< Sentencoj 12 >

1 Kiu amas instruon, tiu amas scion; Sed kiu malamas atentigon, tiu estas malsaĝulo.
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 Bonulo akiras favoron de la Eternulo; Sed homo malica estos kondamnita.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 Ne fortikiĝos homo per malvirto; Sed la radiko de virtuloj ne ŝanceliĝos.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 Brava virino estas krono por sia edzo; Sed senhonora estas kiel puso en liaj ostoj.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 La pensoj de virtuloj estas justeco; La meditado de malvirtuloj estas malico.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 La paroloj de malvirtuloj estas insido pri sango; Sed la buŝo de virtuloj ilin savas.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 La malvirtuloj renversiĝos kaj malaperos; Sed la domo de virtuloj staros forte.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 Oni laŭdas homon laŭ lia saĝo; Sed perversulo estos hontigita.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Pli bona estas homo negrava, sed laboranta por si, Ol homo, kiu serĉas honoron, sed al kiu mankas pano.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 Virtulo kompatas la vivon de sia bruto; Sed la koro de malvirtuloj estas kruela.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 Kiu prilaboras sian teron, tiu havos sate da pano; Sed kiu serĉas vantaĵojn, tiu estas malsaĝulo.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 Malvirtulo serĉas subtenon de malnobluloj; Sed la radiko de virtuloj donas forton.
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 Per siaj pekaj vortoj kaptiĝas malbonulo; Sed virtulo eliras el mizero.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 Per la fruktoj de sia buŝo homo bone satiĝas; Kaj laŭ la merito de siaj manoj homo ricevas redonon.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 La vojo de malsaĝulo estas ĝusta en liaj okuloj; Sed saĝulo aŭskultas konsilon.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 Malsaĝulo tuj montras sian koleron; Sed saĝulo ignoras ofendon.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 Kiu estas verama, tiu eldiras tion, kio estas ĝusta, Sed falsama atestulo trompon.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 Ofte nepripensita parolo vundas kiel glavo; Sed la lango de saĝuloj sanigas.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 Parolo vera restas fortike por ĉiam; Sed parolo malvera nur por momento.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 Malico estas en la koro de malbonintenculoj; Sed ĉe la pacigantoj estas ĝojo.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 Nenio malbona trafos virtulon; Sed la malvirtuloj havas plene da malbono.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 Abomenaĵo por la Eternulo estas buŝo mensogema; Sed kiuj agas laŭ vero, tiuj plaĉas al Li.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 Saĝa homo kaŝas scion; Sed la koro de malsaĝuloj elkrias malsaĝecon.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 La mano de diligentuloj regos; Sed mano maldiligenta pagos tributon.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 Zorgo en la koro de homo ĝin premas; Sed amika vorto ĝin ĝojigas.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 Al la virtulo estas pli bone, ol al lia proksimulo; Sed la vojo de malvirtuloj ilin erarigas.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 Maldiligenteco ne pretigos al si manĝon; Sed homo diligenta havas riĉecon.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 Sur la vojo de virto estas vivo, Kaj ĝi estos ebenigita kontraŭ morto.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.

< Sentencoj 12 >