< 2 Kuninkaiden 13 >

1 Juudan kuninkaan Jooaan, Ahasjan pojan, kahdentenakymmenentenä kolmantena hallitusvuotena tuli Jooahas, Jeehun poika, Israelin kuninkaaksi, ja hän hallitsi Samariassa seitsemäntoista vuotta.
Katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu alianza kutawala Israeli katika Samaria, naye akatawala miaka kumi na saba.
2 Ja hän teki sitä, mikä on pahaa Herran silmissä, ja vaelsi Jerobeamin, Nebatin pojan, synneissä, joilla tämä oli saattanut Israelin tekemään syntiä; hän ei luopunut niistä.
Akafanya maovu machoni pa Bwana kwa kufuata dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, na wala hakuziacha.
3 Niin Herran viha syttyi Israelia kohtaan, ja hän antoi heidät Hasaelin, Aramin kuninkaan, ja Benhadadin, Hasaelin pojan, käsiin koko siksi ajaksi.
Kwa hiyo hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Israeli na kwa muda mrefu akawaweka chini ya utawala wa Hazaeli mfalme wa Aramu, na Ben-Hadadi mwanawe.
4 Mutta Jooahas lepytti Herraa, ja Herra kuuli häntä, sillä hän näki Israelin sorron, kun Aramin kuningas sorti heitä.
Ndipo Yehoahazi akamsihi Bwana rehema, naye Bwana akamsikiliza, kwa maana aliona jinsi mfalme wa Aramu alivyokuwa akiwatesa Israeli vikali.
5 Ja Herra antoi Israelille vapauttajan, ja he pääsivät aramilaisten käsistä. Ja israelilaiset asuivat majoissansa niinkuin ennenkin.
Bwana akamtoa mwokozi kwa ajili ya Israeli, nao wakaokoka kutoka kwenye mamlaka ya Aramu. Hivyo Waisraeli wakaishi katika nyumba zao wenyewe kama ilivyokuwa hapo awali.
6 Eivät he kuitenkaan luopuneet Jerobeamin suvun synneistä, joilla hän oli saattanut Israelin tekemään syntiä, vaan he vaelsivat niissä; aserakin jäi paikoilleen Samariaan.
Lakini hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu, ambazo alisababisha Israeli kuzitenda, bali wakaendelea kuzitenda. Nguzo ya Ashera pia iliendelea kusimama katika Samaria.
7 Niin ei Herra jättänyt Jooahaalle väkeä enempää kuin viisikymmentä ratsumiestä, kymmenet sotavaunut ja kymmenentuhatta jalkamiestä; sillä Aramin kuningas oli hävittänyt ne ja pannut ne tomuksi, niinkuin puitaessa tulee tomua.
Hapakubaki kitu chochote katika jeshi la Yehoahazi isipokuwa wapanda farasi hamsini, magari kumi ya vita na askari wa miguu elfu kumi, kwa kuwa mfalme wa Aramu alikuwa amewaangamiza hao wengine na kuwafanya kama mavumbi wakati wa kupura nafaka.
8 Mitä muuta on kerrottavaa Jooahaasta, kaikesta, mitä hän teki, ja hänen urotöistänsä, se on kirjoitettuna Israelin kuningasten aikakirjassa.
Matukio mengine ya utawala wa Yehoahazi yote aliyoyafanya na mafanikio yake, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
9 Ja Jooahas meni lepoon isiensä tykö, ja hänet haudattiin Samariaan. Ja hänen poikansa Jooas tuli kuninkaaksi hänen sijaansa.
Yehoahazi akalala pamoja na baba zake, akazikwa huko Samaria. Naye Yehoashi mwanawe akawa mfalme baada yake.
10 Juudan kuninkaan Jooaan kolmantenakymmenentenä seitsemäntenä hallitusvuotena tuli Jooas, Jooahaan poika, Israelin kuninkaaksi, ja hän hallitsi Samariassa kuusitoista vuotta.
Katika mwaka wa thelathini na saba wa utawala wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutawala Israeli huko Samaria, naye akatawala miaka kumi na sita.
11 Hän teki sitä, mikä on pahaa Herran silmissä: hän ei luopunut mistään Jerobeamin, Nebatin pojan, synneistä, joilla tämä oli saattanut Israelin tekemään syntiä, vaan vaelsi niissä.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, na hakuacha dhambi yoyote kati ya zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda, bali aliendelea kuzitenda.
12 Mitä muuta on kerrottavaa Jooaasta, kaikesta, mitä hän teki, ja hänen urotöistään, kuinka hän soti Juudan kuningasta Amasjaa vastaan, se on kirjoitettuna Israelin kuningasten aikakirjassa.
Na kwa matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, yote aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita yake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
13 Ja Jooas meni lepoon isiensä tykö, ja Jerobeam istui hänen valtaistuimellensa. Ja Jooas haudattiin Samariaan Israelin kuningasten viereen.
Yehoashi akalala pamoja na baba zake, akazikwa Samaria pamoja na wafalme wa Israeli. Yeroboamu akawa mfalme baada yake.
14 Mutta kun Elisa sairasti kuolintautiansa, tuli Jooas, Israelin kuningas, hänen tykönsä. Ja kumartuneena hänen kasvojensa yli hän itki ja sanoi: "Isäni, isäni! Israelin sotavaunut ja ratsumiehet!"
