< Titus 1 >
1 Paul, a servant of God, and an apostle of Jesus Christ, according to the faith of the choice ones of God, and an acknowledging of truth that [is] according to piety,
Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu na kuijua kweli iletayo utauwa:
2 upon hope of life age-during, which God, who doth not lie, did promise before times of ages, (aiōnios )
imani na ujuzi ulioko katika tumaini la uzima wa milele, ambao Mungu, asiyesema uongo, aliahidi hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, (aiōnios )
3 (and He manifested in proper times His word, ) in preaching, which I was entrusted with, according to a charge of God our Saviour,
naye kwa wakati wake aliouweka alilidhihirisha neno lake kwa njia ya mahubiri ambayo mimi nimewekewa amana kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu:
4 to Titus — true child according to a common faith: Grace, kindness, peace, from God the Father, and the Lord Jesus Christ our Saviour!
Kwa Tito, mwanangu hasa katika imani tunayoshiriki sote: Neema iwe kwako na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Mwokozi wetu.
5 For this cause left I thee in Crete, that the things lacking thou mayest arrange, and mayest set down in every city elders, as I did appoint to thee;
Sababu ya mimi kukuacha huko Krete ni ili uweke utaratibu mambo yale yaliyosalia na kuwaweka wazee wa kanisa katika kila mji, kama nilivyokuagiza.
6 if any one is blameless, of one wife a husband, having children stedfast, not under accusation of riotous living or insubordinate —
Mzee wa kanisa asiwe na lawama, awe mume wa mke mmoja, mtu ambaye watoto wake ni waaminio na wala hawashtakiwi kwa ufisadi.
7 for it behoveth the overseer to be blameless, as God's steward, not self-pleased, nor irascible, not given to wine, not a striker, not given to filthy lucre;
Kwa kuwa mwangalizi, kama wakili wa Mungu, imempasa kuwa mtu asiye na lawama, asiwe mwenye majivuno au mwepesi wa hasira, wala mlevi, wala asiwe mtu mwenye tamaa ya mapato yasiyo ya halali.
8 but a lover of strangers, a lover of good men, sober-minded, righteous, kind, self-controlled,
Bali awe mkarimu, anayependa mema, mwenye kiasi, mwenye haki, mwadilifu, mnyofu, mtakatifu na mwenye kuitawala nafsi yake.
9 holding — according to the teaching — to the stedfast word, that he may be able also to exhort in the sound teaching, and the gainsayers to convict;
Inampasa alishike kwa uthabiti lile neno la imani kama lilivyofundishwa, kusudi aweze kuwaonya wengine kwa mafundisho manyofu na kuwakanusha wale wanaopingana nayo.
10 for there are many both insubordinate, vain-talkers, and mind-deceivers — especially they of the circumcision —
Kwa maana wako wengi wasiotii, wenye maneno yasiyo na maana, hasa wale wa kikundi cha tohara.
11 whose mouth it behoveth to stop, who whole households do overturn, teaching what things it behoveth not, for filthy lucre's sake.
Hao ni lazima wanyamazishwe, kwa sababu wanaharibu watu wa nyumba nzima wakifundisha mambo yasiyowapasa kufundisha. Wanafanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mapato ya udanganyifu.
12 A certain one of them, a prophet of their own, said — 'Cretans! always liars, evil beasts, lazy bellies!'
Hata mmojawapo wa manabii wao mwenyewe amesema, “Wakrete ni waongo siku zote, wanyama wabaya, walafi, wavivu.”
13 this testimony is true; for which cause convict them sharply, that they may be sound in the faith,
Ushuhuda huu ni kweli. Kwa hiyo, uwakemee kwa ukali wapate kuwa wazima katika imani,
14 not giving heed to Jewish fables and commands of men, turning themselves away from the truth;
ili wasiendelee kuangalia hadithi za Kiyahudi au maagizo ya wale watu wanaoikataa kweli.
15 all things, indeed, [are] pure to the pure, and to the defiled and unstedfast [is] nothing pure, but of them defiled [are] even the mind and the conscience;
Kwa wale walio safi, kila kitu ni safi kwao. Lakini kwa wale waliopotoka na wasioamini, hakuna chochote kilicho safi. Kwa kweli nia zao na dhamiri zao zimepotoka.
16 God they profess to know, and in the works they deny [Him], being abominable, and disobedient, and unto every good work disapproved.
Wanadai kumjua Mungu, lakini kwa matendo yao wanamkana. Hao watu ni chukizo, wasiotii, wasiofaa kwa jambo lolote jema.