< 1 Chroniques 23 >

1 David était vieux et rassasié de jours, et il établit Salomon, son fils, roi d'Israël.
Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
2 Il rassembla tous les chefs d'Israël, avec les sacrificateurs et les Lévites.
Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
3 Les Lévites furent comptés depuis l'âge de trente ans et au-dessus, et leur nombre, par tête, fut de trente-huit mille.
Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
4 David dit: « Parmi eux, vingt-quatre mille étaient chargés de surveiller les travaux de la maison de Yahvé, six mille étaient officiers et juges,
Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
5 quatre mille étaient portiers, et quatre mille louaient Yahvé avec les instruments que j'avais fabriqués pour le louer. »
na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
6 David les répartit en divisions selon les fils de Lévi: Guershon, Kehath et Merari.
Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
7 Des Gershonites: Ladan et Shimei.
Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
8 Fils de Ladan: Jehiel, le chef, Zetham et Joël, trois.
Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
9 Fils de Schimeï: Schelomoth, Hatsiel et Haran, trois. Ce sont les chefs de famille de Ladan.
Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
10 Fils de Schimeï: Jahath, Zina, Jeush et Beriah. Ces quatre-là étaient les fils de Schimeï.
Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
11 Jahath était le chef, et Zina le second; mais Jeush et Beriah n'avaient pas beaucoup de fils; c'est pourquoi ils formaient une maison de pères en un seul compte.
Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
12 Fils de Kehath: Amram, Izhar, Hebron et Uzziel, quatre.
Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
13 Fils d'Amram: Aaron et Moïse. Aaron fut séparé pour sanctifier les choses très saintes, lui et ses fils à jamais, pour offrir des parfums devant l'Éternel, pour le servir et pour bénir en son nom à jamais.
Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
14 Quant à Moïse, homme de Dieu, ses fils furent désignés dans la tribu de Lévi.
Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
15 Fils de Moïse: Gershom et Eliezer.
Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
16 Fils de Guershom: Shebuel, le chef.
Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
17 Fils d'Éliézer: Rehabia, le chef. Éliézer n'eut pas d'autres fils, mais les fils de Rehabia furent très nombreux.
Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
18 Fils de Jitsehar: Shelomith, le chef.
Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
19 Fils de Hébron: Jeriah, le chef, Amaria, le second, Jahaziel, le troisième, et Jekameam, le quatrième.
Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
20 Fils d'Uzziel: Michée, le chef, et Ischia, le second.
Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
21 Fils de Merari: Mahli et Mushi. Les fils de Mahli: Éléazar et Kish.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
22 Éléazar mourut et n'eut pas de fils, mais seulement des filles; leurs parents, les fils de Kis, les prirent pour femmes.
Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
23 Fils de Muschi: Mahli, Eder et Jérémoth, au nombre de trois.
Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
24 Ce sont là les fils de Lévi, selon leurs maisons de pères, les chefs de maisons de pères de ceux qui furent comptés individuellement, au nombre des noms selon les sondages, qui faisaient le service de la maison de l'Éternel, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus.
Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
25 Car David avait dit: « L'Éternel, le Dieu d'Israël, a donné du repos à son peuple, et il habite à Jérusalem pour toujours.
Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
26 Aussi les Lévites n'auront plus besoin de porter le tabernacle et tous ses ustensiles pour son service. »
Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
27 En effet, selon les dernières paroles de David, les fils de Lévi ont été comptés, à partir de vingt ans et plus.
Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
28 Car ils étaient chargés de servir les fils d'Aaron pour le service de la maison de Yahvé, dans les parvis, dans les chambres, pour la purification de toutes les choses saintes, pour le service de la maison de Dieu,
Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
29 pour les pains de proposition et pour la farine fine destinée à l'offrande, qu'il s'agisse de galettes sans levain, de galettes cuites au four ou de galettes trempées, et pour toutes les mesures de quantité et de taille;
Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
30 Ils se tiendront debout tous les matins pour remercier et louer Yahvé, ainsi que le soir;
Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
31 ils offriront à Yahvé tous les holocaustes aux sabbats, aux nouvelles lunes et aux fêtes, en nombre suffisant, selon les règles qui leur sont prescrites, en permanence devant Yahvé;
na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
32 ils s'acquitteront des fonctions de la tente d'assignation, des fonctions du lieu saint et des fonctions des fils d'Aaron, leurs frères, pour le service de la maison de Yahvé.
Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.

< 1 Chroniques 23 >