< Sentencoj 10 >
1 Sentencoj de Salomono. Saĝa filo estas ĝojo por sia patro, Kaj filo malsaĝa estas malĝojo por sia patrino.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Maljustaj trezoroj ne donas utilon; Sed bonfaremo savas de morto.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 La Eternulo ne malsatigos animon de piulo; Sed la avidon de malpiulo Li forpuŝas.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 Maldiligenta mano malriĉigas; Sed mano de diligentuloj riĉigas.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 Kiu kolektas dum la somero, tiu estas filo saĝa; Sed kiu dormas en la tempo de rikolto, tiu estas filo hontinda.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 Beno estas sur la kapo de piulo; Sed la buŝo de malpiulo kaŝas krimon.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 La memoro de piulo estas benata; Sed la nomo de malpiuloj forputros.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 Kiu havas saĝan koron, tiu akceptos moralordonojn; Sed kiu havas malsaĝan buŝon, tiu renversiĝos.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 Kiu iras en senkulpeco, tiu iras sendanĝere; Sed kiu kurbigas siajn vojojn, tiu estos punita.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 Kiu grimacas per la okulo, tiu kaŭzas suferon; Kaj kiu havas malsaĝan buŝon, tiu renversiĝos.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 La buŝo de piulo estas fonto de vivo; Sed la buŝo de malpiulo kaŝas krimon.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 Malamo kaŭzas malpacon; Sed amo kovras ĉiujn pekojn.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 Sur la lipoj de prudentulo troviĝas saĝo; Sed vergo apartenas al la dorso de sensaĝulo.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Saĝuloj konservas la scion; Sed la buŝo de malsaĝulo estas proksima al la pereo.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 La havo de riĉulo estas lia fortika urbo; Sed pereo por la malriĉuloj estas ilia malriĉo.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 La laborpago de piulo estas por la vivo; La enspezoj de malpiulo estas por peko.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 Kiu konservas la instruon, tiu iras al vivo; Sed kiu forĵetas atentigon, tiu restas en eraro.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 Kiu kaŝas malamon, tiu havas falseman buŝon; Kaj kiu elirigas kalumnion, tiu estas malsaĝulo.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 Ĉe multo da vortoj ne evitebla estas peko; Sed kiu retenas siajn lipojn, tiu estas saĝa.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 La lango de piulo estas plej bonspeca arĝento; La koro de malpiuloj estas kiel nenio.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 La lipoj de piulo gvidas multajn; Sed malsaĝuloj mortas pro manko de saĝo.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 La beno de la Eternulo riĉigas, Kaj malĝojon Li ne aldonas al ĝi.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 Por malsaĝulo estas ĝojo fari malbonon; Kaj saĝo, por saĝulo.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 Kio timigas malpiulon, tio trafos lin; Kaj kion deziras piuloj, tio estos donita al ili.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Kiel pasanta ventego, tiel malpiulo rapide malaperas; Sed piulo havas eternan fundamenton.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Kiel la vinagro por la dentoj kaj la fumo por la okuloj, Tiel la maldiligentulo estas por tiuj, kiuj lin sendis.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 La timo antaŭ la Eternulo multigas la tagojn; Sed la jaroj de malpiuloj estos mallongigitaj.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 La atendo de piuloj fariĝos ĝojo; Sed la espero de malpiuloj pereos.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 La vojo de la Eternulo estas defendo por la senpekulo, Sed pereo por la malbonfarantoj.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 Piulo neniam falpuŝiĝos; Sed la malpiuloj ne restos sur la tero.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 La buŝo de piulo eligas saĝon; Sed lango falsema estos ekstermita.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 La lipoj de piulo anoncas favoraĵon, Kaj la buŝo de malpiuloj malicaĵon.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.