< 1 Samuel 2 >

1 Hannah pria et dit, « Mon cœur exulte en Yahvé! Ma corne est exaltée en Yahvé. Ma bouche s'élargit sur mes ennemis, car je me réjouis de ton salut.
Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 Il n'y a personne d'aussi saint que Yahvé, car il n'y a personne d'autre que toi, et il n'y a aucun rocher comme notre Dieu.
“Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
3 « Ne continuez pas à parler avec tant d'orgueil. Ne laissez pas l'arrogance sortir de votre bouche, car Yahvé est un Dieu de la connaissance. C'est par lui que les actions sont pesées.
“Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
4 « Les arcs des puissants sont brisés. Ceux qui ont trébuché sont armés de force.
“Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
5 Ceux qui étaient rassasiés se sont loués pour du pain. Ceux qui avaient faim sont satisfaits. Oui, la stérile a donné naissance à sept enfants. Celle qui a beaucoup d'enfants se languit.
Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
6 « Yahvé tue et fait vivre. Il descend au Shéol et remonte. (Sheol h7585)
“Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
7 Yahvé rend pauvre et enrichit. Il abaisse, il élève aussi.
Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
8 Il fait sortir les pauvres de la poussière. Il soulève les nécessiteux du tas de fumier. pour les faire asseoir avec les princes et hériter du trône de gloire. Car les piliers de la terre appartiennent à Yahvé. Il a mis le monde sur eux.
Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
9 Il gardera les pieds de ses saints, mais les méchants seront réduits au silence dans les ténèbres; car aucun homme ne prévaudra par la force.
Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
10 Ceux qui luttent contre Yahvé seront mis en pièces. Il tonnera contre eux dans le ciel. « Yahvé jugera les extrémités de la terre. Il donnera de la force à son roi, et exalte la corne de son oint. »
wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
11 Elkana se rendit à Rama, dans sa maison. L'enfant servit Yahvé devant le prêtre Eli.
Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
12 Or les fils d'Eli étaient des hommes méchants. Ils ne connaissaient pas Yahvé.
Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
13 La coutume des prêtres avec le peuple était que, lorsque quelqu'un offrait un sacrifice, le serviteur du prêtre venait pendant que la viande bouillait, avec une fourchette de trois dents dans la main;
Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
14 et il la plantait dans la casserole, ou la marmite, ou le chaudron, ou le pot. Le prêtre prenait pour lui tout ce que la fourchette faisait remonter. On faisait cela à tous les Israélites qui venaient là, à Silo.
Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
15 Avant de brûler la graisse, le serviteur du prêtre vint et dit à l'homme qui avait sacrifié: « Donne de la viande à rôtir pour le prêtre, car il n'acceptera pas de toi de la viande bouillie, mais crue. »
Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
16 Si l'homme lui disait: « Qu'on brûle d'abord la graisse, et qu'ensuite tu prennes autant que ton âme le désire », il répondait: « Non, mais tu me la donneras maintenant; sinon, je la prendrai de force. »
Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
17 Le péché des jeunes gens fut très grand devant l'Éternel, car ils méprisèrent l'offrande de l'Éternel.
Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
18 Samuel, lui, faisait le service devant l'Éternel; il était encore un enfant, vêtu d'un éphod de lin.
Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
19 Sa mère lui fit aussi une petite robe, qu'elle lui apporta d'année en année, quand elle montait avec son mari pour offrir le sacrifice annuel.
Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
20 Eli bénit Elkana et sa femme et dit: « Que l'Éternel vous donne une descendance de cette femme pour la demande qui a été faite à l'Éternel. » Puis ils s'en allèrent chez eux.
Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
21 Yahvé visita Anne, qui conçut et enfanta trois fils et deux filles. L'enfant Samuel grandit devant Yahvé.
Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
22 Or Éli était très vieux, et il apprit tout ce que ses fils faisaient à tout Israël, et comment ils couchaient avec les femmes qui servaient à l'entrée de la tente de la Rencontre.
Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
23 Il leur dit: « Pourquoi faites-vous de telles choses? Car j'apprends de tous ces gens que vous agissez mal.
Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
24 Non, mes fils, car ce n'est pas un bon rapport que j'entends! Vous faites désobéir le peuple de Yahvé.
Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
25 Si un homme pèche contre un autre, Dieu le jugera; mais si un homme pèche contre Yahvé, qui intercédera pour lui? ». Malgré tout, ils n'ont pas écouté la voix de leur père, car Yahvé avait l'intention de les tuer.
Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
26 L'enfant Samuel grandissait et augmentait sa popularité auprès de Yahvé et des hommes.
Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
27 Un homme de Dieu s'approcha d'Eli et lui dit: « Yahvé dit: « Ne me suis-je pas révélé à la maison de ton père lorsqu'ils étaient en Égypte, en servitude chez Pharaon?
Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
28 Ne l'ai-je pas choisi parmi toutes les tribus d'Israël pour être mon prêtre, pour monter à mon autel, pour brûler les parfums, pour porter l'éphod devant moi? N'ai-je pas donné à la maison de ton père toutes les offrandes consumées par le feu des enfants d'Israël?
Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
29 Pourquoi donnez-vous des coups de pied à mon sacrifice et à mon offrande, que j'ai ordonnés dans ma demeure, et honorez-vous vos fils au-dessus de moi, pour vous engraisser avec les meilleures de toutes les offrandes d'Israël, mon peuple?
Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
30 C'est pourquoi Yahvé, le Dieu d'Israël, dit: « J'ai dit que ta maison et la maison de ton père marcheraient devant moi pour toujours. Mais maintenant, Yahvé dit: 'Loin de moi cette idée, car j'honorerai ceux qui m'honorent, et je maudirai ceux qui me méprisent'.
“Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
31 Voici que les jours viennent où je couperai ton bras et le bras de la maison de ton père, et où il n'y aura plus de vieillard dans ta maison.
Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
32 Tu verras l'affliction de ma demeure, dans toutes les richesses que je donnerai à Israël. Il n'y aura pas à jamais de vieillard dans ta maison.
nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
33 L'homme de ta maison que je ne retrancherai pas de mon autel consumera tes yeux et affligera ton cœur. Tout l'accroissement de ta maison mourra dans la fleur de l'âge.
Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
34 Tel sera pour toi le signe qui viendra sur tes deux fils, Hophni et Phinées: en un seul jour, ils mourront tous les deux.
“‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
35 Je me susciterai un prêtre fidèle qui agira selon ce qui est dans mon cœur et dans mon esprit. Je lui bâtirai une maison sûre. Il marchera devant mon oint pour toujours.
Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
36 Tous ceux qui resteront dans ta maison viendront se prosterner devant lui pour une pièce d'argent et une miche de pain, et diront: « Mets-moi dans l'une des fonctions sacerdotales, je te prie, pour que je mange un morceau de pain. »"
Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”

< 1 Samuel 2 >