< 1 Rois 19 >

1 Achab raconta à Jézabel tout ce qu'Élie avait fait, et comment il avait tué par l'épée tous les prophètes.
Ahabu akamwambia Yezebeli kila kitu Eliya alichokuwa amefanya na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga.
2 Alors Jézabel envoya un messager à Élie, en disant: « Que les dieux me fassent ainsi, et plus encore, si je ne fais pas de ta vie la vie de l'un d'eux, demain à cette heure-ci! ».
Hivyo Yezebeli akamtuma mjumbe kwa Eliya, kusema, “Hao miungu initendee hivyo na kuzidi, kama kufikia kesho wakati kama huu sitaifanya roho yako kama mmojawapo wa hao manabii.”
3 Dès qu'il vit cela, il se leva et courut pour sauver sa vie, et il arriva à Beersheba, qui appartient à Juda, et il y laissa son serviteur.
Eliya aliogopa, na akakimbia kuokoa maisha yake. Alipofika Beer-Sheba katika Yuda, akamwacha mtumishi wake huko,
4 Mais lui-même fit une journée de marche dans le désert, et vint s'asseoir sous un genévrier. Puis il demanda pour lui-même à mourir, et dit: « C'est assez. Maintenant, Yahvé, ôte-moi la vie, car je ne suis pas meilleur que mes pères. »
lakini yeye mwenyewe akatembea mwendo wa kutwa nzima katika jangwa. Akafika kwenye mti wa mretemu, akakaa chini yake na kuomba ili afe. Akasema, “Yatosha sasa, Bwana, ondoa roho yangu, kwani mimi si bora kuliko baba zangu.”
5 Il se coucha et dormit sous un genévrier; et voici qu'un ange le toucha et lui dit: « Lève-toi et mange! »
Kisha akajinyoosha chini ya mti, akalala usingizi. Mara malaika akamgusa na akamwambia, “Inuka na ule.”
6 Il regarda, et voici qu'il y avait à sa tête un gâteau cuit sur les charbons, et une cruche d'eau. Il mangea et but, puis il se recoucha.
Akatazama pande zote, napo hapo karibu na kichwa chake palikuwepo mkate uliookwa kwenye makaa ya moto na gudulia la maji. Akala na kunywa, kisha akajinyoosha tena.
7 L'ange de Yahvé revint une seconde fois, le toucha et lui dit: « Lève-toi et mange, car le voyage est trop long pour toi. »
Yule malaika wa Bwana akaja tena mara ya pili, akamgusa akamwambia, “Inuka na ule, kwa kuwa safari ni ndefu kwako.”
8 Il se leva, mangea et but, et alla, à la force de cette nourriture, quarante jours et quarante nuits, à Horeb, la montagne de Dieu.
Kwa hiyo akainuka, akala na kunywa. Akiwa ametiwa nguvu na kile chakula, akasafiri siku arobaini usiku na mchana mpaka akafika Horebu, mlima wa Mungu.
9 Il arriva dans une caverne, où il campa. Et voici que la parole de Yahvé lui fut adressée, et il lui dit: « Que fais-tu ici, Elie? »
Huko akaingia katika pango, akalala humo usiku ule. Nalo neno la Bwana likamjia, kusema, “Unafanya nini hapa, Eliya?”
10 Il dit: « J'ai été très jaloux de Yahvé, le Dieu des armées, car les enfants d'Israël ont abandonné ton alliance, renversé tes autels et tué tes prophètes par l'épée. Il ne reste que moi, moi seul, et ils cherchent à m'enlever la vie. »
Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
11 Il dit: « Sors et tiens-toi sur la montagne devant Yahvé. » Voici que Yahvé passait, et un vent grand et fort déchirait les montagnes et brisait les rochers devant Yahvé; mais Yahvé n'était pas dans le vent. Après le vent, il y eut un tremblement de terre; mais Yahvé n'était pas dans le tremblement de terre.
Bwana akasema, “Toka nje ukasimame juu ya mlima mbele za Bwana, kwa kuwa Bwana yu karibu kupita hapo.” Kisha upepo mwingi na wenye nguvu ukapasua milima ile na kuvunjavunja miamba mbele za Bwana, lakini Bwana hakuwamo katika ule upepo. Baada ya upepo palikuwa na tetemeko la nchi, lakini Bwana hakuwamo kwenye lile tetemeko.
