< 4 Mooseksen 7 >

1 Ja tapahtui sinä päivänä, koska Moses oli pannut Tabernaklin ylös, voiteli hän sen ja pyhitti sen, ja kaikki sen astiat, niin myös alttarin ja kaikki sen astiat: ja voiteli ne, ja pyhitti ne.
Mose alipomaliza kuisimamisha Maskani, aliitia mafuta na kuiweka wakfu pamoja na samani zake zote. Pia alitia madhabahu mafuta na kuiweka wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
2 Niin uhrasivat Israelin päämiehet, jotka ylimmäiset olivat isäinsä huoneessa; sillä he olivat päämiehet sukukuntain ylitse, ja seisoivat ylimmäisessä siassa heidän seassansa, jotka luetut olivat,
Ndipo viongozi wa Israeli, wale wakuu wa jamaa waliokuwa viongozi wa kabila wasimamizi wa wale waliohesabiwa, wakatoa sadaka.
3 Ja toivat uhrinsa Herran eteen: kuusi peitettyä vaunua ja kaksitoistakymmentä härkää, aina vaunun kahden päämiehen edestä; mutta härjän itsekunkin edestä, ja toivat ne majan eteen.
Walizileta kama matoleo yao mbele za Bwana: magari sita ya kukokotwa yaliyofunikwa, pamoja na maksai kumi na wawili; yaani maksai mmoja kutoka kwa kila kiongozi, na gari moja la kukokotwa kutoka kwa kila viongozi wawili. Haya waliyaleta mbele ya Maskani.
4 Ja Herra puhui Mosekselle, sanoen:
Bwana akamwambia Mose,
5 Ota heiltä, että ne palvelisivat seurakunnan majan palveluksessa ja anna ne Leviläisille, itsekullekin virkansa jälkeen.
“Vikubali vitu hivi kutoka kwao, ili viweze kutumika katika kazi kwenye Hema la Kukutania. Wapatie Walawi kama kazi ya kila mtu itakavyohitaji.”
6 Niin otti Moses vaunut ja härjät, ja antoi ne Leviläisille.
Hivyo Mose akachukua yale magari ya kukokotwa pamoja na maksai, na kuwapa Walawi.
7 Kaksi vaunua ja neljä härkää antoi hän Gersonin lapsille, heidän virkansa jälkeen.
Aliwapa Wagershoni magari mawili ya kukokotwa na maksai wanne, kama walivyohitaji kwa kazi yao,
8 Neljä vaunua ja kahdeksan härkää antoi hän Merarin lapsille, heidän virkansa jälkeen, Itamarin, papin Aaronin pojan käden alla.
na pia aliwapa Wamerari magari manne ya kukokotwa na maksai wanane, kama kazi yao ilivyohitaji. Wote walikuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Aroni.
9 Mutta Kahatin lapsille ei hän mitään antanut; sillä heillä oli pyhän virka, ja piti kantaman olallansa.
Lakini Mose hakuwapa Wakohathi chochote kati ya hivyo, kwa sababu walitakiwa kubeba vitu vitakatifu mabegani mwao, vile walikuwa wanawajibika.
10 Ja päämiehet uhrasivat alttarin vihkimiseksi, sinä päivänä koska se voideltu oli, ja uhrasivat lahjansa alttarin eteen.
Wakati madhabahu yalitiwa mafuta, viongozi walileta sadaka zao kwa ajili ya kule kuwekwa wakfu kwake na kuziweka mbele ya madhabahu.
11 Ja Herra sanoi Mosekselle: anna jokaisen päämiehen tuoda uhrinsa, itsekunkin päivänänsä alttarin vihkimiseksi.
Kwa maana Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Kila siku kiongozi mmoja ataleta sadaka yake ili kuwekwa wakfu madhabahu.”
12 Ensimäisenä päivänä uhrasi lahjansa Nahesson, Amminadabin poika, Juudan sukukunnasta.
Yule ambaye alileta sadaka yake siku ya kwanza alikuwa Nashoni, mwana wa Aminadabu, wa kabila la Yuda.
