< Psalmaro 80 >
1 Al la ĥorestro. Por ŝoŝanoj. Atesto de Asaf. Psalmo. Ho Paŝtisto de Izrael, aŭskultu; Vi, kiu kondukas Jozefon, kiel ŝafojn, Vi, kiu sidas sur keruboj, aperu!
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Antaŭ Efraim kaj Benjamen kaj Manase veku Vian forton, Kaj venu, por savi nin.
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Ho Dio, revenigu nin kaj lumigu Vian vizaĝon, Por ke ni estu savitaj.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Ho Eternulo, Dio Cebaot, Ĝis kiam Vi kolere repuŝos la preĝon de Via popolo?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Vi manĝigis al ili panon larman, Kaj Vi trinkigis al ili larmojn per granda mezuro.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Vi faris nin objekto de disputo por niaj najbaroj; Kaj niaj malamikoj nin mokas.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Ho Dio Cebaot! revenigu nin kaj lumigu Vian vizaĝon, Por ke ni estu savitaj.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Vinberbranĉon el Egiptujo Vi elportis, Vi forpelis popolojn kaj ĝin plantis;
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Vi purigis lokon por ĝi; Kaj ĝi profundigis siajn radikojn kaj plenigis la tutan landon;
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Montojn kovris ĝia ombro, Kaj ĝiaj branĉoj fariĝis kiel cedroj de Dio.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 Ĝi etendis siajn branĉojn ĝis la maro Kaj siajn branĉetojn ĝis la Rivero.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Kial Vi detruis ĝiajn barilojn, Ke ĉiuj pasantoj ĝin ŝiras?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 Subfosas ĝin arbara apro, Kaj kampa besto ĝin mordas.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Ho Dio Cebaot, returniĝu; Rigardu el la ĉielo kaj vidu, kaj rememoru tiun vinbertrunkon,
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 Kaj ŝirmu tion, kion plantis Via dekstra mano, Kaj la kreskaĵidon, kiun Vi fortikigis por Vi.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Ĝi estas bruligita de fajro, krevinta; De Via minaca vizaĝo ili pereis.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Via brako estu super la viro de Via dekstra mano, Super la homido, kiun Vi fortikigis por Vi.
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Kaj ni ne foriros de Vi; Vivigu nin, kaj ni vokos Vian nomon.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Ho Eternulo, Dio Cebaot! revenigu nin, lumigu Vian vizaĝon, Por ke ni estu savitaj.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.