Wakati huu, Elisha alikuwa anaumwa na ugonjwa ambao baadaye ulimuua. Yehoashi mfalme wa Israeli akashuka kwenda kumwona na kumlilia. Akalia, “Baba yangu! Baba yangu! Magari ya vita ya Israeli na wapanda farasi wake!”
15 Niin Elisa sanoi hänelle: "Nouda jousi ja nuolia". Ja hän nouti hänelle jousen ja nuolia.
Elisha akasema, “Leta upinde na baadhi ya mishale,” naye mfalme akafanya hivyo.
16 Sitten hän sanoi Israelin kuninkaalle: "Laske kätesi jouselle". Ja kun hän oli laskenut kätensä, pani Elisa kätensä kuninkaan kätten päälle.
Elisha akamwambia mfalme wa Israeli, “Shika upinde mikononi mwako.” Alipokwisha kuichukua, Elisha akaweka mikono yake juu ya mikono ya mfalme.
17 Ja hän sanoi: "Avaa ikkuna itään päin". Ja kun tämä oli avannut sen, sanoi Elisa: "Ammu". Ja hän ampui. Niin hän sanoi: "Herran voitonnuoli, voitonnuoli Aramia vastaan! Sinä olet voittava aramilaiset Afekissa perinpohjin."
Elisha akasema, “Fungua dirisha la mashariki,” naye akalifungua. Elisha akasema, “Piga mshale!” Naye akapiga mshale. Elisha akasema, “Mshale wa ushindi wa Bwana, mshale wa ushindi juu ya Aramu! Utawaangamiza Waaramu kabisa huko Afeki.”
18 Sitten hän sanoi: "Ota nuolet". Ja kun hän oli ne ottanut, sanoi hän Israelin kuninkaalle: "Lyö maahan". Niin hän löi kolme kertaa ja lakkasi sitten.
Kisha akasema, “Chukua mishale,” naye mfalme akaichukua. Elisha akamwambia, “Piga ardhi kwa hiyo mishale.” Akaipiga mara tatu, halafu akaacha.
19 Mutta Jumalan mies vihastui häneen ja sanoi: "Sinun olisi pitänyt lyödä viisi tai kuusi kertaa: silloin olisit voittanut aramilaiset perinpohjin. Mutta nyt olet voittava aramilaiset ainoastaan kolme kertaa."
Mtu wa Mungu akamkasirikia na akasema, “Ungepiga chini mara tano au sita, ndipo ungeishinda Aramu na kuiangamiza kabisa. Lakini sasa utaishinda mara tatu tu.”
20 Sitten Elisa kuoli, ja hänet haudattiin. Ja mooabilaisten partiojoukkoja tuli maahan vuosi vuodelta.
Elisha akafa, nao wakamzika. Vikosi vya Wamoabu vilikuwa vinashambulia nchi kwa vita kila mwaka wakati wa vuli.
21 Ja kerran, kun he haudatessaan erästä miestä näkivät partiojoukon, heittivät he miehen Elisan hautaan ja menivät matkoihinsa. Kun mies kosketti Elisan luita, virkosi hän ja nousi jaloilleen.
Ikawa Waisraeli fulani walipokuwa wanamzika mtu, ghafula wakaona kikosi cha washambuliaji, basi wakaitupa ile maiti ya yule mtu ndani ya kaburi la Elisha. Wakati ile maiti ilipogusa mifupa ya Elisha, yule mtu akafufuka na kusimama kwa miguu yake.
22 Hasael, Aramin kuningas, sorti Israelia, niin kauan kuin Jooahas eli.
Hazaeli mfalme wa Aramu aliwatesa Israeli wakati wote wa utawala wa Yehoahazi.
23 Mutta Herra oli heille laupias, armahti heitä ja kääntyi heidän puoleensa liiton tähden, jonka hän oli tehnyt Aabrahamin, Iisakin ja Jaakobin kanssa. Sillä hän ei tahtonut tuhota heitä, eikä hän ollut vielä heittänyt heitä pois kasvojensa edestä.
Lakini Bwana akawarehemu na akawahurumia, akaonyesha kujishughulisha nao kwa sababu ya Agano lake na Abrahamu, Isaki na Yakobo. Hadi leo, hajawaangamiza wala kuwafukuza mbele zake.
24 Ja Hasael, Aramin kuningas, kuoli, ja hänen poikansa Benhadad tuli kuninkaaksi hänen sijaansa.
Hazaeli mfalme wa Shamu akafa, naye Ben-Hadadi mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Ja Jooas, Jooahaan poika, otti Benhadadilta, Hasaelin pojalta, takaisin ne kaupungit, jotka tämä oli asevoimalla ottanut hänen isältänsä Jooahaalta. Kolme kertaa Jooas voitti hänet ja otti takaisin Israelin kaupungit.
Kisha Yehoashi mwana wa Yehoahazi akateka tena kutoka kwa Ben-Hadadi mwana wa Hazaeli ile miji aliyokuwa ameitwaa kwa vita kutoka kwa baba yake Yehoahazi. Yehoashi alimshinda mara tatu, hivyo akaweza kuiteka tena ile miji ya Waisraeli.

< 2 Kuninkaiden 13 >