< Ruth 4 >
1 And Boaz hath gone up to the gate, and sitteth there, and lo, the redeemer is passing by of whom Boaz had spoken, and he saith, 'Turn aside, sit down here, such a one, such a one;' and he turneth aside and sitteth down.
Boazi akakwea mpaka kwenye lango la mji, akaketi pale. Yule mtu wa jamaa aliyekuwa wa karibu wa kukomboa, ambaye Boazi alimtaja, akaja. Boazi akasema, “Njoo hapa, rafiki yangu. Karibu uketi.” Naye akakaribia, akaketi.
2 And he taketh ten men of the elders of the city, and saith, 'Sit down here;' and they sit down.
Boazi akatwaa watu kumi miongoni mwa wazee wa mji, akawaambia, “Ketini hapa.” Nao wakaketi.
3 And he saith to the redeemer, 'A portion of the field which [is] to our brother, to Elimelech, hath Naomi sold, who hath come back from the fields of Moab;
Kisha akamwambia yule jamaa wa karibu wa kukomboa, “Naomi, aliyerudi hapa kutoka nchi ya Moabu, anauza sehemu ya ardhi iliyokuwa mali ya ndugu yetu Elimeleki.
4 and I said, I uncover thine ear, saying, Buy before the inhabitants, and before the elders of my people; if thou dost redeem — redeem, and if none doth redeem — declare to me, and I know, for there is none save thee to redeem, and I after thee.' And he saith, I redeem [it].'
Nami niliwaza nikujulishe wewe na kukuambia uinunue mbele ya hawa waliopo hapa, na mbele ya wazee wa watu wangu. Kama wewe utaikomboa, haya fanya hivyo. Lakini kama hutaikomboa, uniambie, ili nijue. Kwa kuwa hakuna mtu mwingine mwenye haki ya kuikomboa ila wewe na baada yako ni mimi.” Naye akasema, “Nitaikomboa mimi.”
5 And Boaz saith, 'In the day of thy buying the field from the hand of Naomi, then from Ruth the Moabitess, wife of the dead, thou hast bought [it], to raise up the name of the dead over his inheritance.'
Ndipo Boazi akasema “Siku utakaponunua hiyo ardhi kutoka kwa Naomi na Ruthu, Mmoabu, itakubidi kumchukua pia huyo mjane, ili kudumisha jina la marehemu pamoja na mali yake.”
6 And the redeemer saith, 'I am not able to redeem [it] for myself, lest I destroy mine inheritance; redeem for thyself — thou — my right of redemption, for I am not able to redeem.'
Aliposikia hili, yule jamaa wa karibu wa kukomboa akasema, “Basi mimi sitaweza kuikomboa, kwa sababu inaonekana nitauhatarisha urithi wangu. Wewe ikomboe mwenyewe. Mimi sitaweza.”
7 And this [is] formerly in Israel for redemption and for changing, to establish anything: a man hath drawn off his sandal, and given [it] to his neighbour, and this [is] the testimony in Israel.
(Basi katika siku za kale huko Israeli, ili kukamilisha tendo la kukomboa na kukabidhiana mali, mmoja huvua kiatu chake na kumpatia mwingine. Hii ilikuwa ni njia ya kuhalalisha mabadilishano katika Israeli.)
8 And the redeemer saith to Boaz, 'Buy [it] for thyself,' and draweth off his sandal.
Basi yule jamaa wa karibu wa kukomboa akamwambia Boazi, “Wewe inunue mwenyewe.” Naye huyo jamaa akavua kiatu chake.
9 And Boaz saith to the elders, and [to] all the people, 'Witnesses [are] ye to-day that I have bought all that [is] to Elimelech, and all that [is] to Chilion and Mahlon, from the hand of Naomi;
Kisha Boazi akawatangazia wazee na watu wote waliokuwepo, “Leo ninyi ni mashahidi kwamba mimi nimenunua kutoka kwa Naomi yote yaliyokuwa mali ya Elimeleki, Kilioni na Maloni.
