< Sananlaskujen 10 >
1 Salomon sananlaskut. Viisas poika on isällensä iloksi, mutta tyhmä poika on äidillensä murheeksi.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Vääryyden aarteet eivät auta, mutta vanhurskaus vapahtaa kuolemasta.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 Herra ei salli vanhurskaan nälkää nähdä, mutta jumalattomien himon hän luotansa työntää.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 Köyhtyy, joka laiskasti kättä käyttää, mutta ahkerain käsi rikastuttaa.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 Taitava poika kokoaa kesällä, kunnoton poika elonaikana nukkuu.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Siunaus on vanhurskaan pään päällä, mutta väkivaltaa kätkee jumalattomien suu.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 Vanhurskaan muistoa siunataan, mutta jumalattomien nimi lahoaa.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 Viisassydäminen ottaa käskyt varteen, mutta hulluhuulinen kukistuu.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 Joka nuhteettomasti vaeltaa, vaeltaa turvassa, jonka tiet ovat väärät, se joutuu ilmi.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 Joka silmää iskee, saa aikaan tuskaa, ja hulluhuulinen kukistuu.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 Vanhurskaan suu on elämän lähde, mutta jumalattomien suu kätkee väkivaltaa.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 Viha virittää riitoja, mutta rakkaus peittää rikkomukset kaikki.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 Ymmärtäväisen huulilta löytyy viisaus, mutta joka on mieltä vailla, sille vitsa selkään!
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Viisaat kätkevät, minkä tietävät, mutta hullun suu on läheinen turmio.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 Rikkaan tavara on hänen vahva kaupunkinsa, mutta vaivaisten köyhyys on heidän turmionsa.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 Vanhurskaan hankkima on elämäksi, jumalattoman saalis koituu synniksi.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 Kuritusta noudattava on elämän tiellä, mutta nuhteet hylkäävä eksyy.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 Joka salavihaa pitää, sen huulilla on valhe, ja joka parjausta levittää, on tyhmä.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 Missä on paljon sanoja, siinä ei syntiä puutu; mutta joka huulensa hillitsee, se on taitava.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 Vanhurskaan kieli on valituin hopea, jumalattomien äly on tyhjän veroinen.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 Vanhurskaan huulet kaitsevat monia, mutta hullut kuolevat mielettömyyteensä.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 Herran siunaus rikkaaksi tekee, ei oma vaiva siihen mitään lisää.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 Tyhmälle on iloksi ilkityön teko, mutta ymmärtäväiselle miehelle viisaus.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 Mitä jumalaton pelkää, se häntä kohtaa; mutta mitä vanhurskaat halajavat, se annetaan.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 Tuulispään käytyä ei jumalatonta enää ole, mutta vanhurskaan perustus pysyy iäti.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 Mitä hapan hampaille ja savu silmille, sitä laiska lähettäjillensä.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 Herran pelko elinpäiviä jatkaa, mutta jumalattomien vuodet lyhenevät.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 Vanhurskasten odotus koituu iloksi, mutta jumalattomien toivo hukkuu.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 Herran johdatus on nuhteettoman turva, mutta väärintekijäin turmio.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 Vanhurskas ei ikinä horju, mutta jumalattomat eivät saa asua maassa.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 Vanhurskaan suu kasvaa viisauden hedelmän, mutta kavala kieli hävitetään.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 Vanhurskaan huulet tietävät, mikä otollista on, mutta jumalattomien suu on sulaa kavaluutta.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.