< Psalms 81 >
1 To the Overseer. — 'On the Gittith.' By Asaph. Cry aloud to God our strength, Shout to the God of Jacob.
Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
2 Lift up a song, and give out a timbrel, A pleasant harp with psaltery.
Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
3 Blow in the month a trumpet, In the new moon, at the day of our festival,
Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
4 For a statute to Israel it [is], An ordinance of the God of Jacob.
Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
5 A testimony on Joseph He hath placed it, In his going forth over the land of Egypt. A lip, I have not known — I hear.
Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
6 From the burden his shoulder I turned aside, His hands from the basket pass over.
“Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
7 In distress thou hast called and I deliver thee, I answer thee in the secret place of thunder, I try thee by the waters of Meribah. (Selah)
Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
8 Hear, O My people, and I testify to thee, O Israel, if thou dost hearken to me:
Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
9 There is not in thee a strange god, And thou bowest not thyself to a strange god.
Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
10 I [am] Jehovah thy God, Who bringeth thee up out of the land of Egypt. Enlarge thy mouth, and I fill it.
Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
11 But, My people hearkened not to My voice, And Israel hath not consented to Me.
Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
12 And I send them away in the enmity of their heart, They walk in their own counsels.
Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
13 O that My people were hearkening to Me, Israel in My ways would walk.
Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
14 As a little thing their enemies I cause to bow, And against their adversaries I turn back My hand,
Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
15 Those hating Jehovah feign obedience to Him, But their time is — to the age.
Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
16 He causeth him to eat of the fat of wheat, And [with] honey from a rock I satisfy thee!
Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”