< Psalms 5 >
1 To the Overseer, 'Concerning the Inheritances.' — A Psalm of David. My sayings hear, O Jehovah, Consider my (meditation)
Sikiliza nikuitapo, Yahweh; tazama kuugua kwangu.
2 Be attentive to the voice of my cry, My king and my God, For unto Thee I pray habitually.
Sikiliza sauti yangu nikuitapo, Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa kuwa ni kwako Bwana naomba.
3 Jehovah, [at] morning Thou hearest my voice, [At] morning I set in array for Thee, And I look out.
Yahweh; sikia kilio changu asubuhi; na asubuhi nitaleta dua yangu kwako na kungoja kwa matarajio.
4 For not a God desiring wickedness [art] Thou, Evil inhabiteth Thee not.
Hakika wewe ni Mungu usiye kubaliana na uovu; watu waovu hawawezi kuwa wageni wako.
5 The boastful station not themselves before Thine eyes: Thou hast hated all working iniquity.
Wenye kiburi hawata simama katika uwepo wako; wewe unawachukia wote wanaofanya maovu.
6 Thou destroyest those speaking lies, A man of blood and deceit Jehovah doth abominate.
Nawe utawaharibu waongo; Yahweh huwadharau vurugu na watu wadanganyifu.
7 And I, in the abundance of Thy kindness, I enter Thy house, I bow myself toward Thy holy temple in Thy fear.
Lakini kwangu mimi, kwa sababu ya ukuu na uaminifu wa agano lako, nitakuja nyumbani mwako; na kwa heshima nitakuinamia mbele ya hekalu lako takatifu.
8 O Jehovah, lead me in Thy righteousness, Because of those observing me, Make straight before me Thy way,
Oh Bwana, uniongoze katika haki yako kwa sababu ya adui zangu; usawazishe njia yako mbele yangu.
9 For there is no stability in their mouth. Their heart [is] mischiefs, An open grave [is] their throat, Their tongue they make smooth.
Kwa kuwa midomoni mwao hamna ukweli; utu wao wa ndani ni mwovu; makoo yao ni kaburi lililo wazi; husifu kinafiki kwa ulimi wao.
10 Declare them guilty, O God, Let them fall from their own counsels, In the abundance of their transgressions Drive them away, Because they have rebelled against Thee.
Mungu, wafanye kuwa na hatia; mipango yao iwe kuanguka kwao! Kwa ajili ya makosa yao mengi uwatoe nje, kwa kuwa wamekuasi wewe.
11 And rejoice do all trusting in Thee, To the age they sing, and Thou coverest them over, And those loving Thy name exult in Thee.
Bali wale wanao kukimbilia wafurahi; uwafanye wapige kelele kwa shangwe siku zote kwa sababu unawapigania; uwafanye wenye furaha ndani yako, wale walipendao jina lako.
12 For Thou blessest the righteous, O Jehovah, As a buckler with favour dost compass him!
Kwa maana utawabariki wenye haki, Yahweh; utawazunguka kwa neema kama ngao.