< Luuka 1 >
1 Nagu sa tead, on paljud teised üritanud kirja panna seda, mis on täide läinud ja puudutab ka meid.
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 Nende jutustused põhinesid esimeste pealtnägijate ja Sõna kuulutajate tõenditel
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 ja ka mina otsustasin, et kuna olen kõike seda algusest peale väga hoolikalt jälginud, oleks hea mõte kõigest toimunust kirja panna täpne jutustus.
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 Tegin seda, kallis Teofilos, et sa võiksid olla kindel, et see, mida sulle õpetati, on täiesti usaldusväärne.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 Sel ajal kui Heroodes oli Juudamaa kuningas, oli üks preester nimega Sakarias, kes oli pärit Abija preesterlikust rühmast. Ta oli abielus Eliisabetiga, kes põlvnes samuti preester Aaronist.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 Nad mõlemad tegid, mis oli Jumala ees õige, ning järgisid hoolikalt kõiki Issanda käske ja määrusi.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 Neil ei olnud lapsi, sest Eliisabet ei olnud selleks suuteline, ja nad mõlemad olid juba vanad.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Kui Sakarias teenis preestrina Jumala ees oma preesterlikus rühmas,
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 valiti ta vastavalt preestrite tavale liisu heitmisega Issanda templisse sisenema ja suitsutusrohtu põletama.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 Suitsutusohvri toomise ajal palvetas väljas suur hulk rahvast.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 Issanda ingel ilmus Sakariasele ja seisis suitsutusohvrialtari kõrval paremal pool.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 Kui Sakarias nägi inglit, oli ta rabatud ja hakkas kartma.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 Aga ingel ütles talle: „Ära karda, Sakarias! Sinu palvet on kuuldud ja su naine Eliisabet sünnitab sulle poja ja sa pead talle nimeks panema Johannes.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 Ta toob sulle rõõmu ja heameelt ning tema sünd rõõmustab paljusid.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 Ta saab suureks Issanda silmis. Ta ei joo veini ega muid alkohoolseid jooke. Teda täidab Püha Vaim juba enne sündimist.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 Ta pöörab paljud iisraellased tagasi Issanda, nende Jumala juurde.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 Ta läheb Issanda eel Eelija vaimus ja väes, et panna isad taas oma laste peale mõtlema, ning tuua need, kes on mässumeelsed, tagasi õige arusaamise juurde, et valmistada rahvas ette Issanda jaoks.“
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 „Kuidas ma saan selles kindel olla?“küsis Sakarias inglilt. „Ma olen vana mees ja ka mu naine on eakas.“
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 „Mina olen Gabriel, “vastas ingel. „Ma seisan Jumala juures ning mind saadeti sinuga rääkima ja sulle seda head uudist tooma.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 Aga kuna sa ei uskunud seda, mida ma sulle rääkisin, jääd sa tummaks ega saa kõneleda kuni määratud hetkeni, mil mu sõnad täide lähevad.“
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 Väljas ootas rahvas Sakariast ja imestas, miks tal templis nii kaua aega läheb.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 Kui ta lõpuks välja tuli, ei saanud ta nendega rääkida. Nad mõistsid, et ta oli templis näinud nägemust, sest kuigi ta suutis teha žeste, ei suutnud ta üldse rääkida.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 Pärast seda, kui ta oma teenistusaja oli lõpetanud, läks ta koju tagasi.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 Mõne aja pärast jäi tema naine Eliisabet lapseootele. Ta jäi koju viieks kuuks.
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 „Issand on seda mulle teinud, “ütles ta. „Nüüd on ta võtnud ära mu häbi teiste silmis.“
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 Eliisabeti lapseootuse kuuendal kuul saatis Jumal ingel Gabrieli noore neiu juurde, kelle nimi oli Maarja ja kes elas Galileas Naatsareti linnas.
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 Ta oli kihlatud Joosepi-nimelise mehega.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 Ingel tervitas teda. „Sul on eriline eesõigus, “ütles ta neiule. „Issand on sinuga.“
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 Maarja oli neist sõnadest hämmelduses ja juurdles, mida selline tervitus tähendab.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 „Ära karda, Maarja, “jätkas ingel, „sest Jumal on osutanud sinu suhtes armulikkust.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 Sa jääd lapseootele ja tood ilmale poja. Sa pead talle nimeks panema Jeesus.
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 Ta saab väga tähtsaks ja teda nimetatakse Kõigekõrgema Pojaks. Issand Jumal annab talle tema isa Taaveti trooni
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 ja ta valitseb igavesti Jaakobi järeltulijate üle. Tema kuningriik ei lõpe iial.“ (aiōn )
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn )
34 „Kuidas see võimalik on?“küsis Maarja. „Ma olen alles neitsi.“
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 Ingel vastas: „Püha Vaim tuleb sinu peale ja Kõigekõrgema vägi varjab sind. Laps, kes sünnib, on püha, ja teda hüütakse Jumala pojaks.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 Ja su sugulane Eliisabet on oma vanas eas samuti lapseootel. Naine, kelle kohta öeldi, et ta ei ole võimeline lapsi saama, on kuuendat kuud lapseootel.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 Jumala jaoks ei ole miski võimatu.“
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 „Siin ma olen, valmis olema Issanda teenija, “ütles Maarja. „Sündigu minuga just nii, nagu sa ütlesid.“Seejärel ingel lahkus tema juurest.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Veidi aja pärast pani Maarja end valmis ja kiirustas Juudamaa mägedesse, linna, kus oli
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 Sakariase maja. Sisse astudes hõikas ta Eliisabetti.
