< Psalms 68 >
1 To the Overseer. — A Psalm, a song of David. Rise doth God — scattered are His enemies! And those hating Him flee from His face.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
2 As the driving away of smoke Thou drivest away, As the melting of wax before fire, The wicked perish at the presence of God.
Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
3 And the righteous rejoice, they exult before God, And they joy with gladness.
Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
4 Sing ye to God — praise His name, Raise up a highway for Him who is riding in deserts, In Jah [is] His name, and exult before Him.
Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
5 Father of the fatherless, and judge of the widows, [Is] God in His holy habitation.
Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
6 God — causing the lonely to dwell at home, Bringing out bound ones into prosperity, Only — the refractory have inhabited a dry place.
Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
7 O God, in Thy going forth before Thy people, In Thy stepping through the wilderness, (Selah)
Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
8 The earth hath shaken, Yea, the heavens have dropped before God, This Sinai — before God, the God of Israel.
dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
9 A shower of free-will gifts thou shakest out, O God. Thine inheritance, when it hath been weary, Thou hast established it.
Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
10 Thy company have dwelt in it, Thou preparest in Thy goodness for the poor, O God.
Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
11 The Lord doth give the saying, The female proclaimers [are] a numerous host.
Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
12 Kings of hosts flee utterly away, And a female inhabitant of the house apportioneth spoil.
“Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
13 Though ye do lie between two boundaries, Wings of a dove covered with silver, And her pinions with yellow gold.
Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
14 When the Mighty spreadeth kings in it, It doth snow in Salmon.
Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
15 A hill of God [is] the hill of Bashan, A hill of heights [is] the hill of Bashan.
Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
16 Why do ye envy, O high hills, The hill God hath desired for His seat? Jehovah also doth tabernacle for ever.
Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
17 The chariots of God [are] myriads, thousands of changes, The Lord [is] among them, in Sinai, in the sanctuary.
Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
18 Thou hast ascended on high, Thou hast taken captive captivity, Thou hast taken gifts for men, That even the refractory may rest, O Jah God.
Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
19 Blessed [is] the Lord, day by day He layeth on us. God Himself [is] our salvation. (Selah)
Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
20 God Himself [is] to us a God for deliverances, And Jehovah Lord hath the outgoings of death.
Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
21 Only — God doth smite The head of His enemies, The hairy crown of a habitual walker in his guilt.
Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
22 The Lord said: 'From Bashan I bring back, I bring back from the depths of the sea.
Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23 So that thou dashest thy foot in blood, [In the blood of] enemies — the tongue of Thy dogs.'
ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
24 They have seen Thy goings, O God, Goings of my God, my king, in the sanctuary.
Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
25 Singers have been before, Behind [are] players on instruments, In the midst virgins playing with timbrels.
Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
26 In assemblies bless ye God, The Lord — from the fountain of Israel.
Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
27 There [is] little Benjamin their ruler, Heads of Judah their defence, Heads of Zebulun — heads of Naphtali.
Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
28 Thy God hath commanded thy strength, Be strong, O God, this Thou hast wrought for us.
Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
29 Because of Thy temple at Jerusalem, To Thee do kings bring a present.
Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
30 Rebuke a beast of the reeds, a company of bulls, With calves of the peoples, Each humbling himself with pieces of silver, Scatter Thou peoples delighting in conflicts.
Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
31 Come do fat ones out of Egypt, Cush causeth her hands to run to God.
Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
32 Kingdoms of the earth, sing ye to God, Praise ye the Lord. (Selah)
Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
33 To him who is riding on the heavens of the heavens of old, Lo, He giveth with His voice a strong voice.
mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
34 Ascribe ye strength to God, Over Israel [is] His excellency, and His strength in the clouds.
Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
35 Fearful, O God, out of Thy sanctuaries, The God of Israel Himself, Giving strength and might to the people. Blessed [is] God!
Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!