< 2 Samuelin 4 >

1 Kun Saulin poika kuuli Abnerin kuolleen Hebronissa, herposivat hänen kätensä, ja koko Israel peljästyi.
Ish-Boshethi mwana wa Sauli aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, akakosa ujasiri, nayo Israeli yote wakatiwa hofu kuu.
2 Ja Saulin pojalla oli partiojoukkojen päämiehinä kaksi miestä, toisen nimi oli Baana ja toisen Reekab, beerotilaisen Rimmonin poikia, benjaminilaisia; sillä Beerotkin luetaan kuuluvaksi Benjaminiin.
Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa vikundi vya uvamizi. Mmoja aliitwa Baana na mwingine Rekabu, waliokuwa wana wa Rimoni, Mbeerothi, kutoka kabila la Benyamini. Beerothi alihesabiwa kuwa sehemu ya Benyamini,
3 Mutta beerotilaiset olivat paenneet Gittaimiin ja asuivat siellä muukalaisina, niinkuin asuvat vielä tänäkin päivänä.
kwa sababu watu wa Beerothi walikimbilia huko Gitaimu na wameishi huko kama wageni mpaka siku hii ya leo.
4 Joonatanilla, Saulin pojalla, oli poika, joka oli rampa jaloistaan. Hän oli viiden vuoden vanha, kun sanoma Saulista ja Joonatanista tuli Jisreelistä; ja hänen hoitajansa otti hänet ja pakeni. Mutta kun tämä hätääntyneenä pakeni, putosi poika ja tuli ontuvaksi; ja hänen nimensä oli Mefiboset.
(Yonathani mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa mlemavu miguu yote miwili. Alikuwa na miaka mitano wakati habari kuhusu Sauli na Yonathani zilipofika kutoka Yezreeli. Yaya wake akambeba ili kukimbia, lakini yaya alipokuwa anaharakisha kuondoka, mtoto alianguka akawa kiwete. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.)
5 Beerotilaisen Rimmonin pojat Reekab ja Baana lähtivät matkaan ja tulivat päivän ollessa palavimmillaan Iisbosetin taloon, kun hän oli puolipäivälevollansa.
Basi Rekabu na Baana, wana wa Rimoni Mbeerothi wakaenda nyumbani kwa Ish-Boshethi, nao walifika huko wakati alipokuwa kwenye mapumziko yake ya mchana.
6 Ja katso, he tulivat sisälle taloon muka ottamaan nisuja, mutta pistivät häntä vatsaan. Ja Reekab ja hänen veljensä Baana pääsivät pakoon.
Wakaingia kwenye chumba cha ndani kana kwamba wanachukua ngano, wakamchoma Ish-Boshethi mkuki wa tumboni. Ndipo Rekabu na Baana nduguye wakatoroka.
7 He tulivat niinmuodoin taloon, kun hän lepäsi vuoteellansa makuuhuoneessaan, pistivät hänet kuoliaaksi, löivät häneltä pään poikki ja ottivat sen mukaansa. He kulkivat sitten Aromaan tietä koko yön,
Walikuwa wameingia ndani ya nyumba wakati alipokuwa amelala kitandani chumbani kwake. Baada ya kumchoma mkuki na kumuua, walikata kichwa chake. Wakiwa wamekichukua, walitembea usiku kucha kwa njia ya Araba.
8 toivat Iisbosetin pään Daavidille Hebroniin ja sanoivat kuninkaalle: "Katso, tässä on Iisbosetin, Saulin pojan, sinun vihamiehesi, pää, hänen, joka väijyi sinun henkeäsi. Herra on tänä päivänä kostanut Saulille ja hänen jälkeläisillensä herrani, kuninkaan, puolesta."
Wakamletea Daudi kichwa cha Ish-Boshethi huko Hebroni, wakamwambia mfalme, “Hiki hapa kichwa cha Ish-Boshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyejaribu kuondoa uhai wako. Siku hii ya leo Bwana amemlipia kisasi mfalme bwana wangu dhidi ya Sauli na mzao wake.”
9 Niin Daavid vastasi Reekabille ja hänen veljellensä Baanalle, beerotilaisen Rimmonin pojille, ja sanoi heille: "Niin totta kuin Herra elää, joka on vapahtanut minut kaikesta hädästä:
Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni, Mbeerothi, akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka taabu zote,
10 sen, joka ilmoitti minulle ja sanoi: 'Katso, Saul on kuollut', luullen tuovansa ilosanoman, minä otatin kiinni ja surmautin Siklagissa antaakseni hänelle sanansaattajan palkan;
yule mtu aliponiambia, ‘Sauli amekufa,’ akadhani ananiletea habari njema, nilimkamata, nikamuua huko Siklagi. Hiyo ndiyo zawadi niliyompa kwa ajili ya taarifa yake!
11 eikö minun paljoa enemmän nyt, kun jumalattomat miehet ovat murhanneet syyttömän miehen hänen omassa kodissaan, hänen vuoteeseensa, ole vaadittava hänen verensä teidän kädestänne ja hävitettävä teidät maan päältä?"
Je, ni mara ngapi zaidi wakati watu waovu wamemuua mtu asiye na hatia akiwa ndani ya nyumba yake mwenyewe na kwenye kitanda chake mwenyewe? Je, sasa nisidai damu yake mikononi mwenu na kuwaondoa duniani?”
12 Ja Daavid käski nuorten miesten surmata heidät. Niin he hakkasivat poikki heidän kätensä ja jalkansa ja hirttivät heidät Hebronin lammikon rannalle. Mutta Iisbosetin pään he ottivat ja hautasivat sen Abnerin hautaan Hebroniin.
Kwa hiyo Daudi akawaamuru watu wake, wakawaua. Wakakata mikono yao na miguu, na kutundika viwiliwili vyao kando ya dimbwi huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ish-Boshethi na kukizika katika kaburi la Abneri huko Hebroni.

< 2 Samuelin 4 >