< Obadiah 1 >
1 Thus said the Lord Jehovah to Edom, A report we have heard from Jehovah, And an ambassador among nations was sent, 'Rise, yea, let us rise against her for battle.'
Maono ya Obadia. Hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi kuhusu Edomu: Tumesikia ujumbe kutoka kwa Bwana: Mjumbe alitumwa kwa mataifa kusema, “Inukeni, twendeni tukapigane vita dhidi yake.”
2 Lo, little I have made thee among nations, Despised [art] thou exceedingly.
“Angalieni, nitawafanya wadogo miongoni mwa mataifa, mtadharauliwa kabisa.
3 The pride of thy heart hath lifted thee up, O dweller in clifts of a rock, (A high place [is] his habitation, He is saying in his heart, 'Who doth bring me down [to] earth?')
Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba na kufanya makao yako juu, wewe unayejiambia mwenyewe, ‘Ni nani awezaye kunishusha chini?’
4 If thou dost go up high as an eagle, And if between stars thou dost set thy nest, From thence I bring thee down, An affirmation of Jehovah.
Ingawa unapaa juu kama tai na kufanya kiota chako kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko,” asema Bwana.
5 If thieves have come in to thee, If spoilers of the night, How hast thou been cut off! Do they not steal their sufficiency? If gatherers have come in to thee, Do they not leave gleanings?
“Ikiwa wevi wangekuja kwako, ikiwa wanyangʼanyi wangekujia usiku: Lo! Tazama ni maafa kiasi gani yangekuwa yanakungojea: je, si wangeiba tu kiasi ambacho wangehitaji? Kama wachuma zabibu wangekuja kwako, je, wasingebakiza zabibu chache?
6 How hath Esau been searched out! Flowed out have his hidden things,
Lakini tazama jinsi Esau atakavyotekwa, jinsi hazina zake zilizofichwa zitatekwa nyara!
7 Unto the border sent thee have all thine allies, Forgotten thee, prevailed over thee, have thy friends, Thy bread they make a snare under thee, There is no understanding in him!
Wote ulioungana nao watakufukuza hadi mpakani, rafiki zako watakudanganya na kukushinda, wale wanaokula mkate wako watakutegea mtego, lakini hutaweza kuugundua.
8 Is it not in that day — an affirmation of Jehovah, That I have destroyed the wise out of Edom, And understanding out of the mount of Esau?
“Katika siku hiyo,” asema Bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau?
9 And broken down have been thy mighty ones, O Teman, So that every one of the mount of Esau is cut off.
Ee Temani, mashujaa wako watatiwa hofu, kila mmoja katika milima ya Esau ataangushwa chini kwa kuchinjwa.
10 For slaughter, for violence [to] thy brother Jacob, Cover thee doth shame, And thou hast been cut off — to the age.
Kwa sababu ya jeuri uliyofanya dhidi ya ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika; utaangamizwa milele.
11 In the day of thy standing over-against, In the day of strangers taking captive his force, And foreigners have entered his gates, And for Jerusalem have cast a lot, Even thou [art] as one of them!
Siku ile ulisimama mbali ukiangalia wakati wageni walipojichukulia utajiri wake na watu wa nchi nyingine walipoingia malango yake wakipiga kura kwa ajili ya Yerusalemu, ulikuwa kama mmoja wao.
12 And — thou dost not look on the day of thy brother, On the day of his alienation, Nor dost thou rejoice over sons of Judah, In the day of their destruction, Nor make great thy mouth in a day of distress.
Usingemdharau ndugu yako katika siku ya msiba wake, wala kufurahia juu ya watu wa Yuda katika siku ya maangamizi yao, wala kujigamba sana katika siku ya taabu yao.
13 Nor come into a gate of My people in a day of their calamity, Nor look, even thou, on its misfortune in a day of its calamity, Nor send forth against its force in a day of its calamity,
Usingeingia katika malango ya watu wangu katika siku ya maafa yao, wala kuwadharau katika janga lao katika siku ya maafa yao, wala kunyangʼanya mali zao katika siku ya maafa yao.
14 Nor stand by the breach to cut off its escaped, Nor deliver up its remnant in a day of distress.
Usingengoja kwenye njia panda na kuwaua wakimbizi wao, wala kuwatoa watu wake waliosalia katika siku ya shida yao.
15 For near [is] the day of Jehovah, on all the nations, As thou hast done, it is done to thee, Thy deed doth turn back on thine own head.
“Siku ya Bwana iko karibu kwa mataifa yote. Kama ulivyofanya, nawe utafanyiwa vivyo hivyo, matendo yako yatakurudia juu ya kichwa chako.
16 For — as ye have drunk on My holy mount, Drink do all the nations continually, And they have drunk and have swallowed, And they have been as they have not been.
Kama vile ulivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, vivyo hivyo mataifa yote watakunywa mfululizo, watakunywa na kunywa, nao watatoweka kana kwamba hawajawahi kuwepo.
17 And in mount Zion there is an escape, And it hath been holy, And the house of Jacob have possessed their possessions.
Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwepo na wale watakaookoka; nao utakuwa mtakatifu, nayo nyumba ya Yakobo itamiliki urithi wake.
18 And the house of Jacob hath been a fire, And the house of Joseph a flame, And the house of Esau for stubble, And they have burned among them, And they have consumed them, And there is not a remnant to the house of Esau, For Jehovah hath spoken.
Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto; nayo nyumba ya Esau itakuwa bua kavu, nao wataiwasha moto na kuiteketeza. Hakutakuwa na watakaosalimika kutoka nyumba ya Esau.” Bwana amesema.
19 And they have possessed the south with the mount of Esau, And the low country with the Philistines, And they have possessed the field of Ephraim, And the field of Samaria, And Benjamin with Gilead.
Watu kutoka nchi ya Negebu wataikalia milima ya Esau, na watu kutoka miteremko ya vilima watamiliki nchi ya Wafilisti. Watayakalia mashamba ya Efraimu na Samaria, naye Benyamini atamiliki Gileadi.
20 And the removed of this force of the sons of Israel, That [is with] the Canaanites unto Zarephat, And the removed of Jerusalem that [is] with the Sepharad, Possess the cities of the south.
Kundi la Waisraeli walioko uhamishoni Kanaani watarudi na kumiliki nchi mpaka Sarepta. Walioko uhamishoni Sefaradi kutoka Yerusalemu watamiliki miji ya Negebu.
21 And gone up have saviours on mount Zion, To judge the mount of Esau, And the kingdom hath been to Jehovah!'
Waokoaji watakwea juu ya Mlima Sayuni kutawala milima ya Esau. Nao ufalme utakuwa wa Bwana.