13 Ja hänen lahjansa oli yksi hopiavati, joka painoi sata ja kolmekymmentä sikliä, yksi hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: ne molemmat täynnänsä öljyllä sekoitettuja sämpyläjauhoja, ruokauhriksi;
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
14 Siihen kultainen lusikka, jossa oli kymmenen sikliä kultaa, täynnänsä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
15 Yksi nuori mulli, yksi oinas, yksi vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
16 Yksi kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
17 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Nahessonin Amminadabin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
18 Toisena päivänä uhrasi Netaneel, Suarin poika, Isaskarin päämies.
Siku ya pili yake Nethaneli mwana wa Suari, kiongozi wa kabila la Isakari, alileta sadaka yake.
19 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
20 Siihen kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnänsä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
21 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
22 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
23 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Netaneelin Suarin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Suari.
24 Kolmantena päivänä Sebulonin lasten päämies, Eliab Helonin poika.
Siku ya tatu Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa kabila la Zabuloni, alileta sadaka yake.
25 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
26 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
27 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
28 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
29 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Eliabin Helonin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana wa Heloni.
30 Neljäntenä päivänä Rubenin lasten päämies, Elisur Sedeurin poika.
Siku ya nne Elisuri mwana wa Shedeuri, kiongozi wa kabila la Reubeni, alileta sadaka yake.
31 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
32 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa täynnänsä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
33 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
34 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
35 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Elisurin Sedeurin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elisuri mwana wa Shedeuri.
36 Viidentenä päivänä Simeonin lasten päämies, Selumiel SuriSaddain poika.
Siku ya tano Shelumieli mwana wa Surishadai, kiongozi wa watu wa Simeoni, alileta sadaka yake.
37 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
38 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnänsä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
39 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
40 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
41 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Selumielin SuriSaddain pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Shelumieli mwana wa Surishadai.
42 Kuudentena päivänä Gadin lasten päämies, Eliasaph Deguelin poika.
Siku ya sita Eliasafu mwana wa Deueli, kiongozi wa watu wa Gadi, alileta sadaka yake.
43 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
44 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnänsä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
45 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
46 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
47 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Eliasaphin Deguelin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deueli.
48 Seitsemäntenä päivänä Ephraimin lasten päämies, Elisama Ammihudin poika.
Siku ya saba Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa watu wa Efraimu, alileta sadaka yake.
49 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
50 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnänsä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
51 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
52 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
53 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Elisaman Ammihudin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elishama mwana wa Amihudi.
54 Kahdeksantena päivänä Manassen lasten päämies, Gamliel Pedatsurin poika.
Siku ya nane Gamalieli mwana wa Pedasuri, kiongozi wa watu wa Manase, alileta sadaka yake.
55 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
56 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
57 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
58 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
59 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Gamlielin Pedatsurin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Gamalieli mwana wa Pedasuri.
60 Yhdeksäntenä päivänä BenJaminin lasten päämies, Abidan Gideonin poika.
Siku ya tisa Abidani mwana wa Gideoni, kiongozi wa watu wa Benyamini, alileta sadaka yake.
61 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
62 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
63 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
64 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
65 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Abidan Gideonin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gideoni.
66 Kymmenentenä päivänä Danin lasten päämies, AhiEser AmmiSaddain poika.
Siku ya kumi Ahiezeri mwana wa Amishadai, kiongozi wa watu wa Dani, alileta sadaka yake.
67 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä sämpyläjauhoja, sekoitetuita öljyllä, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
68 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
69 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
70 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
71 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on AhiEserin AmmiSaddain pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.
72 Ensimäisenätoistakymmenentenä päivänä Asserin lasten päämies, Pagiel Okranin poika.
Siku ya kumi na moja Pagieli mwana wa Okrani, kiongozi wa watu wa Asheri, alileta sadaka yake.
73 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä öljyllä sekoitettuja sämpyläjauhoja, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
74 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
75 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
76 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
77 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Pagielin Okranin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
78 Toisenatoistakymmenentenä päivänä Naphtalin lasten päämies, Ahira Enanin poika.
Siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa watu wa Naftali, alileta sadaka yake.
