< 2 Samuelin 8 >
1 Ja sitte tapahtui, että David löi Philistealaiset ja alensi heitä; ja David otti orjuuden suitset Philistealaisten kädestä
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
2 Ja hän löi Moabilaiset, pani heidät maahan makaamaan ja mittasi heitä nuoralla: ja hän mittasi kaksi nuoraa tapettavaksi ja yhden nuoran elämään jätettäväksi, ja Moabilaiset tulivat Davidin palveliaksi, ja he kantoivat hänelle lahjoja.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
3 David löi myös HadadEserin, Rehobin pojan Zoban kuninkaan, hänen mennessä asettamaan kättänsä Euphratin virran tykö.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
4 Ja David otti heistä tuhannen ja seitsemänsataa hevosmiestä ja kaksikymmentä tuhatta jalkamiestä kiinni, ja raiskasi kaikki vaunuhevoset, ja sata vaunua jätti heistä.
Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
5 Niin tulivat Syrialaiset Damaskusta auttamaan HadadEseriä, Zoban kuningasta; ja David löi Syrialaisista kaksikolmattakymmentä tuhatta miestä.
Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 Ja David asetti vartiat Syrian Damaskuun. Näin tulivat Syrialaiset Davidin palveliaksi ja kantoivat hänelle lahjoja; sillä Herra autti Davidia, kuhunka ikänä hän meni.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 Ja David otti HadadEserin palveliain kultaiset kilvet ja vei ne Jerusalemiin.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 Mutta Betasta ja Berotaista, HadadEserin kaupungeista, otti kuningas David ylen paljon vaskea.
Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
9 Kuin Toi, Hamatin kuningas kuuli Davidin lyöneen kaikki HadadEserin sotaväen,
Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 Lähetti hän poikansa Joramin kuningas Davidin tykö, tervehtimään häntä ystävällisesti ja siunaamaan häntä, että hän soti HadadEserin kanssa ja löi hänen; sillä Toi soti HadadEserin kanssa; ja hänen kädessänsä olivat hopiaiset, kultaiset ja vaskiset astiat.
akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
11 Ne myös kuningas David pyhitti Herralle, sen hopian ja kullan kanssa, jonka hän pyhitti Herralle kaikilta pakanoilta, jotka hän vaatinut oli allensa:
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
12 Syriasta ja Moabista, Ammonin lapsilta, Philistealaisilta, Amalekilaisilta, niin myös HadadEserin, Rehobin pojan, Zoban kuninkaan saaliista.
yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 Ja David teki itsensä kuuluisaksi, kuin hän palasi lyömästä Syrialaisia Suolalaaksossa, kahdeksantoistakymmentä tuhatta.
Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
14 Ja hän asetti vartiat koko Edomiin, ja koko Edom oli Davidin alla; sillä Herra autti Davidia, kuhunka ikänä hän meni.
Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 Niin oli David kaiken Israelin kuningas, ja hän toimitti lain ja oikeuden kaikelle kansallensa.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
16 Ja Joab, ZeruJan poika oli sotajoukon päällä, mutta Josaphat, Ahiludin poika oli kansleri.
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
17 Zadok, Ahitobin poika ja Ahimelek, AbJatarin poika olivat papit; Seraja oli kirjoittaja.
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
18 Benaja, Jojadan poika oli Kretin ja Pletin päällä; ja Davidin pojat olivat papit.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.