< Psalmaro 120 >
1 Kanto de suprenirado. Al la Eternulo mi vokis en mia sufero, Kaj Li aŭskultis min.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Ho Eternulo, savu mian animon de mensoga parolo, De falsa lango.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 Kion Li donos al vi, Kaj kion Li alportos al vi, ho falsa lango?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Akrajn sagojn de fortulo Kun karboj genistaj.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Ve al mi, ke mi gastas en Meŝeĥ, Ke mi loĝas inter la tendoj de Kedar!
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 Tro longe loĝis mia animo Inter malamantoj de paco.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Mi estas pacema; Sed kiam mi ekparolas, ili komencas militon.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.