< Sananlaskujen 14 >
1 Vaimojen viisaus talon rakentaa, mutta hulluus sen omin käsin purkaa.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Joka vaeltaa oikein, se pelkää Herraa, mutta jonka tiet ovat väärät, se hänet katsoo ylen.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 Hullun suussa on ylpeydelle vitsa, mutta viisaita vartioivat heidän huulensa.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Missä raavaita puuttuu, on seimi tyhjä, mutta runsas sato saadaan härkien voimasta.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 Uskollinen todistaja ei valhettele, mutta väärä todistaja puhuu valheita.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 Pilkkaaja etsii viisautta turhaan, mutta ymmärtäväisen on tietoa helppo saada.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Menet pois tyhmän miehen luota: et tullut tuntemaan tiedon huulia.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 Mielevän viisaus on, että hän vaelluksestaan vaarin pitää; tyhmien hulluus on petos.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Hulluja pilkkaa vikauhri, mutta oikeamielisten kesken on mielisuosio.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 Sydän tuntee oman surunsa, eikä sen iloon saa vieras sekaantua.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 Jumalattomain huone hävitetään, mutta oikeamielisten maja kukoistaa.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 Miehen mielestä on oikea monikin tie, joka lopulta on kuoleman tie.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Nauraessakin voi sydän kärsiä, ja ilon lopuksi tulee murhe.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 Omista teistään saa kyllänsä se, jolla on luopunut sydän, mutta itsestään löytää tyydytyksen hyvä mies.
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 Yksinkertainen uskoo joka sanan, mutta mielevä ottaa askeleistansa vaarin.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 Viisas pelkää ja karttaa pahaa, mutta tyhmä on huoleton ja suruton.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 Pikavihainen tekee hullun töitä, ja juonittelija joutuu vihatuksi.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 Yksinkertaiset saavat perinnökseen hulluuden, mutta mielevät tiedon kruunuksensa.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 Pahojen täytyy kumartua hyvien edessä ja jumalattomien seisoa vanhurskaan porteilla.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 Köyhää vihaa hänen ystävänsäkin, mutta rikasta rakastavat monet.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 Syntiä tekee, joka lähimmäistään halveksii, mutta autuas se, joka kurjia armahtaa!
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 Eivätkö eksy ne, jotka hankitsevat pahaa? Mutta armo ja totuus niille, jotka hankitsevat hyvää!
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 Kaikesta vaivannäöstä tulee hyötyä, mutta tyhjästä puheesta vain vahinkoa.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 Viisasten kruunu on heidän rikkautensa, mutta tyhmäin hulluus hulluudeksi jää.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 Uskollinen todistaja on hengen pelastaja, mutta joka valheita puhuu, on petosta täynnä.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 Herran pelossa on vahva varmuus ja turva vielä lapsillekin.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 Herran pelko on elämän lähde kuoleman paulain välttämiseksi.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 Kansan paljous on kuninkaan kunnia, väen vähyys ruhtinaan turmio.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 Pitkämielisellä on paljon taitoa, mutta pikavihaisen osa on hulluus.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 Sävyisä sydän on ruumiin elämä, mutta luulevaisuus on mätä luissa.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 Joka vaivaista sortaa, se herjaa hänen Luojaansa, mutta se häntä kunnioittaa, joka köyhää armahtaa.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 Jumalaton sortuu omaan pahuuteensa, mutta vanhurskas on turvattu kuollessaan.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 Ymmärtäväisen sydämeen ottaa majansa viisaus, ja tyhmien keskellä se itsensä tiettäväksi tekee.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 Vanhurskaus kansan korottaa, mutta synti on kansakuntien häpeä.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 Taitava palvelija saa kuninkaan suosion, mutta kunnoton hänen vihansa.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.