10 and also Ruth the Moabitess, wife of Mahlon, I have bought to myself for a wife, to raise up the name of the dead over his inheritance; and the name of the dead is not cut off from among his brethren, and from the gate of his place; witnesses ye [are] to-day.'
Nimemchukua pia Ruthu, Mmoabu, mjane wa Maloni, awe mke wangu, ili kuendeleza jina la marehemu pamoja na mali zake, ili jina lake marehemu lisitoweke miongoni mwa jamaa yake, wala katika kumbukumbu za mji wake. Leo hivi ninyi ni mashahidi!”
11 And all the people who [are] in the gate say — also the elders — 'Witnesses! Jehovah make the woman who is coming in unto thy house as Rachel and as Leah, both of whom built the house of Israel; and do thou virtuously in Ephrathah, and proclaim the Name in Beth-Lehem;
Kisha wazee pamoja na watu wote waliokuwa langoni wakasema, “Sisi ni mashahidi. Bwana na amfanye mwanamke huyu aingiaye nyumbani mwako kuwa kama Raheli na kama Lea, wale wanawake wawili ambao pamoja waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe ufanikiwe katika Efrathi na uwe mashuhuri katika Bethlehemu.
12 and let thy house be as the house of Pharez (whom Tamar bare to Judah), of the seed which Jehovah doth give to thee of this young woman.'
Kupitia kwa watoto ambao Bwana atakupa kutokana na huyu mwanamwali, jamaa yako na ifanane na ya Peresi, ambaye Tamari alimzalia Yuda.”
13 And Boaz taketh Ruth, and she becometh his wife, and he goeth in unto her, and Jehovah giveth to her conception, and she beareth a son.
Basi Boazi akamwoa Ruthu, naye akawa mke wake. Alipoingia kwake, Bwana akamjalia Ruthu, naye akapata mimba, akamzaa mtoto wa kiume.
14 And the women say unto Naomi, 'Blessed [is] Jehovah who hath not let a redeemer cease to thee to-day, and his name is proclaimed in Israel,
Wanawake wakamwambia Naomi: “Ahimidiwe Bwana, asiyekuacha bila kuwa na jamaa wa karibu wa kukomboa. Na awe mashuhuri katika Israeli yote!
15 and he hath been to thee for a restorer of life, and for a nourisher of thine old age, for thy daughter-in-law who hath loved thee — who is better to thee than seven sons — hath borne him.'
Atakurejeshea uhai wako na kukuangalia katika siku za uzee wako. Kwa maana mkweo ambaye anakupenda, na ambaye kwako ni bora zaidi ya watoto wa kiume saba, ndiye alimzaa.”
16 And Naomi taketh the lad, and layeth him in her bosom, and is to him for a nurse;
Basi Naomi akamchukua yule mtoto, akampakata na akawa mlezi wake.
17 and the neighbouring women give to him a name, saying, 'There hath been a son born to Naomi,' and they call his name Obed; he [is] father of Jesse, father of David.
Wanawake waliokuwa jirani zake wakasema, “Naomi ana mtoto wa kiume.” Wakamwita jina lake Obedi. Yeye ndiye baba yake Yese, aliye baba yake Daudi.
18 And these are genealogies of Pharez: Pharez begat Hezron,
Hivi ndivyo vizazi vya Peresi: Peresi alimzaa Hesroni,
19 and Hezron begat Ram, and Ram begat Amminidab,
Hesroni akamzaa Ramu, Ramu akamzaa Aminadabu,
20 and Amminidab begat Nahshon, and Nahshon begat Salmon,
Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,
21 and Salmon begat Boaz, and Boaz begat Obed,
Salmoni akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obedi,
22 and Obed begat Jesse, and Jesse begat David.
Obedi akamzaa Yese, na Yese akamzaa Daudi.