12 Après le tremblement de terre, il y eut un feu; mais Yahvé n'était pas dans le feu. Après le feu, il y eut une petite voix calme.
Baada ya tetemeko la nchi ukaja moto, lakini Bwana hakuwamo katika ule moto. Baada ya moto ikaja sauti ya utulivu ya kunongʼona.
13 Lorsque Élie l'entendit, il enveloppa son visage dans son manteau, sortit et se tint à l'entrée de la caverne. Et voici qu'une voix s'approcha de lui et dit: « Que fais-tu ici, Élie? »
Eliya alipoisikia, akafunika uso kwa vazi lake, akatoka na kusimama kwenye mdomo wa pango. Kisha ile sauti ikamwambia, “Eliya, unafanya nini hapa?”
14 Il dit: « J'ai été très jaloux de Yahvé, le Dieu des armées, car les enfants d'Israël ont abandonné ton alliance, jeté tes autels et tué tes prophètes par l'épée. Il ne reste que moi, moi seul, et ils cherchent à m'enlever la vie. »
Akajibu, “Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote. Waisraeli wamelikataa Agano lako, wamevunja madhabahu zako na kuwaua manabii wako kwa upanga. Ni mimi, mimi peke yangu, niliyebaki, nao sasa wananitafuta ili waniangamize.”
15 Yahvé lui dit: « Va, retourne sur ton chemin dans le désert de Damas. A ton arrivée, oint Hazaël comme roi de Syrie.
Bwana akamwambia, “Rudi kwa njia uliyoijia, uende kwenye Jangwa la Dameski. Wakati utakapofika huko, mtie Hazaeli mafuta awe mfalme wa Aramu
16 Oint Jéhu, fils de Nimshi, comme roi d'Israël, et oint Élisée, fils de Shaphat, d'Abel Meholah, comme prophète à ta place.
Pia mtie mafuta Yehu mwana wa Nimshi awe mfalme wa Israeli, na umtie Elisha mwana wa Shafati kutoka Abel-Mehola mafuta awe nabii badala yako.
17 Celui qui échappera à l'épée de Hazaël, Jehu le tuera; et celui qui échappera à l'épée de Jehu, Élisée le tuera.
Yehu atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Hazaeli, naye Elisha atamuua yeyote atakayeutoroka upanga wa Yehu.
18 Mais j'en ai réservé sept mille en Israël, tous ceux dont les genoux n'ont pas fléchi devant Baal et toutes les bouches qui ne l'ont pas baisé. »
Hata sasa nimeweka akiba watu elfu saba katika Israeli, wote ambao hawajampigia Baali magoti, na wote ambao midomo yao haijambusu.”
19 Et il partit de là et trouva Élisée, fils de Shaphat, qui labourait avec douze jougs de bœufs devant lui, et lui avec le douzième. Élie s'approcha de lui et le revêtit de son manteau.
Hivyo Eliya akaondoka kutoka huko na kumkuta Elisha mwana wa Shafati. Alikuwa akilima kwa jozi kumi na mbili za maksai, na yeye mwenyewe aliongoza ile jozi ya kumi na mbili. Eliya akapita karibu naye, akamrushia vazi lake.
20 Élisée laissa les bœufs, courut après Élie et dit: « Laisse-moi, s'il te plaît, embrasser mon père et ma mère, et ensuite je te suivrai. » Il lui dit: « Va-t'en, car que t'ai-je fait? »
Kisha Elisha akawaacha maksai wake, akamkimbilia Eliya, akamwambia, “Niruhusu nikawabusu baba yangu na mama yangu, halafu nitafuatana nawe.” Eliya akajibu, “Rudi zako, kwani nimekutendea nini?”
21 Il s'en retourna après l'avoir suivi, prit le joug des bœufs, les tua, fit bouillir leur viande avec l'équipement des bœufs, et la donna au peuple; et ils mangèrent. Puis il se leva, alla après Élie, et le servit.
Basi Elisha akamwacha Eliya, naye akarudi. Akachukua ile jozi yake ya maksai na kuwachinja. Akaipika ile nyama kwa kutumia miti ya nira kama kuni na kuwapa watu, nao wakala. Kisha akaondoka, akamfuata Eliya, akamtumikia.

< 1 Rois 19 >