< 1 Rois 8 >

1 Alors Salomon assembla au roi Salomon, à Jérusalem, les anciens d'Israël, avec tous les chefs de tribus, les chefs de famille des enfants d'Israël, pour faire monter l'arche de l'alliance de Yahvé de la cité de David, qui est Sion.
Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
2 Tous les hommes d'Israël se rassemblèrent auprès du roi Salomon à la fête du mois d'Ethanim, qui est le septième mois.
Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.
3 Tous les anciens d'Israël vinrent, et les prêtres prirent l'arche.
Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano,
4 Ils firent monter l'arche de Yahvé, la tente d'assignation et tous les objets sacrés qui étaient dans la tente. Les sacrificateurs et les Lévites les portèrent.
nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba,
5 Le roi Salomon et toute l'assemblée d'Israël, qui s'était rassemblée autour de lui, étaient avec lui devant l'arche, sacrifiant des brebis et des bœufs qui ne pouvaient être ni comptés ni dénombrés pour la multitude.
naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
6 Les prêtres apportèrent l'arche de l'alliance de Yahvé à sa place, dans le sanctuaire intérieur de la maison, dans le lieu très saint, sous les ailes des chérubins.
Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
7 Car les chérubins étendaient leurs ailes sur le lieu de l'arche, et les chérubins couvraient l'arche et ses poteaux par-dessus.
Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea.
8 Les barres étaient si longues qu'on en voyait les extrémités depuis le lieu saint, devant le sanctuaire intérieur, mais on ne les voyait pas à l'extérieur. Elles y sont encore aujourd'hui.
Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
9 Il n'y avait rien dans l'arche, si ce n'est les deux tables de pierre que Moïse y déposa à Horeb, lorsque l'Éternel fit alliance avec les enfants d'Israël, à leur sortie du pays d'Égypte.
Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
10 Lorsque les prêtres sortirent du lieu saint, la nuée remplit la maison de l'Éternel,
Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana.
11 et les prêtres ne purent se tenir debout pour faire le service, à cause de la nuée, car la gloire de l'Éternel remplissait la maison de l'Éternel.
Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.
12 Alors Salomon dit: « Yahvé a dit qu'il habiterait dans les ténèbres épaisses.
Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;
13 Je t'ai certainement construit une maison d'habitation, un lieu pour que tu y demeures à jamais. »
naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”
14 Le roi tourna son visage et bénit toute l'assemblée d'Israël; et toute l'assemblée d'Israël se tint debout.
Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
15 Il dit: « Béni soit Yahvé, le Dieu d'Israël, qui a parlé de sa bouche à David, ton père, et qui l'a accompli de sa main, en disant:
Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
16 « Depuis le jour où j'ai fait sortir d'Égypte mon peuple d'Israël, je n'ai choisi aucune ville parmi toutes les tribus d'Israël pour y bâtir une maison, afin que mon nom y soit inscrit, mais j'ai choisi David pour être à la tête de mon peuple d'Israël ».
‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
17 « Or, le cœur de David, mon père, était de bâtir une maison pour le nom de l'Éternel, le Dieu d'Israël.
“Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
18 Mais l'Éternel dit à David, mon père: 'Comme tu avais à cœur de bâtir une maison pour mon nom, tu as bien fait d'avoir à cœur de le faire.
Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
19 Néanmoins, ce n'est pas toi qui bâtiras la maison, mais ton fils qui sortira de ton corps, c'est lui qui bâtira la maison à mon nom.'
Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
20 L'Éternel a accompli la parole qu'il avait prononcée, car je me suis levé à la place de David, mon père, et je suis assis sur le trône d'Israël, comme l'Éternel l'avait promis, et j'ai bâti la maison au nom de l'Éternel, le Dieu d'Israël.
“Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
21 J'y ai placé l'arche, dans laquelle se trouve l'alliance de Yahvé, qu'il a conclue avec nos pères lorsqu'il les a fait sortir du pays d'Égypte. »
Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”
22 Salomon se tint devant l'autel de l'Éternel, en présence de toute l'assemblée d'Israël, et il étendit les mains vers le ciel.
Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni
23 Il dit: « Éternel, Dieu d'Israël, il n'y a point de Dieu comme toi, en haut dans les cieux et en bas sur la terre, qui garde l'alliance et la bonté envers tes serviteurs qui marchent devant toi de tout leur cœur.
na kusema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
24 Tu as gardé envers ton serviteur David, mon père, ce que tu lui avais promis. Tu l'as dit de ta bouche, et tu l'as accompli de ta main, comme il en est aujourd'hui.
Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
25 Maintenant, que l'Éternel, le Dieu d'Israël, garde pour ton serviteur David, mon père, ce que tu lui as promis, en disant: « Il ne manquera pas d'homme à mes yeux pour s'asseoir sur le trône d'Israël, si seulement tes enfants prennent garde à leur voie, pour marcher devant moi comme tu as marché devant moi ».
“Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
26 « Maintenant donc, Dieu d'Israël, que s'accomplisse ta parole, celle que tu as dite à ton serviteur David, mon père.
Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
27 Mais Dieu habitera-t-il vraiment sur la terre? Voici, le ciel et le ciel des cieux ne peuvent te contenir; combien moins encore cette maison que j'ai bâtie!
“Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
28 Mais respecte la prière de ton serviteur et sa supplique, Yahvé mon Dieu, pour écouter le cri et la prière que ton serviteur prononce aujourd'hui devant toi;
Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
29 pour que tes yeux soient ouverts nuit et jour sur cette maison, sur le lieu dont tu as dit: « Mon nom y sera », pour écouter la prière que ton serviteur prononce sur ce lieu.
Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
30 Écoute la supplication de ton serviteur et de ton peuple d'Israël, quand ils prient vers ce lieu. Oui, écoute dans les cieux, ta demeure; et quand tu auras entendu, pardonne.
Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
31 « Si un homme pèche contre son prochain, et qu'on lui fasse prêter serment pour qu'il jure, et qu'il vienne jurer devant ton autel dans cette maison,
“Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
32 alors écoute dans les cieux, et agis, et juge tes serviteurs, condamnant le méchant, pour faire retomber sa voie sur sa propre tête, et justifiant le juste, pour lui donner selon sa justice.
basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
33 « Quand ton peuple d'Israël sera battu par l'ennemi parce qu'il a péché contre toi, s'il revient à toi et confesse ton nom, s'il te prie et t'adresse des supplications dans cette maison,
“Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
34 alors écoute dans les cieux, pardonne le péché de ton peuple d'Israël et ramène-le dans le pays que tu as donné à ses pères.
basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
35 « Quand le ciel est fermé et qu'il n'y a pas de pluie parce qu'ils ont péché contre toi, s'ils prient vers ce lieu et confessent ton nom, et s'ils se détournent de leur péché quand tu les affliges,
“Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
36 alors écoute dans les cieux, et pardonne le péché de tes serviteurs et de ton peuple Israël, quand tu leur enseignes la bonne voie dans laquelle ils doivent marcher, et fais tomber la pluie sur ton pays que tu as donné en héritage à ton peuple.
basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
37 « S'il y a famine dans le pays, s'il y a peste, s'il y a fléau, mildiou, sauterelle ou chenille; si leur ennemi les assiège dans le pays de leurs villes, quelle que soit la plaie, quelle que soit la maladie,
“Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
38 quelle que soit la prière et la supplication d'un homme, ou de tout ton peuple d'Israël, qui connaîtra la plaie de son propre cœur, et qui étendra ses mains vers cette maison,
wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili:
39 alors écoute dans les cieux, ta demeure, et pardonne, et agis, et donne à chacun selon toutes ses voies, à celui dont tu connais le cœur (car toi seul connais le cœur de tous les enfants des hommes);
basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
40 afin qu'ils te craignent tous les jours qu'ils vivront dans le pays que tu as donné à nos pères.
ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
41 « De plus, en ce qui concerne l'étranger qui n'est pas de ton peuple d'Israël, lorsqu'il viendra d'un pays lointain à cause de ton nom
“Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako,
42 (car ils entendront parler de ton grand nom, de ta main puissante et de ton bras étendu), lorsqu'il viendra et priera pour cette maison,
kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili,
43 écoute dans les cieux, ta demeure, et fais tout ce pour quoi l'étranger t'appelle; afin que tous les peuples de la terre connaissent ton nom, pour te craindre, comme ton peuple Israël, et qu'ils sachent que cette maison que j'ai bâtie est appelée de ton nom.
basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
44 « Si ton peuple part en guerre contre son ennemi, par quelque moyen que tu l'envoies, et qu'il prie Yahvé vers la ville que tu as choisie et vers la maison que j'ai bâtie pour ton nom,
“Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
45 écoute dans les cieux leur prière et leur supplication, et fais droit à leur cause.
basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
46 S'ils pèchent contre toi, car il n'y a pas d'homme qui ne pèche pas, si tu t'irrites contre eux et les livres à l'ennemi, qui les emmène captifs dans le pays de l'ennemi, au loin ou dans le voisinage,
“Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu;
47 s'ils se repentent dans le pays où ils ont été emmenés captifs, s'ils reviennent et t'adressent des supplications dans le pays de ceux qui les ont emmenés captifs, en disant: « Nous avons péché et nous avons agi avec perversité;
na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’;
48 S'ils reviennent à toi de tout leur cœur et de toute leur âme dans le pays de leurs ennemis qui les ont emmenés captifs, et s'ils te prient pour leur pays que tu as donné à leurs pères, pour la ville que tu as choisie et pour la maison que j'ai bâtie pour ton nom,
kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako;
49 alors écoute leur prière et leur supplication dans le ciel, ta demeure, et fais-leur droit;
basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao.
50 pardonne à ton peuple qui a péché contre toi et à toutes les transgressions qu'il a commises contre toi, et donne-leur compassion devant ceux qui les ont emmenés en captivité, afin qu'ils aient pitié d'eux
Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma;
51 (car ils sont ton peuple et ton héritage, que tu as fait sortir d'Égypte, du milieu de la fournaise de fer);
kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.
52 afin que tes yeux soient ouverts à la supplication de ton serviteur et à la supplication de ton peuple d'Israël, pour les écouter chaque fois qu'ils crient vers toi.
“Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia.
53 Car tu les as séparés d'entre tous les peuples de la terre pour en faire ton héritage, comme tu l'as dit par Moïse, ton serviteur, lorsque tu as fait sortir nos pères d'Égypte, Seigneur Yahvé. »
Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”
54 Lorsque Salomon eut fini d'adresser toutes ces prières et supplications à Yahvé, il se leva de devant l'autel de Yahvé, à genoux, les mains étendues vers le ciel.
Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni.
55 Il se leva et bénit toute l'assemblée d'Israël d'une voix forte, en disant:
Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:
56 « Béni soit Yahvé, qui a donné du repos à son peuple d'Israël, selon tout ce qu'il avait promis. Il n'a pas manqué une seule parole de toute sa bonne promesse, qu'il a faite par Moïse, son serviteur.
“Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose.
57 Que Yahvé notre Dieu soit avec nous comme il a été avec nos pères. Qu'il ne nous quitte pas et ne nous abandonne pas,
Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa.
58 afin qu'il incline nos cœurs vers lui, pour que nous marchions dans toutes ses voies, et que nous observions ses commandements, ses statuts et ses ordonnances, qu'il a prescrits à nos pères.
Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu.
59 Que ces paroles, par lesquelles j'ai supplié Yahvé, soient jour et nuit près de Yahvé notre Dieu, afin qu'il défende la cause de son serviteur et la cause de son peuple d'Israël, comme chaque jour l'exige;
Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku,
60 afin que tous les peuples de la terre sachent que Yahvé lui-même est Dieu. Il n'y a personne d'autre.
ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine.
61 « Que votre cœur soit donc parfait avec Yahvé notre Dieu, pour marcher dans ses statuts et garder ses commandements, comme il l'est aujourd'hui. »
Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”
62 Le roi, et tout Israël avec lui, offrit des sacrifices devant Yahvé.
Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana.
63 Salomon offrit pour le sacrifice d'actions de grâces, qu'il offrit à l'Éternel, vingt-deux mille têtes de bétail et cent vingt mille moutons. Le roi et tous les enfants d'Israël firent ainsi la dédicace de la maison de Yahvé.
Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.
64 Ce même jour, le roi consacra le milieu du parvis qui était devant la maison de l'Éternel, car c'est là qu'il offrait l'holocauste, l'offrande et la graisse des sacrifices de prospérité, car l'autel d'airain qui était devant l'Éternel était trop petit pour recevoir l'holocauste, l'offrande et la graisse des sacrifices de prospérité.
Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.
65 En ce temps-là, Salomon fit la fête, et tout Israël avec lui, une grande assemblée, depuis l'entrée de Hamath jusqu'au torrent d'Égypte, devant l'Éternel, notre Dieu, pendant sept jours et sept autres jours, soit quatorze jours.
Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne.
66 Le huitième jour, il renvoya le peuple; ils bénirent le roi et s'en allèrent dans leurs tentes, joyeux et contents dans leur cœur, à cause de toute la bonté que Yahvé avait manifestée à David, son serviteur, et à Israël, son peuple.
Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.

< 1 Rois 8 >