sifmothi, Eshtemoa
29 à ceux qui étaient à Racal, à ceux qui étaient dans les villes des Jerahmeelites, à ceux qui étaient dans les villes des Kenites,
na Rakali; kwa wale waliokuwa katika miji ya Wayerameeli na ya Wakeni;
30 à ceux qui étaient à Horma, à ceux qui étaient à Borashan, à ceux qui étaient à Athach,
na kwa wale walioko Horma, Bori-Ashani, Athaki,
31 à ceux qui étaient à Hébron, et à tous les endroits où David lui-même et ses hommes avaient l'habitude de séjourner.
na kwa wakazi wa Hebroni; na kwa wale waliokuwa mahali pengine pote ambako Daudi na watu wake walitembelea.

< 1 Samuel 30 >