< Sananlaskujen 25 >
1 Nämäkin ovat Salomon sananlaskuja, Hiskian, Juudan kuninkaan, miesten kokoamia.
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 Jumalan kunnia on salata asia, ja kuningasten kunnia on tutkia asia.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Taivaan korkeus ja maan syvyys ja kuningasten sydän on tutkimaton.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 Kun hopeasta poistetaan kuona, kuontuu kultasepältä astia.
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 Kun jumalaton poistetaan kuninkaan luota, vahvistuu hänen valtaistuimensa vanhurskaudessa.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 Älä tavoittele kunniaa kuninkaan edessä äläkä asetu isoisten sijalle.
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 Sillä parempi on, jos sinulle sanotaan: "Käy tänne ylös", kuin että sinut alennetaan ylhäisen edessä, jonka silmäsi olivat nähneet.
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 Älä ole kärkäs käräjöimään; muutoin sinulla ei lopulta ole, mitä tehdä, kun vastapuolesi on saattanut sinut häpeään.
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 Riitele oma riitasi vastapuolesi kanssa, mutta toisen salaisuutta älä ilmaise.
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 Muutoin sinua häpäisee, kuka sen kuuleekin, eikä huono huuto sinusta lakkaa.
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 Kultaomenia hopeamaljoissa ovat sanat, sanotut aikanansa.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 Kultainen korvarengas ja hienokultainen kaulakoru ovat viisas neuvoja ynnä kuuleva korva.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 Kuin lumen viileys elonaikana on luotettava lähetti lähettäjälleen: herransa sielun hän virvoittaa.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Kuin pilvet ja tuuli, jotka eivät sadetta tuo, on mies, joka kerskuu lahjoilla, joita ei anna.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 Kärsivällisyydellä taivutetaan ruhtinas, ja leppeä kieli murskaa luut.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 Jos hunajata löydät, syö kohtuudella, ettet kyllästyisi siihen ja sitä oksentaisi.
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 Astu jalallasi harvoin lähimmäisesi kotiin, ettei hän sinuun kyllästyisi ja alkaisi sinua vihata.
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Nuija ja miekka ja terävä nuoli on mies, joka väärin todistaa lähimmäistänsä vastaan.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Kuin mureneva hammas ja horjuva jalka on uskottoman turva ahdingon päivänä.
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 Kuin se, joka riisuu vaatteet pakkaspäivänä, kuin etikka lipeän sekaan, on se, joka laulaa lauluja murheelliselle sydämelle.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Jos vihamiehelläsi on nälkä, anna hänelle leipää syödä, ja jos hänellä on jano, anna hänelle vettä juoda.
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 Sillä niin sinä kokoat tulisia hiiliä hänen päänsä päälle, ja Herra sen sinulle palkitsee.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Pohjatuuli saa aikaan sateen ja salainen kielittely vihaiset kasvot.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
24 Parempi on asua katon kulmalla kuin toraisan vaimon huonetoverina.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 Kuin nääntyväiselle raikas vesi on hyvä sanoma kaukaisesta maasta.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Kuin sekoitettu lähde ja turmeltu kaivo on vanhurskas, joka horjuu jumalattoman edessä.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 Liika hunajan syönti ei ole hyväksi, ja raskaitten asiain tutkiminen on raskasta.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 Kuin kaupunki, varustukset hajalla, muuria vailla, on mies, joka ei mieltänsä hillitse.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.