< Luke 1 >
1 Seeing that many did take in hand to set in order a narration of the matters that have been fully assured among us,
Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.
2 as they did deliver to us, who from the beginning became eye-witnesses, and officers of the Word, —
Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.
3 it seemed good also to me, having followed from the first after all things exactly, to write to thee in order, most noble Theophilus,
Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,
4 that thou mayest know the certainty of the things wherein thou wast instructed.
ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, the king of Judea, a certain priest, by name Zacharias, of the course of Abijah, and his wife of the daughters of Aaron, and her name Elisabeth;
Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.
6 and they were both righteous before God, going on in all the commands and righteousnesses of the Lord blameless,
Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.
7 and they had no child, because that Elisabeth was barren, and both were advanced in their days.
Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 And it came to pass, in his acting as priest, in the order of his course before God,
Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,
9 according to the custom of the priesthood, his lot was to make perfume, having gone into the sanctuary of the Lord,
Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.
10 and all the multitude of the people were praying without, at the hour of the perfume.
Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.
11 And there appeared to him a messenger of the Lord standing on the right side of the altar of the perfume,
Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.
12 and Zacharias, having seen, was troubled, and fear fell on him;
Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
13 and the messenger said unto him, 'Fear not, Zacharias, for thy supplication was heard, and thy wife Elisabeth shall bear a son to thee, and thou shalt call his name John,
Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.
14 and there shall be joy to thee, and gladness, and many at his birth shall joy,
Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 for he shall be great before the Lord, and wine and strong drink he may not drink, and of the Holy Spirit he shall be full, even from his mother's womb;
Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 and many of the sons of Israel he shall turn to the Lord their God,
Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.
17 and he shall go before Him, in the spirit and power of Elijah, to turn hearts of fathers unto children, and disobedient ones to the wisdom of righteous ones, to make ready for the Lord, a people prepared.'
Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”
18 And Zacharias said unto the messenger, 'Whereby shall I know this? for I am aged, and my wife is advanced in her days?'
Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”
19 And the messenger answering said to him, 'I am Gabriel, who have been standing near before God, and I was sent to speak unto thee, and to proclaim these good news to thee,
Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.
20 and lo, thou shalt be silent, and not able to speak, till the day that these things shall come to pass, because thou didst not believe my words, that shall be fulfilled in their season.'
Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”
21 And the people were waiting for Zacharias, and wondering at his tarrying in the sanctuary,
Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.
22 and having come out, he was not able to speak to them, and they perceived that a vision he had seen in the sanctuary, and he was beckoning to them, and did remain dumb.
Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.
23 And it came to pass, when the days of his service were fulfilled, he went away to his house,
Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.
24 and after those days, his wife Elisabeth conceived, and hid herself five months, saying —
Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:
25 'Thus hath the Lord done to me, in days in which He looked upon [me], to take away my reproach among men.'
“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”
26 And in the sixth month was the messenger Gabriel sent by God, to a city of Galilee, the name of which [is] Nazareth,
Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,
27 to a virgin, betrothed to a man, whose name [is] Joseph, of the house of David, and the name of the virgin [is] Mary.
kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.
28 And the messenger having come in unto her, said, 'Hail, favoured one, the Lord [is] with thee; blessed [art] thou among women;'
Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”
29 and she, having seen, was troubled at his word, and was reasoning of what kind this salutation may be.
Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30 And the messenger said to her, 'Fear not, Mary, for thou hast found favour with God;
Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31 and lo, thou shalt conceive in the womb, and shalt bring forth a son, and call his name Jesus;
Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.
32 he shall be great, and Son of the Highest he shall be called, and the Lord God shall give him the throne of David his father,
Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.
33 and he shall reign over the house of Jacob to the ages; and of his reign there shall be no end.' (aiōn )
Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
34 And Mary said unto the messenger, 'How shall this be, seeing a husband I do not know?'
Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”
35 And the messenger answering said to her, 'The Holy Spirit shall come upon thee, and the power of the Highest shall overshadow thee, therefore also the holy-begotten thing shall be called Son of God;
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.
36 and lo, Elisabeth, thy kinswoman, she also hath conceived a son in her old age, and this is the sixth month to her who was called barren;
Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.
