< Psalmien 137 >
1 Baabelin virtain vierillä-siellä me istuimme ja itkimme, kun Siionia muistelimme.
Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
2 Pajuihin, joita siellä oli, me ripustimme kanteleemme.
Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
3 Sillä vangitsijamme vaativat meiltä siellä lauluja ja orjuuttajamme iloa: "Veisatkaa meille Siionin virsiä".
Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
4 Kuinka me voisimme veisata Herran virsiä vieraalla maalla?
Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
5 Jos minä unhotan sinut, Jerusalem, niin unhota sinä minun oikea käteni.
Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
6 Tarttukoon kieleni suuni lakeen, ellen minä sinua muista, ellen pidä Jerusalemia ylimpänä ilonani.
Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
7 Muista, Herra, Jerusalemin tuhopäivä, kosta se Edomin lapsille, jotka sanoivat: "Hajottakaa se, hajottakaa perustuksia myöten!"
Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
8 Tytär Baabel, sinä häviön oma, autuas se, joka sinulle kostaa kaiken, minkä olet meille tehnyt!
Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
9 Autuas se, joka ottaa sinun pienet lapsesi ja murskaa ne kallioon!
Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.