< Psalmien 98 >
1 Psalmi. Veisatkaat Herralle uusi veisu; sillä hän tekee ihmeitä. Hän saa voiton oikialla kädellänsä ja pyhällä käsivarrellansa.
Zaburi. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu; kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu umemfanyia wokovu.
2 Herra antaa tiettäväksi tehdä autuutensa: kansain edessä hän ilmoittaa vanhurskautensa.
Bwana ameufanya wokovu wake ujulikane na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.
3 Hän muistaa armonsa ja totuutensa Israelin huoneelle: kaikki maailman ääret näkevät meidän Jumalamme autuuden.
Ameukumbuka upendo wake na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli; miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.
4 Riemuitkaat Herralle kaikki maa: veisatkaat, ylistäkäät ja kiittäkäät.
Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote, ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;
5 Kiittäkäät Herraa kanteleella, kanteleella ja psalmilla,
mwimbieni Bwana kwa kinubi, kwa kinubi na sauti za kuimba,
6 Vaskitorvilla ja basunilla: riemuitkaat Herran, kuninkaan, edessä.
kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume: shangilieni kwa furaha mbele za Bwana, aliye Mfalme.
7 Meri pauhatkaan ja kaikki, mitä hänessä on, maan piiri ja jotka asuvat sen päällä.
Bahari na ivume na kila kiliomo ndani yake, dunia na wote wakaao ndani yake.
8 Kosket pauhatkaan ilosta, ja kaikki vuoret olkaan iloiset,
Mito na ipige makofi, milima na iimbe pamoja kwa furaha,
9 Herran edessä; sillä hän tulee maata tuomitsemaan: hän tuomitsee maan piirin vanhurskaudella ja kansat oikeudella.
vyote na viimbe mbele za Bwana, kwa maana yuaja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki na mataifa kwa haki.