< Matteus 24 >
1 Kui Jeesus oli templist lahkumas, tulid jüngrid tema juurde ja osutasid uhkelt templi hoonetele.
Yesu alitoka hekaluni na kwenda zake. Wanafunzi wake walimwendea na kumuonesha majengo ya hekalu.
2 Aga Jeesus vastas: „Kas näete kõiki neid hooneid? Ma ütlen teile tõtt: neis ei jää üht kivi teise peale. Iga viimane kui üks variseb raginal maha!“
Laikni aliwajibu na kuwaambia, “Je, hamuyaoni mambo haya yote? Kweli nawaambia, hakuna jiwe litalobaki juu ya lingine bila kubomolewa.”
3 Kui Jeesus istus Õlimäel, tulid jüngrid omaette olles tema juurde ja küsisid: „Räägi meile palun, millal see toimub. Mis on sinu tulemise ja maailma lõpu märk?“ (aiōn )
Na alipokaa katika Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake walimwendea kwa faragha na kusema, “Tuambie, mambo haya yatatokea lini? Kitu gani kitakuwa dalili ya kuja kwako na mwisho wa ulimwengu?” (aiōn )
4 „Ärge laske kellelgi end eksitada, “vastas Jeesus.
Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Iweni makini kwamba asije mtu akawapotosha.
5 „Paljud väidavad end minu olevat, öeldes: „Mina olen Messias“, ja petavad paljusid.
Kwa kuwa wengi watakuja kwa jina langu. Watasema, 'Mimi ndiye Kristo', na watawapotosha wengi.
6 Te kuulete sõdadest ja kuuldusi sõdadest, kuid ärge olge ärevil. See kõik peab toimuma, kuid see ei ole lõpp.
Mtasikia vita na taarifa za vita. Angalieni msije mkawa na wasiwasi, kwa kuwa mambo haya hayabudi kutokea; lakini ule mwisho utakuwa bado.
7 Rahvad ründavad teisi rahvaid ja kuningriigid võitlevad teiste kuningriikide vastu. Paljudes paikades on näljahäda ja maavärinaid,
Kwa kuwa taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na matetemeko ya ardhi katika sehemu mbalimbali.
8 kuid kõik see on alles sünnitusvalude algus.
Lakini mambo haya yote ni mwanzo tu wa uchungu wa kujifungua.
9 Siis teid vahistatakse, kiusatakse taga ja tapetakse. Kõik vihkavad teid minu pärast.
Ndipo watawatoa kwa ajili ya mateso na kuwaua. Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.
10 Sel ajal loobuvad paljud usklikud uskumast. Nad reedavad ja vihkavad üksteist.
Ndipo wengi watajikwaa na kusalitiana na watachukiana wenyewe kwa wenyewe.
11 Palju valeprohveteid tuleb ja nad petavad paljusid.
Manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi.
12 Suureneva kurjuse tõttu jahtub paljude armastus,
Kwa sababu uovu utaongezeka, upendo wa wengi utapoa.
13 aga kes lõpuni vastu peavad, need saavad päästetud.
Lakini atakaye vumilia mpaka mwisho, ataokolewa.
14 Head sõnumit kuningriigist kuulutatakse kogu maailmas, nii et kõik võivad seda kuulda, ja siis tuleb lõpp.
Hii Injili ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu mzima kama ushuhuda kwa mataifa yote. Na ndipo ule mwisho utafika.
15 Nii et kui te näete pühas paigas seisvat „rüvetavat ebajumalust“, millest prohvet Taaniel rääkis (kes seda loeb, mõelgu hoolikalt järele),
Kwa hiyo, mtakapoona chukizo la uharibifu, lililosemwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu [asomaye na afahamu],
16 siis need, kes elavad Juudamaal, peaksid põgenema mägedesse.
ndipo walioko Yuda wakimbilie milimani.
