< Psalms 27 >

1 By David. Jehovah [is] my light and my salvation, Whom do I fear? Jehovah [is] the strength of my life, Of whom am I afraid?
Yahwe ni nuru yangu na wokovu wangu; nimuogope nani? Yahwe ni salama ya maisha yangu; ni mhofu nani?
2 When evil doers come near to me to eat my flesh, My adversaries and mine enemies to me, They have stumbled and fallen.
Wakati waovu waliponijia kunila mwili wangu, wapinzani wangu na adui zangu walijikwaa na wakaanguka.
3 Though a host doth encamp against me, My heart doth not fear, Though war riseth up against me, In this I [am] confident.
Ingawa jeshi hujipanga kupigana na mimi, moyo wangu hautaogopa; japo vita vijapo inuka kupigana nami hata hapo nitabaki kuwa jasiri.
4 One [thing] I asked of Jehovah — it I seek. My dwelling in the house of Jehovah, All the days of my life, To look on the pleasantness of Jehovah, And to inquire in His temple.
Kitu kimoja nimekiomba kwa Yahwe, nami nitakitafuta hicho: kwamba niweze kukaa katika nyumba ya Yahwe siku zote za maisha yangu, kuutazama uzuri wa Yahwe na kutafakari hekaruni mwake.
5 For He hideth me in a tabernacle in the day of evil, He hideth me in a secret place of His tent, On a rock he raiseth me up.
Kwa kuwa katika siku ya shida atanificha nyumbani mwake; atanificha katika mfuniko wa hema lake. Yeye ataniinua juu ya mwamba!
6 And now, lifted up is my head, Above my enemies — my surrounders, And I sacrifice in His tent sacrifices of shouting, I sing, yea, I sing praise to Jehovah.
Kisha kichwa changu kitainuliwa juu ya maadui wote wanizungukao, nami nitatoa sadaka ya furaha hemani mwake! Nitaimba na kutunga nyimbo kwa Yahwe!
7 Hear, O Jehovah, my voice — I call, And favour me, and answer me.
Sikia, sauti yangu nikuitapo, Yahwe! Unihurumie, na unijibu!
8 To Thee said my heart 'They sought my face, Thy face, O Jehovah, I seek.'
Moyo wangu huongea kuhusu wewe, “Utafute uso wake!” Nami nautafuta uso wako, Yahwe!
9 Hide not Thy face from me, Turn not aside in anger Thy servant, My help Thou hast been. Leave me not, nor forsake me, O God of my salvation.
Usiufiche uso wako mbali na mimi; usinikasirikie mimi mtumishi wako! Wewe umekuwa msaada wangu; usiniache wala kunitelekeza, Mungu wa wokovu wangu!
10 When my father and my mother Have forsaken me, then doth Jehovah gather me.
Hata kama baba yangu na mama yangu wakiniacha, Yahwe utanitunza kwako.
11 Shew me, O Jehovah, Thy way, And lead me in a path of uprightness, For the sake of my beholders.
Unifundishe njia yako, Yahwe! Kwa sababu ya adui zangu uniongoze katika njia salama.
12 Give me not to the will of my adversaries, For risen against me have false witnesses, And they breathe out violence to me.
Usiwaache adui zangu wanifanyie watamanivyo, kwa sababu mashahidi wa uongo wameinuka kinyume namimi, nao wanapumua vurugu!
13 I had not believed to look on the goodness of Jehovah In the land of the living!
Kitu gani kingeweza kunitokea kama nisingeamini kuwa nitauona uzuri wa Yahwe katika nchi ya walio hai?
14 Look unto Jehovah — be strong, And He doth strengthen thy heart, Yea, look unto Jehovah!
Umngoje Yahwe; uwe imara, na moyo wako uwe jasiri! Umngoje Yahwe!

< Psalms 27 >