< 1 Samuel 13 >

1 Saül avait trente ans lorsqu'il devint roi, et il régna sur Israël pendant quarante-deux ans.
Sauli alikwa na umri wa miaka [thelathini] alipoanza kutawala; alipokuwa ametawala Israeli kwa miaka [arobaini],
2 Saül choisit pour lui trois mille hommes d'Israël, dont deux mille étaient avec Saül à Micmasch et sur la montagne de Béthel, et mille étaient avec Jonathan à Guibea de Benjamin. Il envoya le reste du peuple dans ses tentes.
aliwachagua wanaume elfu tatu wa Israeli. Elfu mbili walikuwa pamoja naye huko Mikmashi na katika nchi ya milima ya Betheli, wakati huo wale elfu moja walikuwa pamoja na Yonathani katika Gibea ya Benyamini. Askari waliobaki aliwarudisha nyumbani, kila mtu hemani kwake.
3 Jonathan frappa la garnison des Philistins qui était à Guéba, et les Philistins l'apprirent. Saül fit sonner la trompette dans tout le pays, en disant: « Que les Hébreux entendent! »
Yonathani akaishinda ngome ya jeshi la Wafilisti iliyokuwa Geba na Wafilisti wakasikia habari hiyo. Baadaye Sauli alipiga tarumbeta katika nchi yote, akisema, “Sikieni enyi Waebrania.”
4 Tout Israël apprit que Saül avait frappé la garnison des Philistins, et aussi qu'Israël était considéré comme une abomination par les Philistins. Le peuple se rassembla après Saül à Guilgal.
Israeli yote imesikia kwamba Sauli ameipiga ngome ya Wafilisti, na pia kwamba Israeli imekuwa uvundo kwa Wafilisti. Ndipo askari wakaitwa kwa pamoja kuungana na Sauli huko Gilgali.
5 Les Philistins se rassemblèrent pour combattre Israël: trente mille chars, six mille cavaliers, et un peuple nombreux comme le sable qui est au bord de la mer. Ils montèrent et campèrent à Micmasch, à l'orient de Beth Aven.
Wafilisti walijikusanya pamoja kupigana dhidi ya Waisraeli: magari elfu tatu, watu elfu sita wakuendesha magari, na majeshi mengi kama mchanga ufukoni mwa bahari. Wakapanda na kupiga kambi huko Mikimashi, mashariki mwa Beth aveni.
6 Lorsque les hommes d'Israël virent qu'ils étaient en difficulté (car le peuple était en détresse), alors le peuple se cacha dans des cavernes, dans des fourrés, dans des rochers, dans des tombeaux et dans des fosses.
Watu wa Israeli walipoona kuwa wapo katika matatizo -kwa maana watu walikata tamaa, wakajificha kwenye mapango, kwenye vichaka, kwenye miamba, kwenye visima na katika mashimo.
7 Une partie des Hébreux avait traversé le Jourdain pour se rendre au pays de Gad et de Galaad; quant à Saül, il était encore à Guilgal, et tout le peuple le suivait en tremblant.
Baadhi ya Waebrania walipanda kwenda Yordani katika nchi ya Gadi na Gileadi. Lakini Sauli alibaki Gilgali, na watu waliomfuata wakitetemeka.
8 Il resta sept jours, selon le temps fixé par Samuel; mais Samuel n'était pas venu à Guilgal, et le peuple se dispersait devant lui.
Alisubiri kwa siku saba, muda uliopangwa na Samweli. Lakini Samweli hakufika huko Gilgali, na watu wakatawanyika mbali na Sauli.
9 Saül dit: « Apportez-moi ici l'holocauste et les sacrifices de paix. » Il offrit l'holocauste.
Sauli akasema, “Nileteeni sadaka ya kuteketezwa na sdaka ya amani.” Kisha akatoa sadaka ya kuteketezwa.
10 Dès qu'il eut achevé d'offrir l'holocauste, voici que Samuel arriva; Saül sortit à sa rencontre pour le saluer.
Mara tu alipomaliza kutoa sadaka ya kuteketezwa Samweli akawasili. Sauli akatoka nje wakutane na kumsalimia.