17 See, kes on katusel, ei tohi tulla alla majast midagi ära tooma.
Na yule aliyeko juu ya paa la nyumba asiweze kuteremka chini kuchukua kitu chochote kutoka ndani ya nyumba yake,
18 See, kes on väljas põllul, ei tohi minna tagasi kuube võtma.
naye aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
19 Kui kohutav on see neile, kes on sel ajal lapseootel või imetavad!
Lakini ole wao ambao wana mtoto na wale ambao wananyonyesha katika siku hizo!
20 Palvetage, et teil ei oleks vaja põgeneda talvel ega hingamispäeval.
Ombeni kwamba kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.
21 Sest sel ajal on kohutav tagakiusamine, kohutavam kui miski, mis on toimunud maailma algusest kuni selle ajani, ja mida ei juhtu enam kunagi uuesti.
Kwa kuwa kutakuwa na dhiki kuu, ambayo haijawahi kuwapo tangu kuumbwa kwa ulimwengu hadi sasa, na wala haitakuwapo tena.
22 Kui neid päevi ei lühendataks, ei pääseks keegi, aga valitute pärast lühendatakse seda aega.
Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna ambaye angeokoka. Lakini kwa sababu ya wateule, siku hizo zitafupishwa.
23 Nii et kui keegi ütleb teile: „Vaata, siin on Messias!“või „Vaata, seal!“, ärge uskuge seda.
Kisha ikiwa mtu yeyote atawaambia 'Tazama, Kristo yuko hapa! au, 'Kristo yuko kule' msiamini maneno hayo.
24 Sest valemessiaid ilmub ja ka valeprohveteid ning nad teevad uskumatuid tunnustähti ja imetegusid, et petta ära ka valitud, kui see oleks võimalik.
Kwa kuwa Makristo wa uongo na manabii wa uongo watakuja na kuonesha ishara kubwa na maajabu, kwa kusudi la kupotosha, kama ingewezekana hata na wateule.
25 Pange tähele, et ma rääkisin teile sellest enne, kui see toimub.
Tazameni, nimewatahadharisha kabla ya mambo hayo kutokea.
26 Nii et kui öeldakse: „Vaata, ta on väljas kõrbes!“, ärge minge sinna vaatama; või kui öeldakse: „Vaata, ta on salaja siin!“, ärge uskuge seda.
Kwa hiyo, ikiwa watawaambia, ''Kristo yuko jangwani,' msiende huko jangwani. Au, 'Tazameni, yuko ndani ya nyumba,' msiamini maneno hayo.
27 Sest inimese Poja tulemine on nagu välk, mis sähvatab eredalt idast läände.
Kama vile radi inavyomulika kutokea mashariki na kuangaza hadi magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
28 „Kus on korjus, sinna kogunevad raisakotkad.“
Popote ulipo mzoga, huko ndiko tai wakusanyikapo.
29 Aga kohe pärast seda tagakiusamise aega läheb päike pimedaks, kuu ei sära, tähed langevad taevast ja taeva vägesid kõigutatakse.
Lakini mara baada ya dhiki kuu ya siku zile, Jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbinguni zitatikisika.
30 Siis ilmub taevasse inimese Poja tunnustäht ja kõik maailma rahvas leinab. Nad näevad inimese Poega tulemas taeva pilvedel väe ja särava hiilgusega.
Ndipo ishara ya Mwana wa Adamu itaonekana angani, na makabila yote ya dunia wataomboleza. Watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu ya angani kwa nguvu na utukufu mkuu.
31 Pasunahäälega läkitab ta inglid koguma oma valituid igalt poolt, ühest taeva ja maa otsast teiseni.
Atawatuma malaika wake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwingine.
32 Õppige näitlikku õppetundi viigipuust. Kui puul kasvavad õrnad võsud ja lehed hakkavad võrsuma, siis teate, et suvi on tulemas.
Jifunzeni somo kutokana na mti mtini. Mara tu tawi linapochipuka na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kinakaribia.
33 Samamoodi kui te näete kõike seda toimumas, siis teadke, et tema tulemine on lähedal, õigupoolest on see otse ukse taga!
Hivyo pia, mtakapoona mambo haya yote, mnapaswa kujua kwamba amekaribia, karibu na malango.
