< Numbers 27 >

1 And daughters of Zelophehad son of Hepher, son of Gilead, son of Machir, son of Manasseh, of the families of Manasseh son of Joseph, draw near — and these [are] the names of his daughters, Mahlah, Noah, and Hoglah, and Milcah, and Tirzah —
Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
2 and stand before Moses, and before Eleazar the priest, and before the princes, and all the company, at the opening of the tent of meeting, saying:
ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
3 'Our father died in the wilderness, and he — he was not in the midst of the company who were met together against Jehovah in the company of Korah, but for his own sin he died, and had no sons;
“Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
4 why is the name of our father withdrawn from the midst of his family because he hath no son? give to us a possession in the midst of the brethren of our father;'
Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
5 and Moses bringeth near their cause before Jehovah.
Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
6 And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
naye Bwana akamwambia Mose,
7 'Rightly are the daughters of Zelophehad speaking; thou dost certainly give to them a possession of an inheritance in the midst of their father's brethren, and hast caused to pass over the inheritance of their father to them.
“Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
8 'And unto the sons of Israel thou dost speak, saying, When a man dieth, and hath no son, then ye have caused his inheritance to pass over to his daughter;
“Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
9 and if he have no daughter, then ye have given his inheritance to his brethren;
Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
10 and if he have no brethren, then ye have given his inheritance to his father's brethren;
Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
11 and if his father have no brethren, then ye have given his inheritance to his relation who is near unto him of his family, and he hath possessed it;' and it hath been to the sons of Israel for a statute of judgment, as Jehovah hath commanded Moses.
Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
12 And Jehovah saith unto Moses, 'Go up unto this mount Abarim, and see the land which I have given to the sons of Israel;
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
13 and thou hast seen it, and thou hast been gathered unto thy people, also thou, as Aaron thy brother hath been gathered,
Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
14 because ye provoked My mouth in the wilderness of Zin, in the strife of the company — to sanctify Me at the waters before their eyes;' they [are] waters of Meribah, in Kadesh, in the wilderness of Zin.
kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
15 And Moses speaketh unto Jehovah, saying,
Mose akamwambia Bwana,
16 'Jehovah — God of the spirits of all flesh — appoint a man over the company,
“Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
17 who goeth out before them, and who cometh in before them, and who taketh them out, and who bringeth them in, and the company of Jehovah is not as sheep which have no shepherd.'
ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
18 And Jehovah saith unto Moses, 'Take to thee Joshua son of Nun, a man in whom [is] the Spirit, and thou hast laid thine hand upon him,
Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
19 and hast caused him to stand before Eleazar the priest, and before all the company, and hast charged him before their eyes,
Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
20 and hast put of thine honour upon him, so that all the company of the sons of Israel do hearken.
Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
21 'And before Eleazar the priest he standeth, and he hath asked for him by the judgment of the Lights before Jehovah; at His word they go out, and at His word they come in; he, and all the sons of Israel with him, even all the company.'
Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
22 And Moses doth as Jehovah hath commanded him, and taketh Joshua, and causeth him to stand before Eleazar the priest, and before all the company,
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
23 and layeth his hands upon him, and chargeth him, as Jehovah hath spoken by the hand of Moses.
Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.

< Numbers 27 >