11 Samuel dit: « Qu'as-tu fait? » Saül dit: « Parce que j'ai vu que le peuple s'était dispersé loin de moi, que tu n'étais pas venu dans les jours fixés, et que les Philistins s'étaient rassemblés à Michmash,
Basi Samweli akasema, “Umefanya nini?” Sauli akajibu, “Nilipoona kwamba watu wanaiacha, na kwamba umechelewa hukufika kwa muda uliopangwa, na kwamba Wafilisti wamekwisha jikusanya huko Mikmashi,
12 j'ai donc dit: « Maintenant les Philistins vont descendre sur moi jusqu'à Gilgal, et je n'ai pas imploré la faveur de Yahvé. Je me suis donc forcé et j'ai offert l'holocauste. »
nikasema, 'Sasa Wafilisti watashuka dhidi yangu huko Gilgali, na sijaomba kibali cha BWANA.' Kwa hiyo nikajilazimisha mwenyewe kutoa sadaka ya kuteketezwa.”.
13 Samuel dit à Saül: « Tu as fait une folie. Tu n'as pas observé le commandement de l'Éternel, ton Dieu, qu'il t'avait donné; car maintenant l'Éternel aurait établi ton règne sur Israël pour toujours.
Ndipo Samweli akamwambia Sauli, “Umetenda mambo ya kipumbavu. Hukuheshimu amri ya BWANA Mungu wako aliyokupatia. Kwa maana BWANA angeutengeneza utawala wako juu ya Israeli milele.
14 Mais maintenant, ton règne ne durera pas. L'Éternel s'est cherché un homme selon son cœur, et l'Éternel l'a établi prince sur son peuple, parce que vous n'avez pas gardé ce que l'Éternel vous avait commandé. »
Lakini sasa utawala wako hautaendelea. BWANA ametafuta mtu anayekubaliwa na moyo wake, kwa sababu wewe hukutii alichokuamuru.”
15 Samuel se leva et alla de Guilgal à Guibea de Benjamin. Saül compta le peuple qui était présent avec lui, soit environ six cents hommes.
Ndipo Samweli akasimama akapanda kutoka Gilgali hadi Gibea ya Benyamini. Basi Sauli akawahesabu watu waliokuwapo pamoja naye, idadi yao ilikuwa kama watu mia sita.
16 Saül, Jonathan, son fils, et le peuple qui était avec eux, restèrent à Guéba de Benjamin; mais les Philistins campaient à Micmash.
Sauli, mtoto wake Yonathani, na watu waliokuwa pamoja nao, wakabaki Geba ya Benyamimni. Lakini Wafilisti wakapiga kambi huko Mikmashi.
17 Les pillards sortirent du camp des Philistins en trois compagnies: une compagnie prit le chemin qui mène à Ophra, au pays de Shual;
Wateka nyara makundi matatu wakaja kutoka kambi ya Wafilisti. Kundi moja likapinda kuelekea Ofra, hadi nchi ya Shuali.
18 une autre compagnie prit le chemin de Beth Horon; et une autre compagnie prit le chemin de la frontière qui regarde la vallée de Zeboïm vers le désert.
Kundi jingine likageuka kuelekea Bethholoni, na kundi jingine likaelekea katika mpaka kulikabili bonde la Seboimu kuelekea jangwani.
19 Il n'y avait pas de forgeron dans tout le pays d'Israël, car les Philistins avaient dit: « De peur que les Hébreux ne se fabriquent des épées ou des lances ».
Hakuna hata mhunzi aliyeonekana katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walisema, “Waebrania wasije wakajitengenezea mapanga au mikuki.”
20 Mais tous les Israélites descendirent chez les Philistins, chacun aiguisant son soc, sa hache et sa faucille.
Lakini Waisraeli wote huwa wakiteremka kwa Wafilisti, kila mtu kunoa jembe lake, sululu yake, shoka lake na mundu wake.
21 Le prix était d'un payim par personne pour aiguiser les socs, les socs de charrue, les fourches, les haches et les aiguillons.
Gharama za kunoa ncha za majembe, sululu, mashoka na kunyoosha michokoo ilikuwa theluthi moja ya shekeli.
22 Au jour du combat, on ne trouva ni épée ni lance dans la main d'aucun des gens qui étaient avec Saül et Jonathan, mais Saül et Jonathan, son fils, les avaient.
Hivyo siku ya vita, hakukuwa na mapanga au mikuki iliyoonekana katika mikono yoyote ya askali waliokuwa na Sauli na Yonathani; Ni Sauli na mtoto wake tu ndio walikuwa nazo.
23 La garnison des Philistins sortit au col de Micmash.
Vikosi vya Wafilisti wakatokeza katika nija ya Mikmashi.

< 1 Samuel 13 >