< Revelation 14 >

1 And I saw, and lo, a Lamb having stood upon the mount Sion, and with him an hundred forty-four thousands, having the name of his Father written upon their foreheads;
Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao.
2 and I heard a voice out of the heaven, as a voice of many waters, and as a voice of great thunder, and a voice I heard of harpers harping with their harps,
Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao.
3 and they sing, as it were, a new song before the throne, and before the four living creatures, and the elders, and no one was able to learn the song except the hundred forty-four thousands, who have been bought from the earth;
Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani.
4 these are they who with women were not defiled, for they are virgin; these are they who are following the Lamb whithersoever he may go; these were bought from among men — a first-fruit to God and to the Lamb —
Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
5 and in their mouth there was not found guile, for unblemished are they before the throne of God.
Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.
6 And I saw another messenger flying in mid-heaven, having good news age-during to proclaim to those dwelling upon the earth, and to every nation, and tribe, and tongue, and people, (aiōnios g166)
Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios g166)
7 saying in a great voice, 'Fear ye God, and give to Him glory, because come did the hour of His judgment, and bow ye before Him who did make the heaven, and the land, and sea, and fountains of waters.'
Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”
8 And another messenger did follow, saying, 'Fall, fall, did Babylon, the great city, because of the wine of the wrath of her whoredom she hath given to all nations to drink.'
Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”
9 And a third messenger did follow them, saying in a great voice, 'If any one the beast doth bow before, and his image, and doth receive a mark upon his forehead, or upon his hand,
Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake,
10 he also shall drink of the wine of the wrath of God, that hath been mingled unmixed in the cup of His anger, and he shall be tormented in fire and brimstone before the holy messengers, and before the Lamb,
yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo.
11 and the smoke of their torment doth go up to ages of ages; and they have no rest day and night, who are bowing before the beast and his image, also if any doth receive the mark of his name. (aiōn g165)
Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn g165)
12 Here is endurance of the saints: here [are] those keeping the commands of God, and the faith of Jesus.'
Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.
13 And I heard a voice out of the heaven saying to me, 'Write: Happy are the dead who in the Lord are dying from this time!' 'Yes, (saith the Spirit, ) That they may rest from their labours — and their works do follow them!'
Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”
14 And I saw, and lo, a white cloud, and upon the cloud [one] sitting like to a son of man, having upon his head a golden crown, and in his hand a sharp sickle;
Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake.
15 and another messenger did come forth out of the sanctuary crying in a great voice to him who is sitting upon the cloud, 'Send forth thy sickle and reap, because come to thee hath the hour of reaping, because ripe hath been the harvest of the earth;'
Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.”
16 and he who is sitting upon the cloud did put forth his sickle upon the earth, and the earth was reaped.
Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
17 And another messenger did come forth out of the sanctuary that [is] in the heaven, having — he also — a sharp sickle,
Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
18 and another messenger did come forth out from the altar, having authority over the fire, and he called with a great cry to him having the sharp sickle, saying, 'Send forth thy sharp sickle, and gather the clusters of the vine of the earth, because come to perfection have her grapes;'
Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”
19 and the messenger did put forth his sickle to the earth, and did gather the vine of the earth, and did cast [it] to the great wine-press of the wrath of God;
Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
20 and trodden was the wine-press outside of the city, and blood did come forth out of the wine-press — unto the bridles of the horses, a thousand, six hundred furlongs.
Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.

< Revelation 14 >