< Sananlaskujen 26 >

1 Niinkuin lumi suvella ja sede elonaikana, niin ei sovi tyhmälle kunnia.
Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2 Niinkuin lintu menee pois, ja pääskynen lentää, niin ei sovi salvaa kirous ilman syytä.
Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3 Hevoselle ruoska ja aasille ohjat, ja hullulle vitsa selkään.
Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4 Älä vastaa tyhmää hänen tyhmyytensä jälkeen, ettes myös sinä hänen kaltaiseksensa tulisi.
Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5 Vastaa tyhmää hänen tyhmyytensä jälkeen, ettei hän näkyisi viisaaksi silmissänsä.
Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6 Joka tyhmäin sanansaattajain kautta asian toimittaa, hän on niinkuin rampa jaloista, ja saa vahingon.
Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7 Niinkuin nilkku voi hypätä, niin tyhmä taitaa puhua viisaudesta.
Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8 Joka tyhmälle taritsee kunniaa, on niinkuin joku heittäisi kalliin kiven kiviroukkioon.
Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9 Sananlasku on tyhmäin suussa niinkuin orjantappura, joka juopuneen käsiin pistelee.
Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10 Taitava ihminen tekee kappaleen oikein; vaan joka taitamattoman palkkaa, hän sen turmelee.
Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
11 Niinkuin koira syö oksennuksensa, niin on hullu joka hulluutensa kertoo.
Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
12 Koskas näet jonkun, joka luulee itsensä viisaaksi, enempi on silloin toivoa tyhmästä kuin hänestä.
Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
13 Laiska sanoo: nuori jalopeura on tiellä, ja jalopeura kujalla.
Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
14 Laiska kääntelee itsiänsä vuoteella niinkuin ovi saranassa.
Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
15 Laiska panee kätensä poveensa: ja se tulee hänelle työlääksi saattaa suuhunsa jälleen.
Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
16 Laiska luulee itsensä viisaammaksi kuin seitsemän, jotka hyviä tapoja opettavat.
Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
17 Joka käy ohitse ja sekoittaa itsensä muiden riitoihin, hän on senkaltainen, joka koiraa korvista vetää.
Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
18 Niinkuin se, joka salaa ampuu, tarkoittaa joutsella ja tappaa,
Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
19 Niin on petollinen ihminen hänen lähimmäisillensä, ja sanoo: leikillä minä sen tein.
ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20 Kuin halot loppuvat, niin tuli sammuu, ja kuin kielikellot pannaan pois, niin riidat lakkaavat.
Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
21 Niinkuin hiilet tuleen, ja puut liekkiin, niin riitainen ihminen saattaa metelin.
Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
22 Panettelian sanat ovat niinkuin haavat, ja käyvät läpi sydämen.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
23 Viekas kieli ja paha sydän on niinkuin saviastia hopian savulla juotettu.
Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
24 Vihamien teeskelee itsensä toisin puheellansa; mutta petos on hänen sydämessänsä.
Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
25 Kuin hän liehakoitsee makeilla puheillansa, niin älä usko häntä; sillä seitsemän kauhistusta on hänen sydämessänsä.
Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
26 Joka pitää salavihaa, tehdäksensä vahinkoa, hänen pahuutensa tulee ilmi kokouksissa.
Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
27 Joka kuopan kaivaa, hän lankee siihen, ja joka kiven vierittää, se kierittää sen itse päällensä.
Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
28 Petollinen kieli vihaa rangaistusta, ja suu, joka myötäkielin puhuu, saattaa kadotukseen.
Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.

< Sananlaskujen 26 >