< Sentencoj 24 >
1 Ne sekvu malbonajn homojn, Kaj ne deziru esti kun ili;
Usiwe na husuda kwa wenye ubaya, wala usitamani kuambatana nao,
2 Ĉar ilia koro pensas pri perfortaĵo, Kaj ilia buŝo parolas malbonaĵon.
kwa sababu mioyo yao inapanga njama za vurugu na midomo ya huongea juu ya madhara.
3 Per saĝo konstruiĝas domo, Kaj per prudento ĝi fortikiĝas;
Kwa hekima nyumba hujengwa na kwa ufahamu huimarishwa.
4 Kaj per sciado la ĉambroj pleniĝas Per ĉia havo grandvalora kaj agrabla.
Kwa maarifa vyumba hujazwa vitu vyote vya thamani na utajiri wa kupendeza.
5 Homo saĝa havas forton, Kaj homo prudenta estas potenca.
Shujaa wa hekima ni imara, na mtu wa maarifa huongeza nguvu zake;
6 Kun pripenso faru militon; Kaj venko venas per multe da konsilantoj.
maana kwa uongozi wa busara unaweza kufanya vita na kwa washauri wengi kuna ushindi.
7 Tro alta estas la saĝo por malsaĝulo; Ĉe la pordego li ne malfermos sian buŝon.
Hekima ipo juu sana kwa mpumbavu; hafumbui kinywa chake kwenye mlango.
8 Kiu intencas fari malbonon, Tiun oni nomas maliculo.
Kuna yule mwenye kupanga kufanya mabaya- watu wanamwita bwana wa njama.
9 Malico de malsaĝulo estas peko; Kaj blasfemanto estas abomenaĵo por homo.
Mipango ya mpumbavu ni dhambi na watu humchukia mwenye dhihaka.
10 Se vi montriĝis malforta en tago de mizero, Via forto estas ja malgranda.
Kama utakuwa dhaifu na mwenye kuogopa siku ya taabu, basi nguvu zako ni haba.
11 Savu tiujn, kiujn oni prenis por mortigi, Kaj ne fortiriĝu de tiuj, kiuj estas kondamnitaj al morto.
Waokoe wanaochukuliwa kwenda kwenye mauti na uwashikilie wale wanaopepesuka kwenda kwa mchinjaji.
12 Se vi diras: Ni tion ne sciis, La esploranto de koroj ja komprenas, Kaj la gardanto de via animo ja scias, Kaj Li redonas al homo laŭ liaj faroj.
Kama utasema, “Tazama, hatujui chochote juu ya hili,” je yule anayepima mioyo hajui unachosema? Na yule anayelinda maisha yako, je hajui? Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?
13 Manĝu, mia filo, mielon, ĉar ĝi estas bona; Kaj la mieltavolo estas dolĉa por via gorĝo;
Mwanangu, kula asali kwa kuwa ni nzuri, kwa sababu matone ya sega la asali ni matamu unapoonja.
14 Tia estas por via animo la sciado de saĝo, se vi ĝin trovis, Kaj ekzistas estonteco, kaj via espero ne pereos.
Hekima ndiyo ilivyo katika nafsi yako - kama utaitafuta, tumaini lako halitabatilika na kutakuwa na tumaini.
15 Ne insidu, ho malvirtulo, kontraŭ la domo de virtulo; Ne ataku lian ripozejon;
Usisubiri kwa kuvizia kama waovu ambao hushambulia nyumba ya mwenye haki. Usiiharibu nyumba yake!
16 Ĉar sep fojojn virtulo falos, kaj tamen leviĝos; Sed malvirtuloj implikiĝas en la malfeliĉo.
Maana mwenye haki huanguka mara saba na kuinuka tena, lakini waovu huangushwa kwa maafa.
