< Psalms 130 >

1 A Song of the Ascents. From depths I have called Thee, Jehovah.
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Lord, hearken to my voice, Thine ears are attentive to the voice of my supplications.
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 If iniquities Thou dost observe, O Lord, who doth stand?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 But with Thee [is] forgiveness, that Thou mayest be feared.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 I hoped [for] Jehovah — hoped hath my soul, And for His word I have waited.
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 My soul [is] for the Lord, More than those watching for morning, Watching for morning!
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Israel doth wait on Jehovah, For with Jehovah [is] kindness, And abundant with Him [is] redemption.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 And He doth redeem Israel from all his iniquities!
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

< Psalms 130 >