37 because nothing shall be impossible with God.'
Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”
38 And Mary said, 'Lo, the maid-servant of the Lord; let it be to me according to thy saying,' and the messenger went away from her.
Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.
39 And Mary having arisen in those days, went to the hill-country, with haste, to a city of Judea,
Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.
40 and entered into the house of Zacharias, and saluted Elisabeth.
Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.
41 And it came to pass, when Elisabeth heard the salutation of Mary, the babe did leap in her womb; and Elisabeth was filled with the Holy Spirit,
Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,
42 and spake out with a loud voice, and said, 'Blessed [art] thou among women, and blessed [is] the fruit of thy womb;
akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.
43 and whence [is] this to me, that the mother of my Lord might come unto me?
Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 for, lo, when the voice of thy salutation came to my ears, leap in gladness did the babe in my womb;
Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 and happy [is] she who did believe, for there shall be a completion to the things spoken to her from the Lord.'
Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”
46 And Mary said, 'My soul doth magnify the Lord,
Naye Maria akasema,
47 And my spirit was glad on God my Saviour,
“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.
48 Because He looked on the lowliness of His maid-servant, For, lo, henceforth call me happy shall all the generations,
Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.
49 For He who is mighty did to me great things, And holy [is] His name,
Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.
50 And His kindness [is] to generations of generations, To those fearing Him,
Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.
51 He did powerfully with His arm, He scattered abroad the proud in the thought of their heart,
Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52 He brought down the mighty from thrones, And He exalted the lowly,
amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.
53 The hungry He did fill with good, And the rich He sent away empty,
Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.
54 He received again Israel His servant, To remember kindness,
Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.
55 As He spake unto our fathers, To Abraham and to his seed — to the age.' (aiōn )
Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.” (aiōn )
56 And Mary remained with her about three months, and turned back to her house.
Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.
57 And to Elisabeth was the time fulfilled for her bringing forth, and she bare a son,
Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.
58 and the neighbours and her kindred heard that the Lord was making His kindness great with her, and they were rejoicing with her.
Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.
59 And it came to pass, on the eighth day, they came to circumcise the child, and they were calling him by the name of his father, Zacharias,
Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.
60 and his mother answering said, 'No, but he shall be called John.'
Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”
61 And they said unto her — 'There is none among thy kindred who is called by this name,'
Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”
62 and they were making signs to his father, what he would wish him to be called,
Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.
63 and having asked for a tablet, he wrote, saying, 'John is his name;' and they did all wonder;
Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.
64 and his mouth was opened presently, and his tongue, and he was speaking, praising God.
Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And fear came upon all those dwelling around them, and in all the hill-country of Judea were all these sayings spoken of,
Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.
66 and all who heard did lay them up in their hearts, saying, 'What then shall this child be?' and the hand of the Lord was with him.
Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.
67 And Zacharias his father was filled with the Holy Spirit, and did prophesy, saying,
Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:
68 'Blessed [is] the Lord, the God of Israel, Because He did look upon, And wrought redemption for His people,
“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.
69 And did raise an horn of salvation to us, In the house of David His servant,
Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.
70 As He spake by the mouth of His holy prophets, Which have been from the age; (aiōn )
Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu, (aiōn )
71 Salvation from our enemies, And out of the hand of all hating us,
kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 To do kindness with our fathers, And to be mindful of His holy covenant,
Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.
73 An oath that He sware to Abraham our father,
Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi
74 To give to us, without fear, Out of the hand of our enemies having been delivered,
tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,
75 To serve Him, in holiness and righteousness Before Him, all the days of our life.
kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.
76 And thou, child, Prophet of the Highest Shalt thou be called; For thou shalt go before the face of the Lord, To prepare His ways.
Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;
77 To give knowledge of salvation to His people In remission of their sins,
kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.
78 Through the tender mercies of our God, In which the rising from on high did look upon us,
Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,
79 To give light to those sitting in darkness and death-shade, To guide our feet to a way of peace.'
na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”
80 And the child grew, and was strengthened in spirit, and he was in the deserts till the day of his shewing unto Israel.
Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.