< Ilmutus 15 >

1 Siis ma nägin taevas veel üht suurt ja imelist tunnustähte: seitse inglit ja nende käes seitse viimset nuhtlust – sellega viidi lõpule Jumala raev.
Kisha nikaona ishara nyingine mbinguni, kubwa na ya kushangaza. Palikuwa hapo malaika saba wenye mabaa makubwa saba ya mwisho. Kwa mabaa hayo makubwa saba, ghadhabu ya Mungu imekamilishwa.
2 Ja ma nägin otsekui tulega segatud klaasmerd. Selle klaasmere ääres seisid Jumala kanneldega need, kes olid võitnud metsalise, tema kuju ja ta nime arvu.
Kisha nikaona kitu kama bahari ya kioo, imechanganywa na moto. Nikawaona pia wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake na ambaye jina lake lilitajwa kwa ile tarakimu. Watu hao walikuwa wamesimama kando ya hiyo bahari ya kioo, wakiwa na vinubi walivyopewa na Mungu.
3 Nad laulsid Jumala sulase Moosese laulu ja Talle laulu: „Suured ja imelised on sinu teod, Issand Jumal, Kõigeväeline! Õiged ja tõelised on sinu teed, rahvaste kuningas!“
Walikuwa wakiimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwanakondoo: “Bwana Mungu Mwenye Uwezo, matendo yako ni makuu mno! Ewe Mfalme wa mataifa, njia zako ni za haki na za kweli!
4 „Kes ei peaks kartma sind ning ülistama sinu nime, Issand? Sina üksi oled püha, kõik rahvad tulevad ning kummardavad sinu ees, sest sinu õiged kohtuotsused on saanud avalikuks.“
Bwana, ni nani asiyekucha wewe? Nani asiyelitukuza jina lako? Wewe peke yako ni Mtakatifu. Mataifa yote yatakujia na kukuabudu maana matendo yako ya haki yameonekana na wote.”
5 Pärast seda vaatasin ja nägin taevas templit – see tähendab lepinguseaduse telki – ja see avati.
Baada ya hayo nikaona Hekalu limefunguliwa mbinguni, na ndani yake hema ionyeshayo kuwapo kwa Mungu.
6 Templist väljusid seitse inglit seitsme nuhtlusega. Nende riided olid säravpuhtast linasest kangast ja rinna ümber olid kuldvööd.
Basi, wale malaika saba wenye mabaa saba wakatoka humo Hekaluni, wakiwa wamevaa nguo za kitani safi zenye kung'aa, na kanda za dhahabu vifuani mwao.
7 Ja üks neljast olevusest andis seitsmele inglile seitse kuldkaussi, täis selle Jumala raevu, kes elab igavesest ajast igavesti. (aiōn g165)
Kisha, mmojawapo wa vile viumbe vinne akawapa hao malaika saba mabakuli ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, aishiye milele na milele. (aiōn g165)
8 Ja tempel sai täis suitsu Jumala auhiilgusest ja tema väest ning ükski ei saanud minna templisse enne, kui seitsme ingli seitse nuhtlust olid lõpetatud.
Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya wale malaika saba.

< Ilmutus 15 >