< Psalms 78 >
1 An Instruction of Asaph. Give ear, O my people, to my law, Incline your ear to sayings of my mouth.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 I open with a simile my mouth, I bring forth hidden things of old,
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 That we have heard and do know, And our fathers have recounted to us.
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 We do not hide from their sons, To a later generation recounting praises of Jehovah, And His strength, and His wonders that He hath done.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 And He raiseth up a testimony in Jacob, And a law hath placed in Israel, That He commanded our fathers, To make them known to their sons.
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 So that a later generation doth know, Sons who are born, do rise and recount to their sons,
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 And place in God their confidence, And forget not the doings of God, But keep His commands.
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 And they are not like their fathers, A generation apostate and rebellious, A generation! it hath not prepared its heart, Nor stedfast with God [is] its spirit.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 Sons of Ephraim — armed bearers of bow, Have turned in a day of conflict.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 They have not kept the covenant of God, And in His law they have refused to walk,
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 And they forget His doings, And His wonders that He shewed them.
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Before their fathers He hath done wonders, In the land of Egypt — the field of Zoan.
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 He cleft a sea, and causeth them to pass over, Yea, He causeth waters to stand as a heap.
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 And leadeth them with a cloud by day, And all the night with a light of fire.
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 He cleaveth rocks in a wilderness, And giveth drink — as the great deep.
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 And bringeth out streams from a rock, And causeth waters to come down as rivers.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 And they add still to sin against Him, To provoke the Most High in the dry place.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 And they try God in their heart, To ask food for their lust.
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 And they speak against God — they said: 'Is God able to array a table in a wilderness?'
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Lo, He hath smitten a rock, And waters flow, yea, streams overflow. 'Also — bread [is] He able to give? Doth He prepare flesh for His people?'
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Therefore hath Jehovah heard, And He sheweth Himself wroth, And fire hath been kindled against Jacob, And anger also hath gone up against Israel,
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 For they have not believed in God, Nor have they trusted in His salvation.
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 And He commandeth clouds from above, Yea, doors of the heavens He hath opened.
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 And He raineth on them manna to eat, Yea, corn of heaven He hath given to them.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Food of the mighty hath each eaten, Venison He sent to them to satiety.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 He causeth an east wind to journey in the heavens, And leadeth by His strength a south wind,
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 And He raineth on them flesh as dust, And as sand of the seas — winged fowl,
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 And causeth [it] to fall in the midst of His camp, Round about His tabernacles.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 And they eat, and are greatly satisfied, And their desire He bringeth to them.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 They have not been estranged from their desire, Yet [is] their food in their mouth,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 And the anger of God hath gone up against them, And He slayeth among their fat ones, And youths of Israel He caused to bend.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 With all this they have sinned again, And have not believed in His wonders.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 And He consumeth in vanity their days, And their years in trouble.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 If He slew them, then they sought Him, And turned back, and sought God earnestly,
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 And they remember that God [is] their rock, And God Most High their redeemer.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 And — they deceive Him with their mouth, And with their tongue do lie to Him,
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 And their heart hath not been right with Him, And they have not been stedfast in His covenant.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 And He — the Merciful One, Pardoneth iniquity, and destroyeth not, And hath often turned back His anger, And waketh not up all His fury.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 And He remembereth that they [are] flesh, A wind going on — and it returneth not.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 How often do they provoke Him in the wilderness, Grieve Him in the desolate place?
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Yea, they turn back, and try God, And the Holy One of Israel have limited.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 They have not remembered His hand The day He ransomed them from the adversary.
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 When He set His signs in Egypt, And His wonders in the field of Zoan,
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 And He turneth to blood their streams, And their floods they drink not.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 He sendeth among them the beetle, and it consumeth them, And the frog, and it destroyeth them,
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 And giveth to the caterpillar their increase, And their labour to the locust.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 He destroyeth with hail their vine, And their sycamores with frost,
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 And delivereth up to the hail their beasts, And their cattle to the burning flames.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 He sendeth on them the fury of His anger, Wrath, and indignation, and distress — A discharge of evil messengers.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 He pondereth a path for His anger, He kept not back their soul from death, Yea, their life to the pestilence He delivered up.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 And He smiteth every first-born in Egypt, The first-fruit of the strong in tents of Ham.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 And causeth His people to journey as a flock, And guideth them as a drove in a wilderness,
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 And He leadeth them confidently, And they have not been afraid, And their enemies hath the sea covered.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 And He bringeth them in unto the border of His sanctuary, This mountain His right hand had got,
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 And casteth out nations from before them, And causeth them to fall in the line of inheritance, And causeth the tribes of Israel to dwell in their tents,
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 And they tempt and provoke God Most High, And His testimonies have not kept.
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 And they turn back, And deal treacherously like their fathers, They have been turned like a deceitful bow,
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 And make Him angry with their high places, And with their graven images make Him zealous,
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 God hath heard, and sheweth Himself wroth. And kicketh exceedingly against Israel.
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 And He leaveth the tabernacle of Shiloh, The tent He had placed among men,
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 And He giveth His strength to captivity, And His beauty into the hand of an adversary,
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 And delivereth up to the sword His people, And with His inheritance shewed Himself angry.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 His young men hath fire consumed, And His virgins have not been praised.
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 His priests by the sword have fallen, And their widows weep not.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 And the Lord waketh as a sleeper, As a mighty one crying aloud from wine.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 And He smiteth His adversaries backward, A reproach age-during He hath put on them,
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 And He kicketh against the tent of Joseph, And on the tribe of Ephraim hath not fixed.
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 And He chooseth the tribe of Judah, With mount Zion that He loved,
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 And buildeth His sanctuary as a high place, Like the earth, He founded it to the age.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 And He fixeth on David His servant, And taketh him from the folds of a flock,
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 From behind suckling ones He hath brought him in, To rule over Jacob His people, And over Israel His inheritance.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 And he ruleth them according to the integrity of his heart, And by the skilfulness of his hands leadeth them!
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.