< Sananlaskujen 17 >

1 Parempi kuiva kannikka rauhassa kuin talon täysi uhripaistia riidassa.
Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
2 Taitava palvelija hallitsee kunnotonta poikaa ja pääsee perinnönjaolle veljesten rinnalla.
Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
3 Hopealle sulatin, kullalle uuni, mutta sydämet koettelee Herra.
Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
4 Paha kuuntelee häijyjä huulia, petollisuus kuulee pahoja kieliä.
Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
5 Joka köyhää pilkkaa, se herjaa hänen luojaansa; joka toisen onnettomuudesta iloitsee, ei jää rankaisematta.
Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
6 Vanhusten kruunu ovat lastenlapset, ja isät ovat lasten kunnia.
Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
7 Ei sovi houkalle ylevä puhe, saati sitten ruhtinaalle valhe.
Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
8 Lahjus on käyttäjänsä silmissä kallis kivi: mihin vain hän kääntyy, hän menestyy.
Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
9 Joka rikkeen peittää, se rakkautta harrastaa; mutta joka asioita kaivelee, se erottaa ystävykset.
Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
10 Nuhde pystyy paremmin ymmärtäväiseen kuin sata lyöntiä tyhmään.
Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
11 Pelkkää onnettomuutta hankkii kapinoitsija, mutta häntä vastaan lähetetään armoton sanansaattaja.
Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
12 Kohdatkoon miestä karhu, jolta on riistetty poikaset, mutta älköön tyhmä hulluudessansa.
Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Joka hyvän pahalla palkitsee, sen kodista ei onnettomuus väisty.
Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
14 Alottaa tora on päästää vedet valloilleen; herkeä, ennenkuin riita syttyy.
Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
15 Syyllisen syyttömäksi ja syyttömän syylliseksi tekijä ovat kumpikin Herralle kauhistus.
Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
16 Mitä hyötyä on rahasta tyhmän käsissä? Viisauden hankkimiseen ei ole ymmärrystä.
Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
17 Ystävä rakastaa ainiaan ja veli syntyy varaksi hädässä.
Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
18 Mieltä vailla on mies, joka kättä lyöpi, joka menee toista takaamaan.
Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
19 Joka toraa rakastaa, se rikkomusta rakastaa; joka ovensa korottaa, se hankkii kukistumistaan.
Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
20 Väärämielinen ei onnea löydä, ja kavalakielinen suistuu onnettomuuteen.
Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
21 Tyhmä on murheeksi siittäjällensä, ja houkan isä on iloa vailla.
Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
22 Terveydeksi on iloinen sydän, mutta murtunut mieli kuivuttaa luut.
Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 Jumalaton ottaa lahjuksen vastaan toisen povelta vääristääksensä oikeuden tiet.
Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
24 Ymmärtäväisellä on viisaus kasvojensa edessä, mutta tyhmän silmät kiertävät maailman rantaa.
Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
25 Tyhmä poika on isällensä suruksi ja synnyttäjällensä mielihaikeaksi.
Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
26 Paha jo sekin, jos syytöntä sakotetaan; kovin kohtuutonta, jos jaloja lyödään.
Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
27 Joka hillitsee sanansa, on taitava, ja mielensä malttava on ymmärtäväinen mies.
Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
28 Hullukin käy viisaasta, jos vaiti on; joka huulensa sulkee, on ymmärtäväinen.
Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.

< Sananlaskujen 17 >