< Psalmaro 149 >

1 Haleluja! Kantu al la Eternulo novan kanton, Lian gloron en la anaro de fideluloj.
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2 Izrael ĝoju pri sia Kreinto, La filoj de Cion ĝoju pri sia Reĝo.
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3 Ili gloru Lian nomon en danco, Per tamburino kaj harpo ili muziku al Li.
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 Ĉar al la Eternulo plaĉas Lia popolo; Li ornamas humilulojn per savo.
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 La fideluloj ĝoju en honoro, Kantu ĝoje sur siaj kuŝejoj.
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6 Glorado al Dio estas en ilia buŝo, Kaj dutranĉa glavo en ilia mano,
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 Por fari venĝon super la popoloj, Punkorektadon super la gentoj;
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8 Por malliberigi iliajn reĝojn per ĉenoj Kaj iliajn eminentulojn per feraj katenoj;
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 Por fari super ili antaŭdestinitan juĝon. Tio estas honoro por ĉiuj Liaj fideluloj. Haleluja!
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.

< Psalmaro 149 >