17 Kiam falas via malamiko, ne ĝoju, Kaj ĉe lia malfeliĉo via koro ne plezuriĝu;
Usisherekee wakati adui yako anapoanguka na wala moyo wako usifurahi anapojikwaa,
18 Ĉar eble la Eternulo vidos, kaj tio ne plaĉos al Li, Kaj Li returnos de li Sian koleron.
au Yehova ataona na kutoridhika na kuondoa ghadhabu juu yake.
19 Ne koleru kontraŭ malbonfarantoj, Kaj ne enviu la malvirtulojn;
Usifadhaike kwa sababu ya watenda mabaya, na wala usiwahusudu watu waovu,
20 Ĉar la malbonulo ne havos estontecon; La lumilo de malvirtuloj estingiĝos.
maana mtu mbaya hana matumaini na taa ya watu waovu itazimika.
21 Timu, mia filo, la Eternulon kaj la reĝon; Kun ribeluloj ne komunikiĝu.
Mwanangu; mche Yehova, na umwogope mfalme, usishirikiane na watu wenye kuasi dhidi yao,
22 Ĉar subite venos ilia pereo; Kaj kiu scias, kiam venos la puno de ambaŭ?
maana kwa ghafula msiba wao utakuja na ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu utakao kuja kutoka kwa hao wote?
23 Ankaŭ ĉi tio estas vortoj de saĝuloj: Konsideri personojn ĉe juĝado estas ne bone.
Haya ni maneno ya wenye busara pia. Upendeleo katika kuhukumu kesi kwa sheria si vizuri.
24 Kiu diras al malvirtulo: Vi estas virtulo, Tiun malbenos popoloj, tiun malamos gentoj.
Anayemwambia mwenye hatia, “Wewe upo sawa,” atalaaniwa na watu na mataifa yatamchukia.
25 Sed kiuj faras riproĉojn, tiuj plaĉas, Kaj sur ilin venos bona beno.
Bali wenye kuwakemea waovu watakuwa na furaha na zawadi za wema zitakuja kwao.
26 Kiu respondas ĝustajn vortojn, Tiu kisas per la lipoj.
Anayetoa jibu la kweli hutoa busu kwenye midomo.
27 Plenumu vian laboron ekstere, Pretigu ĉion sur via kampo; Kaj poste aranĝu vian domon.
Andaa kazi yako ya nje, na tayarisha kila kitu kwa ajili yako mwenyewe shambani; baada ya hapo, jenga nyumba yako.
28 Ne atestu sen kaŭzo kontraŭ via proksimulo; Ĉu vi trompus per via buŝo?
Usitoe ushahidi dhidi ya jirani yako bila sababu na usidanganye kwa midomo yako.
29 Ne diru: Kiel li agis kontraŭ mi, tiel mi agos kontraŭ li; Mi redonos al la homo laŭ lia faro.
Usiseme, “Mimi nitamtendea kile alichonitendea; nitalipiza kwa kile alichofanya.”
30 Mi pasis tra kampo de homo maldiligenta Kaj tra vinberĝardeno de sensaĝulo;
Nilikwenda jirani na shamba la mtu mvivu, nikapita kwenye shamba la mzabibu la mtu asiye na akili.
31 Kaj jen ĉie elkreskis urtiko, Ĉio estas kovrita de dornoj, Kaj la ŝtona muro estas detruita.
Miiba imeota kila sehemu, ardhi ilikuwa imefunikwa kwa upupu, na ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Kaj kiam mi vidis, mi prenis ĝin en mian koron, Mi rigardis, kaj ricevis instruon:
Kisha nikaliona na kufikiria juu yake; nikatazama na kupokea mafundisho.
33 Iom da dormo, iom da dormeto, Iom da kunmeto de la manoj por kuŝado;
Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kupumzika kwa kukunja mikono kidogo-
34 Kaj venos via malriĉeco kiel rabisto, Kaj via senhaveco kiel viro armita.
na umasikini huja kwa kutembea juu yako, na mahitaji yako kama askari mwenye silaha.