< Sananlaskujen 25 >

1 Nämät ovat myös Salomon sananlaskut, jotka Hiskian ja Juudan kuninkaan miehet ovat tähän panneet tykö.
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 Se on Jumalan kunnia, salata asiaa; mutta kuninkaan kunnia, tutkia asiaa.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Taivas on korkia ja maa syvä, ja kuninkaan sydän on tutkimatoin.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 Raiska otetaan hopiasta pois, niin siitä tulee puhdas astia.
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 Jos jumalatoin otetaan pois kuninkaan kasvoin edestä, niin hänen istuimensa vanhurskaudella vahvistetaan.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 Älä koreile kuninkaan nähden, ja älä astu suurten sialle.
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 Sillä se on sinulle parempi, koska sinulle sanotaan: astu tänne ylemmä! kuin ettäs ruhtinaan edessä alennettaisiin, jota sinun silmäs näkisivät.
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 Älä ole pikainen riitelemään, ettes tiedä mitäs teet, koska lähimmäiseltäs häväisty olet?
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 Toimita asias lähimmmäises kanssa, älä ilmoita toisen salaisuutta,
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 Ettei se, joka sen kuulee, sinua häpäisisi, ja ettei sinun paha sanomas lakkaa.
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 Sana, aikanansa puhuttu, on niinkuin kultainen omena hopiamaljassa.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 Koska viisas rankaisee sitä, jaka häntä kuulee, se on niinkuin korvarengas, ja niinkuin kaunistus parhaasta kullasta.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 Niinkuin lumen kylmä elonaikana, niin on uskollinen sanansaattaja sille, joka hänen lähettänyt on, ja virvoittaa herransa sielun.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Joka paljon puhuu ja vähän pitää, hän on niinkuin tuuli ja pilvi ilman sadetta.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 Kärsivällisyydellä päämies lepytetään, ja siviä kieli pehmittää kovuuden.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 Jos sinä löydät hunajaa, niin syö tarpeekses, ettes ylönpalttisesti tulisi ravituksi, ja antaisi sitä ylen.
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 Anna jalkas harvoin tulla lähimmäises huoneeseen, ettei hän suuttuis sinuun, ja vihaisi sinua.
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Joka väärää todistusta puhuu lähimmäistänsä vastaan, hän on vasara, miekka ja terävä nuoli.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Pilkkaajan toivo hädän aikana on niinkuin murrettu hammas, ja vilpisteleväinen jalka.
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 Joka murheellisen sydämen edessä virsiä veisaa, hän on niinkuin se, joka vaatten tempaa pois talvella, ja etikka pleikun päällä.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Jos sinun vihamiehes isoo, niin ravitse häntä leivällä: jos hän janoo, niin juota häntä vedellä;
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 Sillä sinä kokoot hiilet hänen päänsä päälle, ja Herra kostaa sen sinulle.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Pohjatuuli tuottaa sateen, ja salainen kieli saattaa kasvot vihaisiksi.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
24 Parempi on istus katon kulmalla, kuin riitaisen vaimon kanssa yhdessä huoneessa.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 Hyvä sanoma kaukaiselta maalta on kylmän veden kaltainen janoovaiselle sielulle.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Vanhurskas, joka jumalattoman eteen lankee, on niinkuin sekoitettu kaivo ja turmeltu lähde.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 Joka paljon hunajaa syö, ei se ole hyvä, ja joka työtläitä asioita tutkii, se tulee hänelle työlääksi.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 Joka ei taida hillitä henkeänsä, hän on niinkuin hävitetty kaupunki ilman muuria.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< Sananlaskujen 25 >