< Sananlaskujen 13 >
1 Viisas poika kuulee isän kuritusta, mutta pilkkaaja ei ota nuhdetta kuullaksensa.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 Suunsa hedelmästä saa nauttia hyvää, mutta uskottomilla on halu väkivaltaan.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 Joka suistaa suunsa, se säilyttää henkensä, mutta avosuinen joutuu turmioon.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 Laiskan sielu haluaa, saamatta mitään, mutta ahkerain sielu tulee ravituksi.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 Vanhurskas vihaa valhepuhetta, mutta jumalattoman meno on iljettävä ja häpeällinen.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 Vanhurskaus varjelee nuhteettomasti vaeltavan, mutta jumalattomuus syöksee syntisen kumoon.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 Toinen on olevinaan rikas, omistamatta mitään, toinen olevinaan köyhä, vaikka on tavaraa paljon.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 Rikkautensa saa mies antaa henkensä lunnaiksi, mutta köyhän ei tarvitse uhkauksia kuunnella.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 Vanhurskasten valo loistaa iloisesti, mutta jumalattomien lamppu sammuu.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 Ylpeys tuottaa pelkkää toraa, mutta jotka ottavat neuvon varteen, niillä on viisaus.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 Tyhjällä saatu tavara vähenee, mutta joka vähin erin kokoaa, se saa karttumaan.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 Pitkä odotus tekee sydämen sairaaksi, mutta täyttynyt halu on elämän puu.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Joka sanaa halveksii, joutuu sanan pantiksi; mutta joka käskyä pelkää, saa palkan.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 Viisaan opetus on elämän lähde kuoleman paulain välttämiseksi.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 Hyvä ymmärrys tuottaa suosiota, mutta uskottomien tie on koleikkoa.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Jokainen mielevä toimii taitavasti, mutta tyhmä levittää hulluutta.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 Jumalaton sanansaattaja suistuu turmioon, mutta uskollinen lähetti on kuin lääke.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 Köyhyys ja häpeä kuritusta vierovalle, kunnia nuhdetta noudattavalle!
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 Tyydytetty halu on sielulle suloinen, pahan karttaminen tyhmille kauhistus.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 Vaella viisasten kanssa, niin viisastut; tyhmäin seuratoverin käy pahoin.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Syntisiä vainoaa onnettomuus, mutta vanhurskaat saavat onnen palkakseen.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 Hyvä jättää perinnön lastensa lapsillekin, mutta syntisen tavara talletetaan vanhurskaalle.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 Köyhien uudiskyntö antaa runsaan ruuan; mutta moni tuhoutuu, joka ei oikeudessa pysy.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 Joka vitsaa säästää, se vihaa lastaan; mutta joka häntä rakastaa, se häntä ajoissa kurittaa.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 Vanhurskas saa syödä kylläksensä, mutta jumalattomain vatsa jää vajaaksi.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.