< Psalmaro 116 >

1 Mi amas, ke la Eternulo aŭdas mian voĉon Kaj mian petegon,
Ninampenda Bwana kwa maana amesikia sauti yangu; amesikia kilio changu ili anihurumie.
2 Ke Li klinis Sian orelon al mi; Kaj en miaj tagoj mi Lin vokos.
Kwa sababu amenitegea sikio lake, nitamwita siku zote za maisha yangu.
3 Ĉirkaŭis min la ondoj de la morto, Kaj turmentoj de Ŝeol min trafis; Suferon kaj ĉagrenon mi trovis. (Sheol h7585)
Kamba za mauti zilinizunguka, maumivu makuu ya kuzimu yalinipata, nikalemewa na taabu na huzuni. (Sheol h7585)
4 Sed la nomon de la Eternulo mi vokis: Ho Eternulo, savu mian animon.
Ndipo nikaliitia jina la Bwana: “Ee Bwana, niokoe!”
5 Favorkora estas la Eternulo kaj justa, Kaj nia Dio estas kompatema.
Bwana ni mwenye neema na haki, Mungu wetu ni mwingi wa huruma.
6 La Eternulo gardas la simplanimulojn; Mi estis en mizero, kaj Li min savis.
Bwana huwalinda wanyenyekevu, nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
7 Revenu, ho mia animo, al via trankvileco, Ĉar la Eternulo faris al vi bonon.
Ee nafsi yangu, tulia tena, kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
8 Ĉar Vi savis mian animon de la morto, Miajn okulojn de larmoj, Miajn piedojn de falpuŝiĝo.
Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umeniokoa nafsi yangu na mauti, macho yangu kutokana na machozi, miguu yangu kutokana na kujikwaa,
9 Mi irados antaŭ la Eternulo En la lando de la vivo.
ili niweze kutembea mbele za Bwana, katika nchi ya walio hai.
10 Kun kredo mi diris: Mi estas tre afliktita.
Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”
11 Mi diris en mia konfuziĝo: Ĉu homo mensogas.
Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”
12 Kion mi redonu al la Eternulo Por ĉiuj Liaj bonfaroj al mi?
Nimrudishie Bwana nini kwa wema wake wote alionitendea?
13 Mi levos la pokalon de savo, Kaj mi vokos la nomon de la Eternulo.
Nitakiinua kikombe cha wokovu na kulitangaza jina la Bwana.
14 Miajn promesojn al la Eternulo mi plenumos Antaŭ Lia tuta popolo.
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote.
15 Grandvalora en la okuloj de la Eternulo Estas la morto de Liaj fideluloj.
Kifo cha watakatifu kina thamani machoni pa Bwana.
16 Ho Eternulo, mi ja estas Via sklavo, Mi estas Via sklavo, filo de Via sklavino; Vi disigis miajn ligilojn.
Ee Bwana, hakika mimi ni mtumishi wako, mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umeniweka huru toka katika minyororo yangu.
17 Al Vi mi oferdonos dankan oferon, Kaj la nomon de la Eternulo mi vokos.
Nitakutolea dhabihu ya kukushukuru na kuliita jina la Bwana.
18 Miajn promesojn al la Eternulo mi plenumos Antaŭ Lia tuta popolo,
Nitazitimiza nadhiri zangu kwa Bwana mbele za watu wake wote,
19 En la kortoj de la domo de la Eternulo, Interne de vi, ho Jerusalem.
katika nyua za nyumba ya Bwana, katikati yako, ee Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalmaro 116 >