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 Kohe kui Eliisabet kuulis Maarja häält, hüppas laps tema ihus rõõmu pärast. Püha Vaim täitis Eliisabeti
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 ja ta hüüdis valju häälega: „Kui õnnistatud oled sina naiste hulgas ja kui õnnistatud on laps, kes sinust sünnib!
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 Miks mind nõnda austatakse, et mu Issanda ema mind külastab?
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 Kui ma kuulsin sind tervitust hüüdmas, hüppas laps mu ihus rõõmu pärast.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 Kui õnnelik sa oled, sest sa oled veendunud, et Issand teeb seda, mida ta sulle tõotas!“
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 Maarja vastas: „Kuidas ma ülistan Issandat!
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 Olen väga õnnelik Jumalas, mu Päästjas,
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 sest ta otsustas, et mina, tema teenija, olen oma tagasihoidlikust taustast hoolimata tema silmis väärtuslik. Nüüdsest peale ütlevad kõik põlvkonnad, et ma olen õnnistatud.
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 Kõigeväeline Jumal on teinud mulle suuri asju, tema nimi on püha.
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 Tema halastus kestab põlvest põlve nendele, kes teda austavad.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 Oma suure jõuga on ta lõhkunud tükkideks need, kes ülbelt ennast targaks peavad.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 Ta kisub mõjukad nende troonidelt maha ja ülendab need, kes on alandlikud.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 Ta annab näljastele häid asju süüa ja saadab rikkad tühje käsi minema.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 Ta on aidanud oma sulast Iisraeli ja pidanud teda halastuses meeles,
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 just nagu ta meie isadele, Aabrahamile ja tema järeltulijatele, igaveseks ajaks tõotas.“ (aiōn )
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn )
56 Maarja jäi Eliisabeti juurde kolmeks kuus ja naasis siis koju.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 Eliisabetil jõudis sünnitamise aeg kätte ja ta tõi ilmale poja.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 Naabrid ja sugulased kuulsid, kuidas Issand oli talle oma suurt headust osutanud, ning nad tähistasid seda koos temaga.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 Kaheksa päeva pärast tulid nad poissi ümber lõikama. Nad kavatsesid talle isa järgi nimeks panna Sakarias.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 „Ei, “ütles Eliisabet. „Tema nimeks peab saama Johannes.“
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 „Aga teie sugulaste hulgas pole kedagi, kellel see nimi oleks, “ütlesid nad talle.
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 Žestide abil küsisid nad Sakariaselt, poisi isalt, mis nime tahaks ta oma pojale panna.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 Sakarias andis märku, et talle antaks midagi, mille peale kirjutada. Kõigi üllatuseks kirjutas ta: „Tema nimi on Johannes.“
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 Kohe suutis ta jälle rääkida ja hakkas Jumalat ülistama.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 Kõiki läheduses elavaid inimesi täitis juhtunu tõttu aukartus ning kuuldus sellest levis kogu Juuda mägismaal.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 Igaüks, kes seda kuulis, mõtles, mida see peaks tähendama. „Kes sellest poisist saab?“küsisid nad, sest oli selge, et ta oli Jumala jaoks väga eriline.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 Tema isa Sakarias täitus Püha Vaimuga ja kuulutas prohvetlikult:
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 „Issand, Iisraeli Jumal, on imeline, sest ta on tulnud oma rahva juurde ja nad vabastanud.
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 Ta on andnud meile suure Päästja oma sulase Taaveti järglaste hulgast,
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 nagu ta tõotas ammu aega tagasi oma pühade prohvetite kaudu. (aiōn )
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn )
71 Ta tõotas päästa meid meie vaenlaste käest, nende käest, kes meid vihkavad.
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 Ta halastas meie isade peale ja pidas meeles oma püha lepingut −
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 tõotust, mille ta oli andnud meie isale Aabrahamile.
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 Ta vabastab meid hirmust ja päästab meid meie vaenlaste käest,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 et saaksime teda teenida ning teha kogu oma elu seda, mis on hea ja õige.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 Kuigi sa oled alles väike laps, hüütakse sind Kõigekõrgema prohvetiks, sest sa lähed Issanda eel valmistama talle teed ja
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 kuulutama tema rahvale teadmisi päästest pattude andestuse kaudu.
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 Tänu Jumala hoolitsevale headusele laseb taevas meile koiduvalgust paista,
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 et see säraks neile, kes elavad pimeduses ja surma varjus, ning juhiks meid rahu teel.“
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 Poiss Johannes kasvas ja sai vaimulikult tugevaks. Ta elas kõrbes, kuni jõudis kätte aeg avalikult Iisraeli teenida.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.