34 Ma ütlen teile tõtt: see põlvkond ei kao enne, kui kõik see on toimunud.
Kweli nawaambia, kizazi hiki hakitapita, hadi mambo yote haya yatakuwa yametokea.
35 Taevas ja maa võivad kaduda, aga minu sõnad ei kao.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36 Aga keegi ei tea päeva ega tundi, millal see toimub, ei inglid taevas ega Poeg. Ainult Isa teab.
Lakini kuhusu siku ile na saa hakuna mtu ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, bali Baba peke yake.
37 Kui inimese Poeg tuleb, on see nagu Noa ajal.
Kama vile ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
38 See on nagu enne veeuputust, kui nad sõid ja jõid, võtsid naisi ja läksid mehele, lausa päevani, mil Noa läks laeva.
Kwa kuwa katika siku hizo kabla ya gharika watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa hadi siku ile ambayo Nuhu aliingia katika safina,
39 Nad ei mõistnud, mis hakkab toimuma, kuni tuli uputus ja pühkis nad kõik minema. Nii on ka inimese Poja tulemine.
na hawakujua kitu chochote hadi gharika ilipokuja na kuwasomba wote - ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
40 Kaks meest töötavad põllul. Üks võetakse, teine jäetakse maha.
Ndipo watu wawili watakuwa shambani- mmoja atachukuliwa, na mmoja ataachwa nyuma.
41 Kaks naist jahvatavad veskiga vilja. Üks võetakse, teine jäetakse maha.
Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja - mmoja atachukuliwa, na mmoja atabaki.
42 Nii et olge valvsad, sest te ei tea, mis päeval teie Issand tuleb.
Kwa hiyo, kuweni macho kwa sababu hamjui ni siku gani ambayo atakuja Bwana wenu.
43 Aga võtke arvesse seda: kui majaomanik teaks aega, mil varas tuleb, oleks ta valvel. Ta ei laseks oma majja sisse murda ja sealt röövida.
Lakini mjue kwamba, ikiwa bwana mwenye nyumba angejua ni saa ipi ambayo mwizi angekuja, angekesha na asingeruhusu nyumba yake kuvamiwa.
44 Ka teie peate olema valmis, sest inimese Poeg tuleb ajal, mil te teda ei oota.
Kwa hiyo, pia mnapaswa kuwa tayari, kwa kuwa Mwana wa Adamu atakuja katika saa msiyoitarajia.
45 Sest kes on usaldusväärne ja tähelepanelik sulane? See on see, kelle isand paneb oma majapidamise eest hoolitsema, et ta varustaks neid toiduga õigel ajal.
Hivyo ni nani aliye mwaminifu, mtumwa mwenye akili, ambaye bwana wake amempa madaraka juu ya walio katika nyumba yake, ili awape chakula kwa wakati unaofaa?
46 Kui hea on selle sulase jaoks, kui isand tagasi tulles leiab ta seda tegemas!
Amebarikiwa mtumishi huyo, ambaye bwana wake atamkuta akifanya hivyo wakati ajapo.
47 Ma ütlen teile tõtt: isand paneb selle sulase vastutama kõige eest, mis tal on.
Kweli nawaambia kwamba bwana atamweka juu ya kila kitu kilicho chake.
48 Aga kui see sulane oleks nurjatu, ütleks ta endale: „Mu isandal läheb kaua aega“,
Lakini kama mtumwa mwovu akisema moyoni mwake, 'Bwana wangu amekawia,'
49 ning ta hakkaks teisi sulaseid peksma, pidutsema ning joobnutega jooma.
na akaanza kuwapiga watumishi wake, na akala na kulewa vileo,
50 Siis selle sulase isand tuleb tagasi siis, kui sulane ei oota, ajal, mil ta ei tea.
Bwana wa mtumwa huyo atakuja katika siku ambayo haitarajii, na katika saa ambayo haijui.
51 Ta raiub ta tükkideks ja kohtleb samamoodi nagu silmakirjatsejaid, saates ta paika, kus on nutmine ja hammaste kiristamine.
Bwana wake atamkata vipande viwili na kumweka katika nafasi moja sawa na wanafiki, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.