< 1 Kuninkaiden 15 >

1 Ja kuningas Jerobeamin, Nebatin pojan, kahdeksantenatoista hallitusvuotena tuli Abiam Juudan kuninkaaksi.
Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya akawa mfalme wa Yuda,
2 Hän hallitsi kolme vuotta Jerusalemissa. Hänen äitinsä oli nimeltään Maaka, Abisalomin tytär.
naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
3 Ja hän vaelsi kaikissa isänsä synneissä, joita tämä oli tehnyt ennen häntä, eikä hänen sydämensä ollut ehyesti antautunut Herralle, hänen Jumalallensa, niinkuin hänen isänsä Daavidin sydän oli ollut.
Alitenda dhambi zote baba yake alizotenda kabla yake; moyo wake haukuwa mkamilifu kwa Bwana Mungu wake kama moyo wa Daudi baba yake ulivyokuwa.
4 Mutta Daavidin tähden Herra, hänen Jumalansa, antoi hänen lamppunsa palaa Jerusalemissa, korottamalla hänen jälkeläisekseen hänen poikansa ja pitämällä Jerusalemia pystyssä-
Pamoja na hayo, kwa ajili ya Daudi, Bwana Mungu wake akampa taa katika Yerusalemu kwa kumwinua mwana atawale badala yake na kwa kuifanya Yerusalemu kuwa imara.
5 koska Daavid oli tehnyt sitä, mikä on oikein Herran silmissä, eikä koko elinaikanaan ollut poikennut mistään, mitä hän on käskenyt, paitsi heettiläisen Uurian asiassa.
Kwa kuwa Daudi alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana na hakushindwa kushika maagizo yote ya Bwana siku zote za uhai wake, isipokuwa katika habari ya Uria, Mhiti.
6 Ja Abiam oli koko elinaikansa sodassa Jerobeamin kanssa.
Kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu wakati wote wa maisha ya Abiya.
7 Mitä muuta on kerrottavaa Abiamista ja kaikesta, mitä hän teki, se on kirjoitettuna Juudan kuningasten aikakirjassa. Mutta Abiam ja Jerobeam olivat sodassa keskenään.
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Abiya na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
8 Ja Abiam meni lepoon isiensä tykö, ja hänet haudattiin Daavidin kaupunkiin. Ja Aasa, hänen poikansa, tuli kuninkaaksi hänen sijaansa.
Naye Abiya akalala na baba zake akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake.
9 Israelin kuninkaan Jerobeamin kahdentenakymmenentenä hallitusvuotena tuli Aasa Juudan kuninkaaksi.
Katika mwaka wa ishirini wa utawala wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akawa mfalme wa Yuda,
10 Hän hallitsi neljäkymmentä yksi vuotta Jerusalemissa. Hänen äitinsä oli nimeltään Maaka, Abisalomin tytär.
naye akatawala katika Yerusalemu miaka arobaini na mmoja. Bibi yake aliitwa Maaka binti Abishalomu.
11 Ja Aasa teki sitä, mikä oli oikein Herran silmissä, niinkuin hänen isänsä Daavid,
Asa akatenda yaliyo mema machoni mwa Bwana, kama alivyokuwa ametenda Daudi baba yake.
12 ja toimitti haureelliset pyhäkköpojat pois maasta ja hävitti kaikki ne kivijumalat, jotka hänen isänsä olivat tehneet.
Akawafukuza mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu kutoka nchi na kuondoa sanamu zote ambazo baba zake walikuwa wametengeneza.
13 Jopa hän erotti äitinsä Maakan kuningattaren arvosta, koska tämä oli pystyttänyt inhotuksen Aseralle; ja Aasa kukisti inhotuksen ja poltti sen Kidronin laaksossa.
Hata akamwondoa bibi yake Maaka kwenye wadhifa wake kama mama malkia, kwa sababu alikuwa ametengeneza nguzo ya Ashera ya kuchukiza. Asa akaikata hiyo nguzo na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.
