< 1 Rois 3 >
1 Salomon fit une alliance matrimoniale avec Pharaon, roi d'Égypte. Il prit la fille de Pharaon et l'amena dans la cité de David jusqu'à ce qu'il ait fini de construire sa propre maison, la maison de Yahvé et la muraille autour de Jérusalem.
Solomoni akafanya urafiki na Mfalme Farao wa Misri na kumwoa binti yake. Akamleta huyo binti katika Mji wa Daudi mpaka alipomaliza kujenga jumba lake la kifalme na Hekalu la Bwana, pamoja na ukuta kuzunguka Yerusalemu.
2 Cependant, le peuple sacrifiait sur les hauts lieux, car il n'y avait pas encore de maison construite au nom de Yahvé.
Hata hivyo, watu bado walikuwa wakitoa dhabihu huko kwenye vilima, kwa sababu Hekalu lilikuwa bado halijajengwa kwa ajili ya Jina la Bwana.
3 Salomon aimait l'Éternel et suivait les lois de David, son père, sauf qu'il offrait des sacrifices et brûlait des parfums sur les hauts lieux.
Solomoni akaonyesha upendo wake kwa Bwana kwa kuenenda sawasawa na amri za Daudi baba yake, ila yeye alitoa dhabihu na kufukiza uvumba huko mahali pa juu.
4 Le roi alla à Gabaon pour y sacrifier, car c'était le grand haut lieu. Salomon offrit mille holocaustes sur cet autel.
Mfalme akaenda Gibeoni kutoa dhabihu, kwa maana ndipo palipokuwa mahali pa juu pa kuabudia, naye Solomoni akatoa sadaka elfu moja za kuteketezwa juu ya hayo madhabahu.
5 À Gabeon, Yahvé apparut en songe à Salomon, la nuit, et Dieu lui dit: « Demande ce que je dois te donner. »
Bwana akamtokea Solomoni huko Gibeoni wakati wa usiku katika ndoto, naye Mungu akasema, “Omba lolote utakalo nikupe.”
6 Salomon dit: « Tu as montré à ton serviteur David, mon père, une grande bonté, parce qu'il a marché devant toi dans la vérité, dans la droiture et dans la droiture de cœur avec toi. Tu as gardé pour lui cette grande bonté, en lui donnant un fils pour s'asseoir sur son trône, comme c'est le cas aujourd'hui.
Solomoni akajibu, “Umemfanyia mtumishi wako, baba yangu Daudi, fadhili nyingi, kwa kuwa alikuwa mwaminifu kwako na mwenye haki, tena mnyofu wa moyo. Nawe umemzidishia fadhili hii kuu kwani umempa mwana wa kuketi kwenye kiti chake cha ufalme, kama ilivyo leo.
7 Maintenant, Yahvé mon Dieu, tu as établi ton serviteur comme roi à la place de David, mon père. Je ne suis qu'un petit enfant. Je ne sais ni sortir ni entrer.
“Sasa, Ee Bwana Mungu wangu, umemfanya mtumishi wako mfalme badala ya baba yangu Daudi. Lakini mimi ni mtoto mdogo tu, wala sijui jinsi ya kutekeleza wajibu wangu.
8 Ton serviteur est au milieu de ton peuple que tu as choisi, un grand peuple, qui ne peut être ni dénombré ni compté pour la multitude.
Mtumishi wako yuko hapa miongoni mwa watu uliowachagua: taifa kubwa, watu wengi wasioweza kuhesabika wala kutoa idadi yao.
9 Donne donc à ton serviteur un cœur compréhensif pour juger ton peuple, afin que je puisse discerner le bien du mal; car qui est capable de juger ton grand peuple? »
Hivyo mpe mtumishi wako moyo wa ufahamu ili kutawala watu wako na kupambanua kati ya mema na mabaya. Kwa maana, ni nani awezaye kutawala watu wako hawa walio wengi hivi?”
10 Cette demande plut à l'Éternel, car Salomon avait demandé cette chose.
Bwana akapendezwa kwamba Solomoni ameliomba jambo hili.
11 Dieu lui dit: « Parce que tu as demandé cela, et que tu n'as pas demandé pour toi une longue vie, ni la richesse pour toi-même, ni la vie de tes ennemis, mais que tu as demandé pour toi l'intelligence pour discerner la justice,
Basi Mungu akamwambia, “Kwa kuwa umeomba neno hili na hukuomba maisha marefu au upate utajiri kwa nafsi yako, wala adui zako wafe, bali umeomba ufahamu katika kutoa haki,
12 voici, j'ai fait selon ta parole. Voici, je t'ai donné un cœur sage et compréhensif, de sorte qu'il n'y a eu personne comme toi avant toi, et qu'après toi, il n'y aura personne comme toi.
nitafanya lile uliloomba. Nitakupa moyo wa hekima na wa ufahamu, kiasi kwamba hajakuwepo mtu mwingine kama wewe, wala kamwe hatakuwepo baada yako.
13 Je t'ai aussi donné ce que tu n'as pas demandé, la richesse et la gloire, de sorte qu'il n'y aura pas de roi comme toi pendant toute ta vie.
Zaidi ya hayo, nitakupa yale ambayo hukuomba, yaani utajiri na heshima, ili kwamba maisha yako yote hapatakuwa na mtu kama wewe miongoni mwa wafalme.
14 Si tu marches dans mes voies, pour observer mes lois et mes commandements, comme a marché ton père David, j'allongerai tes jours. »
Nawe kama ukienenda katika njia zangu na kutii sheria na amri zangu kama baba yako Daudi alivyofanya, nitakupa maisha marefu.”
