< Psalms 128 >
1 A Song of the Ascents. O the happiness of every one fearing Jehovah, Who is walking in His ways.
Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
2 The labour of thy hands thou surely eatest, Happy [art] thou, and good [is] to thee.
Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 Thy wife [is] as a fruitful vine in the sides of thy house, Thy sons as olive plants around thy table.
Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
4 Lo, surely thus is the man blessed who is fearing Jehovah.
Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
5 Jehovah doth bless thee out of Zion, Look, then, on the good of Jerusalem, All the days of thy life,
Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6 And see the sons of thy sons! Peace on Israel!
nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.