< Psalms 83 >
1 A Song, — A Psalm of Asaph. O God, let there be no silence to Thee, Be not silent, nor be quiet, O God.
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 For, lo, Thine enemies do roar, And those hating Thee have lifted up the head,
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 Against Thy people they take crafty counsel, And consult against Thy hidden ones.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 They have said, 'Come, And we cut them off from [being] a nation, And the name of Israel is not remembered any more.'
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 For they consulted in heart together, Against Thee a covenant they make,
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 Tents of Edom, and Ishmaelites, Moab, and the Hagarenes,
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal, and Ammon, and Amalek, Philistia with inhabitants of Tyre,
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 Asshur also is joined with them, They have been an arm to sons of Lot. (Selah)
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Do to them as [to] Midian, As [to] Sisera, as [to] Jabin, at the stream Kishon.
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 They were destroyed at Endor, They were dung for the ground!
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Make their nobles as Oreb and as Zeeb, And as Zebah and Zalmunna all their princes,
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 Who have said, 'Let us occupy for ourselves The comely places of God.'
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 O my God, make them as a rolling thing, As stubble before wind.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 As a fire doth burn a forest, And as a flame setteth hills on fire,
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 So dost Thou pursue them with Thy whirlwind, And with Thy hurricane troublest them.
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Fill their faces [with] shame, And they seek Thy name, O Jehovah.
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 They are ashamed and troubled for ever, Yea, they are confounded and lost.
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 And they know that Thou — (Thy name [is] Jehovah — by Thyself, ) [Art] the Most High over all the earth!
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.