< Psalmaro 66 >
1 Al la ĥorestro. Kanto-psalmo. Ĝoje kriu al Dio tuta la tero.
Kwa mwimbishaji. Wimbo. Zaburi. Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote!
2 Muziku la gloron de Lia nomo, Faru honoron al Lia gloro.
Imbeni utukufu wa jina lake; mpeni sifa zake kwa utukufu!
3 Diru al Dio: Kiel timindaj estas Viaj faroj! Pro Via granda forto kaŝiĝas antaŭ Vi Viaj malamikoj.
Mwambieni Mungu, “Jinsi gani yalivyo ya kutisha matendo yako! Uwezo wako ni mkuu mno kiasi kwamba adui wananyenyekea mbele zako.
4 La tuta tero kliniĝas antaŭ Vi kaj kantas al Vi, Kantas Vian nomon. (Sela)
Dunia yote yakusujudia, wanakuimbia wewe sifa, wanaliimbia sifa jina lako.”
5 Venu, kaj rigardu la farojn de Dio, Kiu estas timinda pro Siaj faroj inter la homidoj.
Njooni mwone yale Mungu aliyoyatenda, mambo ya kutisha aliyoyatenda miongoni mwa wanadamu!
6 Li faris el maro sekan teron; Riveron oni transpaŝis piede; Tie ni ĝojis pro Li.
Alifanya bahari kuwa nchi kavu, wakapita kati ya maji kwa miguu, njooni, tumshangilie.
7 Li regas per Sia potenco eterne; Liaj okuloj rigardas la popolojn; La ribelantoj ne leviĝu. (Sela)
Yeye hutawala kwa uwezo wake milele, macho yake huangalia mataifa yote: waasi wasithubutu kujiinua dhidi yake.
8 Laŭdu, ho popoloj, nian Dion, Kaj laŭte aŭdigu Lian gloron.
Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu, sauti ya sifa yake isikike,
9 Li donis vivon al nia animo, Kaj ne lasis falŝanceliĝi nian piedon.
ameyahifadhi maisha yetu na kuizuia miguu yetu kuteleza.
10 Ĉar Vi esploris nin, ho Dio; Vi refandis nin, kiel oni refandas arĝenton.
Ee Mungu, wewe ulitujaribu, ukatusafisha kama fedha.
11 Vi enirigis nin en kaptilon, Vi metis ŝarĝon sur niajn lumbojn;
Umetuingiza kwenye nyavu na umetubebesha mizigo mizito migongoni mwetu.
12 Vi rajdigis homojn sur niaj kapoj; Ni trapasis fajron kaj akvon, Sed Vi elirigis nin en bonstaton.
Uliwaruhusu watu watukalie vichwani, tulipita kwenye moto na kwenye maji, lakini ulituleta kwenye nchi iliyojaa utajiri tele.
13 Mi eniros en Vian domon kun bruloferoj; Mi plenumos al Vi miajn promesojn,
Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa na kukutimizia nadhiri zangu:
14 Kiujn eligis miaj lipoj kaj elparolis mia buŝo, Kiam mi estis en premo.
nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi na nilizotamka kwa kinywa changu nilipokuwa katika shida.
15 Grasajn bruloferojn mi alportos al Vi kun fumo de virŝafoj; Mi oferos bovidojn kaj kaprojn. (Sela)
Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono na sadaka za kondoo dume, nitakutolea mafahali na mbuzi.
16 Venu, aŭskultu, ĉiuj, kiuj timas Dion; Kaj mi rakontos, kion Li faris por mia animo.
Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu, nami niwaambie aliyonitendea.
17 Al Li mi vokis per mia buŝo, Kaj Lia glorado estis sub mia lango.
Nilimlilia kwa kinywa changu, sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu.
18 Se mi vidus maljustaĵon en mia koro, Mia Sinjoro min ne aŭskultus;
Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu, Bwana asingekuwa amenisikiliza;
19 Sed Dio aŭskultis, Li atentis la voĉon de mia preĝo.
lakini hakika Mungu amenisikiliza na amesikia sauti yangu katika maombi.
20 Glorata estu Dio, Kiu ne forpuŝis mian preĝon kaj ne rifuzis al mi Sian bonecon.
Sifa apewe Mungu, ambaye hakulikataa ombi langu wala kunizuilia upendo wake!