< Psalms 114 >
1 In the going out of Israel from Egypt, The house of Jacob from a strange people,
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Judah became His sanctuary, Israel his dominion.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 The sea hath seen, and fleeth, The Jordan turneth backward.
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 The mountains have skipped as rams, Heights as sons of a flock.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 What — to thee, O sea, that thou fleest? O Jordan, thou turnest back!
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 O mountains, ye skip as rams! O heights, as sons of a flock!
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 From before the Lord be afraid, O earth, From before the God of Jacob,
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 He is turning the rock to a pool of waters, The flint to a fountain of waters!
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.