14 Mutta uhrikukkulat eivät hävinneet. Kuitenkin oli Aasan sydän ehyesti antautunut Herralle, niin kauan kuin hän eli.
Ijapokuwa hakuondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, moyo wa Asa ulikuwa umejiweka kwa Bwana kikamilifu maisha yake yote.
15 Ja hän vei Herran temppeliin isänsä pyhät lahjat ja omat pyhät lahjansa: hopeata, kultaa ja kaluja.
Akaleta ndani ya Hekalu la Bwana fedha na dhahabu na vile vyombo ambavyo yeye na baba yake walikuwa wameviweka wakfu.
16 Mutta Aasa ja Israelin kuningas Baesa olivat kaiken aikansa sodassa keskenään.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli siku zote za utawala wao.
17 Baesa, Israelin kuningas, lähti Juudaa vastaan ja linnoitti Raaman, estääkseen ketään pääsemästä Aasan, Juudan kuninkaan, luota tai hänen luokseen.
Mfalme Baasha wa Israeli akashambulia Yuda na kuweka ngome mji wa Rama ili kumzuia yeyote asitoke wala kuingia nchi ya Mfalme Asa wa Yuda.
18 Ja Aasa otti kaiken hopean ja kullan, mikä vielä oli jäljellä Herran temppelin ja kuninkaan linnan aarrekammioissa, ja antoi sen palvelijainsa haltuun; ja kuningas Aasa lähetti heidät Benhadadin, Tabrimmonin pojan, Hesjonin pojanpojan, Aramin kuninkaan, luo, joka asui Damaskossa, ja käski sanoa hänelle:
Kisha Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imeachwa katika hazina za Hekalu la Bwana na za jumba lake mwenyewe la kifalme. Akawakabidhi maafisa wake na kuwatuma kwa Ben-Hadadi mwana wa Tabrimoni, mwana wa Hezioni, mfalme wa Aramu, aliyekuwa akitawala Dameski.
19 "Onhan liitto meidän välillämme, minun ja sinun, niinkuin oli minun isäni ja sinun isäsi välillä. Katso, minä lähetän sinulle hopeata ja kultaa lahjaksi; mene ja riko Baesan, Israelin kuninkaan, kanssa tekemäsi liitto, että hän lähtisi pois minun kimpustani."
“Akasema na pawepo mkataba kati yangu na wewe, kama ulivyokuwepo kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, nimekuletea zawadi ya fedha na dhahabu. Sasa vunja mkataba wako na Baasha mfalme wa Israeli ili aniondokee mimi.”
20 Niin Benhadad kuuli kuningas Aasaa ja lähetti sotajoukkojensa päälliköt Israelin kaupunkeja vastaan ja valtasi Iijonin, Daanin, Aabel-Beet-Maakan ja koko Kinnerotin ynnä koko Naftalin maan.
Ben-Hadadi akakubaliana na Mfalme Asa na kutuma majemadari wa majeshi yake dhidi ya miji ya Israeli. Akaishinda miji ya Iyoni, Dani, Abel-Beth-Maaka na Kinerethi yote, pamoja na Naftali.
21 Kun Baesa kuuli sen, lakkasi hän linnoittamasta Raamaa ja jäi Tirsaan.
Wakati Baasha aliposikia hili, akaacha kuijenga Rama na akaenda kuishi Tirsa.
22 Mutta kuningas Aasa kutsui kokoon kaiken Juudan, vapauttamatta ketään. Ja he veivät pois kivet ja puut, joilla Baesa oli linnoittanut Raamaa. Niillä kuningas Aasa linnoitti Geban, joka on Benjaminissa, ja Mispan.
Kisha Mfalme Asa akatoa amri kwa Yuda yote, pasipo kumbagua hata mmoja, kubeba mawe na mbao kutoka Rama, ambazo Baasha alikuwa akitumia huko. Mfalme Asa akazitumia kujengea Geba iliyoko Benyamini na Mispa pia.
23 Mitä muuta kaikkea on kerrottavaa Aasasta, kaikista hänen urotöistään, kaikesta, mitä hän teki, ja kaupungeista, jotka hän rakensi, se on kirjoitettuna Juudan kuningasten aikakirjassa. Mutta vanhuutensa päivinä hän oli sairas jaloistaan.
