< Jobin 37 >
1 "Niin, siitä vapisee sydämeni ja hypähtää paikoiltansa.
Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
2 Kuulkaa, kuulkaa hänen äänensä pauhinaa ja kohinaa, joka käy hänen suustansa.
Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
3 Hän laskee sen kaikumaan kaiken taivaan alla, lähettää leimauksensa maan ääriin asti.
Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
4 Sen kintereillä ärjyy ääni, hän korottaa väkevän äänensä jylinän, eikä hän säästä salamoitaan, äänensä raikuessa.
Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
5 Ihmeellisesti Jumala korottaa äänensä jylinän, hän tekee suuria tekoja, joita emme käsittää taida.
Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
6 Sillä hän sanoo lumelle: 'Putoa maahan', samoin sadekuurolle, rankkasateittensa ryöpylle.
Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
7 Niin hän kytkee jokaiselta kädet, että kaikki ihmiset hänen tekonsa tietäisivät.
Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
8 Pedot vetäytyvät piiloon ja pysyvät luolissansa.
Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
9 Tähtitarhasta tulee tuulispää, pohjan ilmalta pakkanen.
Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
10 Jumalan henkäyksestä syntyy jää, ja aavat vedet ahdistuvat.
Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
11 Hän myös kuormittaa pilvet kosteudella ja hajottaa välähtelevät ukkosvaarunsa.
Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
12 Ne vyöryvät sinne tänne hänen ohjauksestaan, tehdäkseen maanpiirin päällä kaiken, mitä hän niille määrää.
Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
13 Hän antaa niiden osua milloin maalle vitsaukseksi, milloin siunaukseksi.
Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
14 Ota tämä korviisi, Job; pysähdy ja tarkkaa Jumalan ihmetöitä.
Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
15 Tiedätkö, kuinka Jumala niillä tekonsa teettää ja kuinka hän antaa pilviensä leimausten loistaa?
Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
16 Käsitätkö pilvien punnituksen, hänen ihmeensä, joka on kaikkitietävä?
Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
17 Sinä, jonka vaatteet kuumenevat, kun maa on raukeana etelän helletuulesta,
Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
18 kaarrutatko sinä hänen kanssansa taivaan, joka on vahva kuin valettu kuvastin?
Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
19 Neuvo, mitä meidän on hänelle sanottava; pimeydessämme emme voi tuoda esiin mitään.
Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
20 Olisiko hänelle ilmoitettava, että tahtoisin puhua? Kukapa vaatisi omaa tuhoansa!
Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
21 Ja nyt: ei voida katsella valoa, joka kirkkaana loistaa, kun tuuli on puhaltanut puhdistaen taivaan.
Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
22 Pohjoisesta tulee kultainen hohde; Jumalan yllä on peljättävä valtasuuruus.
Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
23 Kaikkivaltiasta emme saata käsittää, häntä, joka on suuri voimassa, joka ei oikeutta ja täydellistä vanhurskautta polje.
Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
24 Sentähden peljätkööt häntä ihmiset; hän ei katso keneenkään, joka on omasta mielestään viisas."
Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”