79 Hänen lahjansa oli hopiavati, joka maksoi sata ja kolmekymmentä sikliä, hopiamalja, joka maksoi seitsemänkymmentä sikliä, pyhän siklin jälkeen: molemmat täynnä öljyllä sekoitettuja sämpyläjauhoja, ruokauhriksi,
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
80 Kultainen lusikka, joka maksoi kymmenen sikliä kultaa, täynnä suitsutusta,
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
81 Mulli karjasta, oinas, vuosikuntainen karitsa, polttouhriksi,
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
82 Kauris syntiuhriksi,
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
83 Ja kiitosuhriksi kaksi härkää, viisi oinasta, viisi kaurista, ja viisi vuosikuntaista karitsaa. Tämä on Ahiran Enanin pojan lahja.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahira mwana wa Enani.
84 Tämä on alttarin vihkimys sinä päivänä, jona se voideltiin, johonka Israelin lasten ruhtinaat uhrasivat: kaksitoistakymmentä hopiavatia, kaksitoistakymmentä hopiamaljaa, kaksitoistakymmentä kultaista lusikkaa,
Hizi ndizo zilikuwa sadaka za viongozi wa Israeli madhabahu yalipowekwa wakfu, wakati yalitiwa mafuta: sahani kumi na mbili za fedha, bakuli kumi na mbili za fedha za kunyunyizia, na masinia kumi na mawili ya dhahabu.
85 Niin että jokainen vati painoi sata ja kolmekymmentä sikliä hopiaa, ja jokainen malja seitsemänkymmentä sikliä, niin että kaikkein astiain hopian luku juoksi kaksituhatta ja neljäsataa sikliä, pyhän siklin jälkeen.
Kila sahani ya fedha ilikuwa na uzito wa shekeli 130, na kila bakuli la fedha la kunyunyizia lilikuwa na uzito wa shekeli sabini. Masinia yote kumi na mawili yalikuwa na uzito wa shekeli 2,400kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
86 Ja ne kaksitoistakymmentä kultaista lusikkaa, jotka suitsutusta täynnä olivat, jokainen painoi kymmenen sikliä, pyhän siklin jälkeen, niin että luku lusikkain kullasta juoksi sata ja kaksikymmentä sikliä.
Sahani kumi na mbili za dhahabu zilizojazwa uvumba zilikuwa na uzito wa shekeli kumi kila moja, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Kwa jumla, sahani za dhahabu zilikuwa na uzito wa shekeli 120.
87 Eläinten luku polttouhriksi, kaksitoistakymmentä mullia, kaksitoistakymmentä oinasta, kaksitoistakymmentä vuosikuntaista karitsaa, ja heidän ruokauhrinsa, ja kaksitoistakymmentä kaurista syntiuhriksi.
Jumla ya wanyama waliotolewa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa walikuwa fahali kumi na wawili wachanga, kondoo dume kumi na wawili na wana-kondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja, pamoja na sadaka zao za nafaka. Mbuzi waume kumi na wawili walitolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi.
88 Ja karjan luku kiitosuhriksi oli neljä härkää kolmattakymmentä, kuusikymmentä oinasta, kuusikymmentä kaurista, kuusikymmentä vuosikuntaista karitsaa. Tämä on alttarin vihkimys koska se voideltiin.
Jumla ya wanyama kwa ajili ya dhabihu ya sadaka ya amani walikuwa maksai ishirini na wanne, kondoo dume sitini, mbuzi dume wa mwaka mmoja sitini na wana-kondoo dume wa mwaka mmoja sitini. Hizi ndizo zilikuwa sadaka zilizoletwa kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu baada ya kutiwa mafuta.
89 Ja koska Moses meni seurakunnan majaan, että häntä siellä puhuteltaisiin, niin kuuli hän äänen puhuvan kanssansa armoistuimelta, joka oli todistuksen arkin päällä, kahden Kerubimin vaiheella, ja sieltä puhuteltiin häntä.
Mose alipoingia kwenye Hema la Kukutania kuzungumza na Bwana, alisikia sauti ikisema naye kutoka kati ya wale makerubi wawili waliokuwa juu ya kile kiti cha rehema, juu ya Sanduku la Ushuhuda. Mose akazungumza naye.

< 4 Mooseksen 7 >