Kwa matukio yote ya utawala wa Asa, mafanikio yake yote, yote aliyofanya na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda? Katika uzee wake, hata hivyo, alipata ugonjwa wa miguu.
24 Sitten Aasa meni lepoon isiensä tykö, ja hänet haudattiin isiensä viereen hänen isänsä Daavidin kaupunkiin. Ja hänen poikansa Joosafat tuli kuninkaaksi hänen sijaansa.
Kisha Asa akalala pamoja na baba zake na kuzikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Naye Yehoshafati mwanawe akawa mfalme baada yake.
25 Ja Naadab, Jerobeamin poika, tuli Israelin kuninkaaksi Aasan, Juudan kuninkaan, toisena hallitusvuotena, ja hän hallitsi Israelia kaksi vuotta.
Nadabu mwana wa Yeroboamu akawa mfalme wa Israeli katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Asa wa Yuda, naye akatawala Israeli kwa miaka miwili.
26 Hän teki sitä, mikä on pahaa Herran silmissä, ja vaelsi isänsä teitä ja hänen synnissänsä, jolla hän oli saattanut Israelin tekemään syntiä.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za baba yake na katika dhambi yake, ambayo alisababisha Israeli kuifanya.
27 Mutta Baesa, Ahian poika, Isaskarin sukua, teki salaliiton häntä vastaan, ja Baesa surmasi hänet Gibbetonin luona, joka oli filistealaisilla; sillä Naadab ja koko Israel piirittivät Gibbetonia.
Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya shauri baya dhidi yake, naye akamuua huko Gibethoni, mji wa Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli yote walipokuwa wameuzingira.
28 Baesa tappoi hänet Juudan kuninkaan Aasan kolmantena hallitusvuotena ja tuli kuninkaaksi hänen sijaansa.
Baasha akamuua Nadabu katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, naye Baasha akaingia mahali pake kuwa mfalme.
29 Kuninkaaksi tultuaan hän surmasi koko Jerobeamin suvun jättämättä Jerobeamin jälkeläisistä eloon ainoatakaan henkeä: hän hävitti heidät Herran sanan mukaan, jonka hän oli puhunut palvelijansa, siilolaisen Ahian, kautta-
Mara tu alipoanza kutawala, aliua jamaa yote ya Yeroboamu. Hakumwachia Yeroboamu yeyote aliyekuwa hai, bali aliwaangamiza wote, kulingana na neno la Bwana lililotolewa kupitia kwa mtumishi wake Ahiya Mshiloni,
30 niiden syntien tähden, jotka Jerobeam oli tehnyt ja joilla hän oli saattanut Israelin tekemään syntiä, siten vihoittaen Herran, Israelin Jumalan.
kwa sababu ya dhambi alizokuwa amezitenda Yeroboamu na kusababisha Israeli kuzitenda, tena kwa sababu alimkasirisha Bwana, Mungu wa Israeli.
31 Mitä muuta on kerrottavaa Naadabista ja kaikesta, mitä hän teki, se on kirjoitettuna Israelin kuningasten aikakirjassa.
Kwa matukio mengine ya utawala wa Nadabu na yote aliyofanya, je hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
32 Mutta Aasa ja Israelin kuningas Baesa olivat kaiken aikansa sodassa keskenään.
Kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli wakati wote wa utawala wao.
33 Aasan, Juudan kuninkaan, kolmantena hallitusvuotena tuli Baesa, Ahian poika, koko Israelin kuninkaaksi Tirsassa, ja hän hallitsi kaksikymmentä neljä vuotta.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akawa mfalme wa Israeli yote huko Tirsa, naye akatawala kwa miaka ishirini na minne.
34 Hän teki sitä, mikä on pahaa Herran silmissä, ja vaelsi Jerobeamin teitä ja hänen synneissänsä, joilla hän oli saattanut Israelin tekemään syntiä.
Akatenda maovu machoni pa Bwana, akienenda katika njia za Yeroboamu na dhambi yake, ambayo alikuwa amesababisha Israeli kuitenda.

< 1 Kuninkaiden 15 >