< Psalmien 149 >
1 Halleluja! Veisatkaat Herralle uusi veisu: pyhäin seurakunnan pitää häntä kiittämän.
Msifuni Yahwe. Mwimbieni Yahwe wimbo mpya; imbeni sifa zake katika kusanyiko la waaminifu.
2 Iloitkaan Israel tekiässänsä: Zionin lapset riemuitkaan Kuninkaastansa.
Israeli ishangilie katika yeye aliye iumba; watu wa Sayuni na washangilie katika mfalme wao.
3 Heidän pitää tanssissa hänen nimeänsä kiittämän: harpuilla ja kanteleilla pitää heidän soittaman.
Nao walisifu jina lake kwa kucheza; na wamuimbie sifa yeye kwa ngoma na kinubi.
4 Sillä Herra rakastaa kansaansa: hän kunnioittaa nöyriä autuudella.
Kwa kuwa Yahwe hupata furaha katika watu wake; huwapa utukufu wanyeyekevu kwa wokovu.
5 Pyhäin pitää iloitseman kunnialla, ja kiittämän vuoteissansa.
Wacha Mungu wauchangilie ushindi; nao waimbe kwa furaha vitandani mwao.
6 Heidän suussansa pitää Jumalan ylistys oleman, ja kaksiteräiset miekat heidän käsissänsä,
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na panga mbili zenye makali mkononi mwao
7 Kostamaan pakanoille, ja rankaisemaan kansoja,
kutekeleza kisasi juu ya mataifa na matendo ya adhabu juu ya watu.
8 Heidän kuninkaitansa sitomaan kahleisiin, ja heidän jaloimpiansa rautakahleisiin,
Nao watawafunga wafalme wao kwa minyororo na wakuu wao kwa pingu za chuma. Watatekeleza hukumu ambayo imeandikwa.
9 Ja tekemään heille kirjoitetun oikeuden: tämä kunnia pitää kaikille hänen pyhillensä oleman, Halleluja!
Hii itakuwa ni heshima kwa ajili ya watakatifu wake wote. Msifuni Yahwe.