15 Salomon se réveilla; et voici, c'était un rêve. Il vint à Jérusalem, se plaça devant l'arche de l'alliance de Yahvé, offrit des holocaustes et des sacrifices de paix, et fit un festin pour tous ses serviteurs.
Ndipo Solomoni akaamka, akatambua kuwa ilikuwa ndoto. Akarudi Yerusalemu, akasimama mbele ya Sanduku la Agano la Bwana, naye akatoa dhabihu za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha akawafanyia watumishi wake wote karamu.
16 Alors deux femmes qui se prostituaient vinrent auprès du roi et se présentèrent devant lui.
Basi wanawake wawili makahaba walikuja kwa mfalme na kusimama mbele yake.
17 L'une d'elles dit: « Oh, mon seigneur, cette femme et moi habitons dans une même maison. J'ai accouché d'un enfant avec elle dans la maison.
Mmojawapo akasema, “Bwana wangu, mimi na mwanamke huyu tunaishi kwenye nyumba moja. Nilikuwa nimezaa alipokuwa pamoja nami.
18 Le troisième jour après mon accouchement, cette femme a aussi accouché. Nous étions ensemble. Il n'y avait pas d'étranger avec nous dans la maison, seulement nous deux dans la maison.
Siku ya tatu baada ya mtoto wangu kuzaliwa, mwanamke huyu pia naye akazaa mtoto. Tulikuwa peke yetu, hapakuwa na mtu mwingine yeyote katika nyumba isipokuwa sisi wawili.
19 L'enfant de cette femme mourut pendant la nuit, parce qu'elle était couchée sur lui.
“Wakati wa usiku mwana wa huyu mwanamke akafa kwa sababu alimlalia.
20 Elle s'est levée à minuit, a pris mon fils à côté de moi, pendant que ton serviteur dormait, et l'a mis dans son sein; elle a mis son enfant mort dans mon sein.
Hivyo akaondoka katikati ya usiku na kumchukua mwanangu kutoka ubavuni pangu wakati mimi mtumishi wako nilipokuwa nimelala. Akamweka kifuani mwake na kumweka mwanawe aliyekufa kifuani mwangu.
21 Lorsque je me levai le matin pour allaiter mon enfant, voici qu'il était mort; mais lorsque je l'eus regardé le matin, voici que ce n'était pas mon fils que j'avais porté. »
Asubuhi yake, nikaamka ili kumnyonyesha mwanangu, naye alikuwa amekufa! Lakini nilipomwangalia sana katika nuru ya asubuhi, niliona kuwa hakuwa yule mwana niliyekuwa nimemzaa.”
22 L'autre femme a dit: « Non! Mais celui qui vit est mon fils, et celui qui est mort est ton fils. » Le premier dit: « Non! Mais le mort est ton fils, et le vivant est mon fils. » Ils se disputèrent ainsi devant le roi.
Huyo mwanamke mwingine akasema, “Hapana! Mwana aliye hai ndiye wangu, aliyekufa ni wako.” Lakini yule wa kwanza akasisitiza, “Hapana! Mwana aliyekufa ni wako, aliye hai ni wangu.” Hivi ndivyo walivyobishana mbele ya mfalme.
23 Alors le roi dit: « L'un dit: C'est mon fils qui vit, et ton fils est le mort; et l'autre dit: Non! Mais ton fils est le mort, et mon fils est le vivant. »
Mfalme akasema, “Huyu anasema, ‘Mwanangu ndiye aliye hai, na aliyekufa ndiye mwanao,’ maadamu yule anasema, ‘Hapana! Aliyekufa ni wako, na aliye hai ni wangu.’”
24 Le roi dit: « Apportez-moi une épée. » Ils apportèrent donc une épée devant le roi.
Kisha mfalme akasema, “Nileteeni upanga.” Basi wakamletea mfalme upanga.
25 Le roi dit: « Divisez l'enfant vivant en deux, donnez-en la moitié à l'un et la moitié à l'autre. »
Ndipo mfalme akatoa amri: “Mkate mtoto aliye hai vipande viwili; mpe huyu nusu na mwingine nusu.”
26 Alors la femme à qui appartenait l'enfant vivant parla au roi, car son cœur se languissait de son fils, et elle dit: « Oh, mon seigneur, donne-lui l'enfant vivant, et ne le tue en aucun cas! ». Mais l'autre a dit: « Il ne sera ni à moi ni à toi. Divise-le. »
Mwanamke ambaye mwanawe alikuwa hai akajawa na huruma kwa ajili ya mwanawe na kumwambia mfalme, “Tafadhali, bwana wangu, mpe yeye mtoto aliye hai! Usimuue!” Lakini yule mwanamke mwingine akasema, “Mkate vipande viwili. Asiwe wangu au wake!”
27 Le roi répondit: « Donne à la première femme l'enfant vivant, et ne le tue surtout pas. Elle est sa mère. »
Kisha mfalme akatoa uamuzi wake: “Mpeni mama wa kwanza mtoto aliye hai. Msimuue; ndiye mama yake.”
28 Tout Israël apprit le jugement que le roi avait rendu, et ils craignirent le roi, car ils virent que la sagesse de Dieu était en lui pour faire justice.
Wakati Israeli yote iliposikia hukumu aliyotoa mfalme, wakamwogopa mfalme, kwa sababu waliona kuwa alikuwa na hekima kutoka kwa Mungu kwa kutoa haki.