< Psalmaro 51 >
1 Al la ĥorestro. Psalmo de David, kiam venis al li la profeto Natan post lia aliĝo al Bat-Ŝeba. Korfavoru min, ho Dio, laŭ Via boneco; Laŭ Via granda kompatemeco elstreku miajn pekojn.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba. Ee Mungu, unihurumie, kwa kadiri ya upendo wako usiokoma, kwa kadiri ya huruma yako kuu, uyafute makosa yangu.
2 Lavu min tute pure de mia krimo, Kaj purigu min de mia peko.
Unioshe na uovu wangu wote na unitakase dhambi yangu.
3 Ĉar miajn kulpojn mi konsciadas; Kaj mia peko estas ĉiam antaŭ mi.
Kwa maana ninajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
4 Antaŭ Vi sola mi pekis, Kaj mi faris tion, kio estas malbona antaŭ Viaj okuloj; Tial Vi estas justa en Via vorto Kaj pura en Via juĝo.
Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi na kufanya yaliyo mabaya machoni pako, ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo, na kuwa na haki utoapo hukumu.
5 Mi estas ja naskita en krimo; Kaj en peko gravediĝis per mi mia patrino.
Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi, mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu.
6 Vi amas ja veron en la koro, Kaj en kaŝiteco Vi aperigas al mi saĝon.
Hakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni, ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima.
7 Senpekigu min per hisopo, kaj mi fariĝos pura; Lavu min, kaj mi estos pli blanka ol neĝo.
Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi, unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
8 Aŭdigu al mi ĝojon kaj gajecon, Kaj regajiĝos la ostoj, kiujn Vi batis.
Unipe kusikia furaha na shangwe, mifupa uliyoiponda na ifurahi.
9 Kaŝu Vian vizaĝon de miaj pekoj, Kaj ĉiujn miajn krimojn elstreku.
Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu, na uufute uovu wangu wote.
10 Koron puran kreu al mi, ho Dio, Kaj spiriton fidelan novigu en mi.
Ee Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.
11 Ne forpuŝu min de Via vizaĝo, Kaj Vian sanktan spiriton ne forprenu de mi.
Usinitupe kutoka mbele zako wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu.
12 Redonu al mi la ĝojon de Via helpo; Kaj spirito bonfara fortikigu min.
Unirudishie tena furaha ya wokovu wako, unipe roho ya utii, ili initegemeze.
13 Mi instruos al la krimuloj Vian vojon; Kaj pekuloj revenos al Vi.
Ndipo nitakapowafundisha wakosaji njia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
14 Liberigu min de sango, ho Dio, Dio de mia savo; Mia lango kantos Vian justecon.
Ee Mungu, Mungu uniokoaye, niokoe na hatia ya kumwaga damu, nao ulimi wangu utaimba juu ya haki yako.
15 Ho, mia Sinjoro, malfermu miajn lipojn; Kaj mia buŝo rakontos Vian gloron.
Ee Bwana, fungua midomo yangu, na kinywa changu kitatangaza sifa zako.
16 Ĉar Vi ne deziras oferdonon, alie mi ĝin donus; Brulofero ne plaĉas al Vi.
Wewe hupendezwi na dhabihu, au ningaliileta, hufurahii sadaka za kuteketezwa.
17 Oferdonoj al Dio estas spirito suferanta; Koron suferantan kaj humilan Vi, ho Dio, ne malŝatas.
Bali dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika, moyo uliovunjika wenye toba, Ee Mungu, hutaudharau.
18 Bonfaru al Cion laŭ Via favoro, Konstruu la murojn de Jerusalem;
Kwa wema wa radhi yako uifanye Sayuni istawi, ukazijenge upya kuta za Yerusalemu.
19 Tiam plaĉos al Vi oferdonoj de pieco, brulofero kaj plenofero; Tiam oni metos sur Vian altaron junajn bovojn.
Hapo ndipo kutakapokuwa na dhabihu za haki, sadaka nzima za kuteketezwa za kukupendeza sana, pia mafahali watatolewa madhabahuni mwako.